Mashine za kutotolesha mayai (Incubators): Upatikanaji wake, aina zake, matumizi na ushauri

Mdau hizo made in tanzania zina guarantee ya mda gan? Mimi nahitaji za mayai 1000 na pia sehemu ambayo naweza kupata hayo mayai please jibu bajeti kuanzia 2m/
Habari, Naulizia incubators za solar naweza kupata wapi. Nipo Dodoma vijijini
 
USHAURI
Kweli kuna aina nyingi za incubator
Kama mtoa ushauri mmoja alivyo eleza hapo juu ametoa maelezo mazuri sana na kwa kina sana.

Matatizo kila kifaa kina matatizo hivyo nakushauri ukipata incubator hata zilizotengenezwa hapa nchini ni nzuri sana kwa maana zilizotengenezwa hapa mafundi wapo kama kuna matatizo wanaweza kukutatulia kwa haraka zaidi.

Hata mimi natengeneza incubator tena ni nzuri na imara sana. Kwa mawasiliano kama utapenda kuja kuziona na ushauri zaidi.
0713 852 296
0755 450 970
 
Habari, Naulizia incubators za solar naweza kupata wapi. Nipo Dodoma vijijini

Piga number hiyo
0713 852 296
0755 450 970
0787 309 396

Ni watengeneza wa incubator zinazotumia SOLAR NA GAS
Matumizi ya uendeshaji ni madogo sana kwa mwezi ni gharama 20,000/= tu
Ufanisi wake 98%
Warranty mwaka mmoja
Mafundi wapo hizo ni made in Tanzania
Tupo Dar es salaam
Ubungo Riverside




 
mkuu kitu ambacho sijaelewa hizi machine zinafanyeje kazi yani mfano kuku wa kienyeji akitaga tu naweza kuweka kwenye machine hiyo na kifaranga kikatoka au inakuwaje?
embu naomba nieleweshe kifaranga kinatokaje hapo au ni yai la aina gani linatoa kifaranga
 
Unakusanya mayai idadi ya uwezo wa mashine mfano kuna za mayai 42 mpaka 8000. Hivyo yakifika idadi ya uwezo wa mashine unayaweka kwenye mashine(fuatilia jinsi ya kuweka kweny kijitabu cha maelezo) then unaweka maji na kuunganisha kwenye umeme ili kupata joto na unyevunyevu.

Joto na unyevunyevu kwa kipimo stahiki nadhan unaregulate wewe then baada ya siku 21 unapata vifaranga vyako kulingana na mayai uliyoweka LAKIN VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA otherwise mayai yote yataharibika
 
nashukuru sana mkuu nilikuwa sijui, asante,
na je mayai yakiwa chini ya hapo itakuwaje?
 
nashukuru sana mkuu nilikuwa sijui, asante,
na je mayai yakiwa chini ya hapo itakuwaje?
Yasizid idadi husika lkn yakiwa chini sawa tu japo kibiashara ni hasara maana umeme ni uleule utakaotumika pia muda ni uleule wa siku 21
 
asante mkuu
Yasizid idadi husika lkn yakiwa chini sawa tu japo kibiashara ni hasara maana umeme ni uleule utakaotumika pia muda ni uleule wa siku 21
nimekupata vizuri ubarikiwe sana
nimekupata u
 
ni
faida gani naweza pata nikiwa na hizo mashine?
 
ni

faida gani naweza pata nikiwa na hizo mashine?
Bushland faida zipo nying tu mfano ni kupata vifaranga wengi kwa wakati mmoja either uwauze au uwakuze na kuuza wakiwa wakubwa, pia unaweza fanya biashara ya kutotoleshea vifaranga vya wateja wako yaan wanaleta mayai na wewe unatotolesha kwa 500 kwa yai.

Mashine ya mayai 1000 mara 500 una 500000 kwa siku 21 tu za mayai kuanguliwa
 
nashukuru sana nikiwa na shida nyingine ntakuja tena,
barikiwa
 
Wakuu kama una mashine za kuangulia mayai unaweza pata kutoka kwangu.

1. Spare parts zote za incubators


2. Trays za kuwekea mayai kwenye mashine




3. Tray za kutotoleshea


4. Kufanya repair za mashine mbovu/iliyo haribika
Weka mawasiliano kwa ajiri ya kukutafuta kupata hizo spare parts mkuu.
 
Habari?
Wanajamvi,nimenunua mashine ya kutotolesha vifaranga hivyo napata changamoto ya malighafi yaan MAYAI. Hivyo nanunua mayai YA KIENYEJI yawe yanatokana na kuku halisi wa KIENYEJI.

Mwenye nayo au anaemjua supplier yeyote anayeweza niuzia mayai 500 kila mwezi kwa miezi 4 tuwasiliane PM kwa makubaliano ya bei na mengineyo.
Mimi napatikana Mbeya na vizuri kama supplier atakuwa mbeya na maeneo ya jirani yaani sumbawanga, tunduma, songwe, mbalali, makambako, njombe, iringa na morogoro

Asanteni!.
 
mkuu nakuja pm mara moja
 
Wakuu habariiii...

Naomba mnipe utaalam wa kutengenezea incubator jamani natamani sana kuwa na kuku wa kutosha ila ndoto inanifia pua kwa kutokuwa na hii mashine na uwezo wa kununua dukani ni mfinyu kidogo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…