Mashabiki wa timu za Ulaya waliopo Afrika wamepatikanaje?

Mashabiki wa timu za Ulaya waliopo Afrika wamepatikanaje?

Chief...
Swali ni jepesi sana..!
Hao mashabiki wa Arsenal na Man Utd wamepatikanaje..?
Pia unataka kutuaminisha kuwa mtu aliyeanza kuangalia mpira mwaka 2010 ataishabikia Arsenal..?
Ahahaaaah..!
Acha utani aisee...
Kuna jamaa was Czechoslovakia alikuwa anaitwa Poborsky alikuwa na kina Patrick Berger walikuwa wanaupiga mwingi sana kombe LA ulaya 1996 hapo na tangazo maarufu LA I Feel good lalalalaaa na tangazo LA fegi ya aspen king size.... Aliposajiliwa man utd nikazidi kuipenda..ila nilianza kuipenda 1994 bimkubwa alienda kusoma mji Wa Manchester sasa kila akituma Zawadi nembo za united hapo nipo darasa la tatu...
 
Soka la ulaya lilianza kupendwa baada ya kuanza kuonyeshwa kwenye setilite TV na kuanza kuonekana Africa. Kwa EPL timu kubwa zilikuwa ni United, Liverpool, Aston Villa, Nottingham Forest, Westham na Spurs.

Arsenal, Chelsea, na timu nyingi za kawaida zilizokuwa zikitoka nje ya london hazikuwa tishio kabisa, yaani zilikuwa za kawaida kabisa kama ilivyo kwa sasa timu kama New castle, everton,nk.

Ila kwa hapa Africa soka la ulaya hususani england lilikuja kushika wengi mwishoni mwa miaka ya 90 baada ya Arsenal chini ya meneja Arsene wenger kumsajili kiungo/mshambuliaji wa kiNageria Nwanko Kanu, ambaye alivuma sana kwenye mashindano ya Olimpic ya Atalanta mwaka 1996 nchini marekani.

Kwa kifupi, mtu aliyelitangaza soka la uingereza barani Africa kwa kiwango kikubwa ni Nwanko Kanu. Na % kubwa ya mashabiki wa mwanzo wa Arsenal chanzo kikubwa kilikuwa ni Kanu. Nakumbuka kumsikia mtu m1 kwenye kibanda umiza akisema anahamia Pouthmous baada ya kanu kusajiliwa huko akitokea Asernal.

Kwa chelsea, City, nyingine sijui nini kiliwavutia.
 
Back
Top Bottom