Tumerudi nyuma enzi za Malinzi za taifa stars maboresho. Malinzi na wenzake wakawaza jinsi ya kuiboresha taifa stars ni kukusanya wachezaji wasiochezea timu za ligi kuu wenye vipaji kutoka mikoani na kuwaweka kambini eti kutengeneza timu ya taifa. Ilifeli vibaya mno!
Mchezaji mpira ni zaidi ya kujua control, kupiga pasi na chenga. Mchezaji pia anatakiwa awe na stamina, makini, ajue mifumo (formations) yaani akiambiwa tunacheza 4 3 3 aelewe n.k na hivi vinapatikana kwa kiasi kikubwa kwa klabu zetu kubwa kwa maana ndizo zina miundo mbinu angalau mizuri na makocha wa viwango.
Kwa hiyo asilimia kubwa wachezaji wa klabu kubwa wana vitu vingi kuliko wa klabu ndogo na hii ni kwa dunia yote.
Siasa ziachwe simba na yanga hazikwepeki, ili zikwepeke nyanyueni akina ihefu, gwambina ,biashara utd n.k ziwe level moja na akina Tp mazembe, Al ahly, Mamelod sundowns la sivyo ni kujidanganya tu.