Mashindano ya Ajabu Yenye Kushangaza.

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,265
Katika kujiburudisha, binadamu wamevumbua michezo/mashindano ambayo kwa watu wengine
ni kitu cha kustaajabisha na kushangaza. Fuatilia mashindano/michezo hii hapa chini ushangae
kiasi!

1 Mashindano/Mchezo wa 'kuvaa' nyuki. Mashindano haya hufanyika nchini china kila mwaka.Washiriki hushindana
kuvaa nyuki wengi iwezekanavyo.Mshindi ni yule liyevaa nyuki wengi.Mmoja alishinda kwa kuvaa nyuki 350,000 walokuwa na uzito wa kilo 47.

Mshiriki kavaa nyuki

2.Mashindano ya Watoto kutambaa. Hii pia hufanyika china kwa kushindanisha watoto walioko
kwenye umri wa kutambaa.Watoto hupangwa kwenye mstari kisha kuamriwa kutambaa kuelekea
sehemu maalumu iliyochaguliwa. Shindano moja lililopo kwenye rekodi lilishirikisha watoto 451
Watoto kwenye mbio za kutambaa

3.Kutupa Simu. Mashindano haya hufanyika huko Finland kwa ufadhili wa makampuni ya simu.
Washiriki hushindana kutupa mbali simu zao kuukuu na anayeweza kutupa simu yake mbali zaidi ya wengine
ndiye mshindi na huzawadiwa simu mpya.

Simu hiyo inavurumishwa


Itaendelea...........
 
[h=3]Wife Carrying Competition(mashindano ya kubeba mke)[/h]Uhusisha wanaume kubeba wake zao kwa umbali wa 253.5m.Umbali huo unajumuisha maeneo ya nchi kavu na majini.Mshindi hufanikiwa kupata simu na wake zao hupata bia(pombe).Shindano hili huifanyika kila mwaka nchini Finland
 
Ewaaa Tyta, asante kunisaidia! Kipengele hiki cha wife carrying kilikuwa kwenye visa vyangu.
Picha nyingine hii hapa:
 
Mashindano ya ajabu na ya kushangaza (Inaendelea sehemu yaII)

4.Ngono ya Kufikiria. Mashindano haya hufanyika nchini Marekani.Wanachotakiwa
kufanya, washiriki (awe me au ke) hujifanya yuko kwenye tendo la ngono na
hivyo kuonesha manjonjo yote yafanywayo kwenye tendo lote la ngono. Mshindi
ni mshiriki yule aliyeonesha uhalisia wa jinsi hilo tendo linavyofanywa.
Mshiriki mwanamke akionesha jinsi ngono inavyofanywa.


Mshiriki wa kiume akionesha manjonjo ya ngono.Wenyewe wanaita 'air sex'

5. Mbio za kitanda. Mbio hizi ni maarufu mjini Yorkshire, Uingereza na zilianza mwaka 1965 washiriki wakiwa ni
wanajeshi tu ila baadaye watu wengine waliruhusiwa kushiriki. Kila kitanda kinachokimbizwa kina washiriki 5 mmoja hulala kwenye hicho kitanda, waliobaki hukisukuma kwa mbio kali.

Mbio za kitanda.

6.Michuano ya Ndevu. Hii hufanyika kila baada ya miaka 2 huko mjini Brighton
Uingereza. Wenye ndevu ndefu na zilitotunzwa vizuri hushindanishwa.

Mshiriki wa michuano ya ndevu.
Itaendelea...........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…