Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Serikali imeruhusu mashabiki wa soka kuhudhuria uwanjani kwa kuzingatia taratibu za afya, isipokuwa kwa mechi kubwa wataingia nusu.
Mei 21 Rais Magufuli alitoa tamko la kuruhusu michezo yote na shule kuendela kuanzia Juni 1, 2020 kwa kuwa #CoronaVirus imepungua nchini. Alizitaka Wizara ya Afya kuweka taratibu za kushangilia.
Michezo yote ilizuiliwa tangu mwezi Machi baada ya #kuthibitishwa maambukizi ya #CoronaVirus nchini.
----
Serikali imetoa mwongozo wa kufuata katika michezo ya Ligi Kuu za Soka Nchini ambazo zinatarajiwa kuanza Juni Mosi, 2020, hivyo ni muhimu kuzingatia na kwa yoyote atakayekiuka taratibu hizo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake - Dkt. Hassan Abbasi.
Katika kuzingatia Mwongozo wa Afya Michezoni, Serikali kupitia wizara zenya dhamana ya Afya na Michezo ilishatoa mwongozo wa mei 28, 2020 unaoelekeza hatua za kuchukuliwa katika kila hatua za kuendesha michezo nchini - Dkt. Hassan Abbasi.
Kuhusu mtindo wa uendeshaji wa Ligi za Soka, Serikali inaruhusu Ligi za Soka ambazo kikanuni timu zinatakiwa kucheza nyumbani na ugenini kwa kuzingatia kanuni na taratibu za kiafya - Dkt. Hassan Abbas.
Serikali imeridhia ligi zote zilizoruhusiwa kurejea kwa mashabiki watakaotaka kuhudhuria viwanjani waruhusiwe kwa taratibu za kawaida isipokuwa tu kwa mechi zitakazotathminiwa - Dkt. Hassan Abbasi.
===
Mei 21 Rais Magufuli alitoa tamko la kuruhusu michezo yote na shule kuendela kuanzia Juni 1, 2020 kwa kuwa #CoronaVirus imepungua nchini. Alizitaka Wizara ya Afya kuweka taratibu za kushangilia.
Michezo yote ilizuiliwa tangu mwezi Machi baada ya #kuthibitishwa maambukizi ya #CoronaVirus nchini.
----
Serikali imetoa mwongozo wa kufuata katika michezo ya Ligi Kuu za Soka Nchini ambazo zinatarajiwa kuanza Juni Mosi, 2020, hivyo ni muhimu kuzingatia na kwa yoyote atakayekiuka taratibu hizo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake - Dkt. Hassan Abbasi.
Katika kuzingatia Mwongozo wa Afya Michezoni, Serikali kupitia wizara zenya dhamana ya Afya na Michezo ilishatoa mwongozo wa mei 28, 2020 unaoelekeza hatua za kuchukuliwa katika kila hatua za kuendesha michezo nchini - Dkt. Hassan Abbasi.
Kuhusu mtindo wa uendeshaji wa Ligi za Soka, Serikali inaruhusu Ligi za Soka ambazo kikanuni timu zinatakiwa kucheza nyumbani na ugenini kwa kuzingatia kanuni na taratibu za kiafya - Dkt. Hassan Abbas.
Serikali imeridhia ligi zote zilizoruhusiwa kurejea kwa mashabiki watakaotaka kuhudhuria viwanjani waruhusiwe kwa taratibu za kawaida isipokuwa tu kwa mechi zitakazotathminiwa - Dkt. Hassan Abbasi.
===