Masheikh kurundikwa Magereza bila kufunguliwa kesi Mahakamani nchini Tanzania, nini hatma yake?

Masheikh kurundikwa Magereza bila kufunguliwa kesi Mahakamani nchini Tanzania, nini hatma yake?

Dua lao limesikiwa watakuwa huru.Mkapa hayupo commando ndo hivyo kapigwa upofu.
 
Hawa waendelee kupiga duna la mwisho mwisho wanatoka muda si mwingi
Watoke nafasi zao zichukuliwe na wasiojulikana na mabosi zao nao waoze ndani kama miaka 9 hivi wakisubiria ushahidi kukamilika
 
Afadhali kwamba wapo mikono ya serikali kwa kuwa ni serikali lakini kama wangefanikiwa kuyafanya hayo matendo ya kigaidi walengwa wake wangekuwa makaburini hivyo mshukuru sana JPM na serikali kwa ujumla kwamba wapo hai.
 
mhe Rais HUSSEIN MWINYI , naona ni mtu RAHIIM. , hili aliangalie kwa macho ya mbaaali, kwani walioko ndani kama wana kesi ya kujibu wawapeleke MAHAKAMANI. kuliko0 kuwaacha tu hili haliko sawa. NCHI HII NI YETU SOTE MAADAMU KUNA WIZARA YA SHERIA NA UTAWALA BORA , watusaidie.
Sio Rahimu tu ni Waislamu wwnzake. Asiichukue hiyo dhima akawaacha huko magereza.
 
[Kamanda, hujui usemalo. Hawa ni Uamsho, magaidi wa kimataifa. Kwanza, walifungwa na Rais Kikwete, Islamu, siyo Magufuli. Walikamatwa na Rais Karume, Islam, siyo Kikwete. Pili, magaidi ni magaidi, mahakama yao huwa ni tofauti. Kuna Uamsho wa Pemba alihusika kulipua ubalozi wa Marekani pale Kinondoni mwaka ule, hadi leo yuko jela Guantanamo hajapelekwa mahakamani na Obama, Islam.

Kiongozi wao Usama bin Laden hakupelekwa mahakamani pia, ndiye amgekuwa shahidi wa kwanza. Tatu, ugaidi ni jambo la kimataifa, jambo la Muungano. Kuletwa Tanganyika kushitakiwa ni sawa kwa sababu polisi na makada wa CCM waliochinjwa mashimoni tanga na stakisheri police station ukonga, na baadaye kibitilindi ni raia wa Tanganyika, ni sawa kushitakiwa tanganyika.

Unaulizwa tumelipuliwa mara ngapi? Hilo ndiyo jibu lako, lizingatie. Tangu bin Laden alipouliwa na Obama, Islam, Marekani nao pia hawajalipuliwa. Ukiwaachia masheikh wako tutalipuliwa tena. Futa dhana ya dini, Mungu si gaidi.
 
Hakuna masheikh walioko ndani!! Walioko ndani ni watuhumiwa wa ugaidi! Utuhumiwa huo hauhusiani kabisa na dini yao wala Imani yao. Magereza yote tana wafungwa kwa mujibu wa makosa yao na si kwa mujibu wa dini zao au nafasi zao kwenye dini. Wanaweza kuwa wakristo, waislamu au wapagani.
 
Swala lako ni zuri sana tatizo lako umeingiza UDINI mno na kujifanya waislamu mnaonewa kwa kila jambo kitu ambacho si kweli kabisa.Na kwa kuwa umelileta kidini zaidi ufumbuzi wake utakuwa mgumu sana sana.
 
Serikali inashikilia suspected terrorists. Dini zao sio relevant; hata wakibadili dini zao leo hakuna kitakachobadilika.

Suspected terrorists wanahitaji kibano mwanzo mwisho. Katika vita dhidi ya terrorism ni sawa kuwaumiza wachache ili wengi wapone! Ukiwachekea nyani utavuna mabua. Boko haram na Al-Shabaab walianza hivyo hivyo; walichekewa na hatimaye nguvu yao ikawa haidhibitiki!
 
Tuombe Allah muda si mwingi Bi: Samia atakapo kuwa up to the top ili suala litaisha. Tuseme inshanlah!
Jinga kabisa wewe.
Na hilo neno halikusaidii lolote.

Huyo Bi Samia ni pambo tu kama mapambo mengine Magufuli baba lao
 
Serikali inashikilia suspected terrorists. Dini zao sio relevant; hata wakibadili dini zao leo hakuna kitakachobadilika.

Suspected terrorists wanahitaji kibano mwanzo mwisho. Katika vita dhidi ya terrorism ni sawa kuwaumiza wachache ili wengi wapone! Ukiwachekea nyani utavuna mabua. Boko haram na Al-Shabaab walianza hivyo hivyo; walichekewa na hatimaye nguvu yao ikawa haidhibitiki!
Ingekuwa baba ako yupo ndani usingeongea huu utumbo
 
Lakini ndugu kwanini usimlaumu kikwete aliyewaacha ndani uje umlaumu magufuli aliyewakuta ndani na unajuwqa ni maelekezo gani kapewa na kikwete kuhusu ni hatari gani waliyonayo hao mashehe? hebu anza na aliyewaweka ndani kabla ya kumlaumu aliyewakuta tena aliyewaweka ni muislamu mwenzao ndo ujue hao jamaa ni hatari kiasi gani kwa nchi
 
Umeeleweka vizuri sana mkuu wenzetu wanaangalia upande mmoja tu hawaangalii mazara ya hawa jamaa
 
Back
Top Bottom