bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Hatupo mbali sana na kombe la dunia kule kwa mzee Putin Russia Tumeona makundi ndo hayo tiyari yametoka huyu akipangwa na yule ili mradi burudani.
Zaidi ya burudani ya soka kiwanjani pia mashabiki nao wanatoa burudani tosha kuna wale dakika 90 wao ni kushangilia hata kama timu yao imepigwa goli kadhaa na kuna wale watukutu/wakorofi mnoo wao ni fujo mwanza mwisho.
Tulishuhudia pale Ufaransa kombe la mataifa Ya Ulaya mashabiki wa Soka wa Uingereza wakichapana ngumi kavukavu na wale wa Kirusi nusura Timu ya Taifa ya Urusi irudishwe Moscow kabla ya mashindano kwisha.
Kipindi cha Nyuma kidogo tulishuhudia Liverpool wakienda kucheza na club mmoja ya Uturuki kama sikosei Galatary mashabiki walichapana mnoo na mwishowe Vifo vilitokea.
Pale Italia San siro/Giusepe Meaza uwanja umepigwa nyaya kwa ajili ya kuzuia ukorofi wa mashabiki wa vilabu vya Inter Milan na Ac Milan.
Je tukienda kwenye Kombe la Dunia ni Mashabiki wa nchi gani wanahitaji Ulinzi wa ziada kutokana na utukutu wao???
Zaidi ya burudani ya soka kiwanjani pia mashabiki nao wanatoa burudani tosha kuna wale dakika 90 wao ni kushangilia hata kama timu yao imepigwa goli kadhaa na kuna wale watukutu/wakorofi mnoo wao ni fujo mwanza mwisho.
Tulishuhudia pale Ufaransa kombe la mataifa Ya Ulaya mashabiki wa Soka wa Uingereza wakichapana ngumi kavukavu na wale wa Kirusi nusura Timu ya Taifa ya Urusi irudishwe Moscow kabla ya mashindano kwisha.
Kipindi cha Nyuma kidogo tulishuhudia Liverpool wakienda kucheza na club mmoja ya Uturuki kama sikosei Galatary mashabiki walichapana mnoo na mwishowe Vifo vilitokea.
Pale Italia San siro/Giusepe Meaza uwanja umepigwa nyaya kwa ajili ya kuzuia ukorofi wa mashabiki wa vilabu vya Inter Milan na Ac Milan.
Je tukienda kwenye Kombe la Dunia ni Mashabiki wa nchi gani wanahitaji Ulinzi wa ziada kutokana na utukutu wao???