Mashirika ya kijasusi duniani

Night shadow

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2015
Posts
574
Reaction score
1,098
Mimi si mtaalamu sana wa mambo haya,ndo mana napenda kuuliza maswali machache juu ya mashirika haya.

Tayari nishasikia machache kuhusu CIA,MOSSAD na hapa kwetu TISS.

Ningependa kujua mashirika haya huwajibika kwa nani? je ni rais? ama kitengo gani katika serikali? na jee uhusiano wa vitengo hivi pamoja na majeshi ya nchi husika huwaje?

Na jee vitengo hivi huwa havipenyezi watu wake katika majeshi? nakama hupenyeza kwanini baadhi ya serikali hupinduliwa wakati vitengo hivi vipo?


KAMA WATU MSIOJULIKANA MTAUDHIKA KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE..,IM SORRY.
 
Ngoja wataalamu waje ila The bold angekuwepo angekujibu hili swali fresh
 
Intelligence apparatuses zinaweza pia kutumika katika shughuli za kuhujumu mipango ya maadui pamoja na kujikinga na njama za maadui dhidi ya maslahi mapana na taifa husika. Mfano. Marekani wanavyojaribu kuwauwa scientists wa Iran for the sake of halting the believed Nukes programme.
 
KWa tz TISS huwajibika kwa mkulu na mkurugenzi wao na si tz tu ni katika mataiga mengi duniani.mfano uingereza wanaripoti kwa malkia na mkutugenzi na kwa udogo sana waziri mkuu.kuhusu mapinduzi ni pale ambapo wote wanakuwa wechoshwa na uongozi uliopo mf.tunisia na misri.lkn pia usisahau mapinduz mengi africa hufadhiliwa na mataifa makubwa ambayo kiteknolojia wako juu hivyo hupanga lwa weredi bil kujulikana.
 
CIA kwa mfano wanaweza kutumika kufuatilia mienendo ya viongozi wa marekani wanapokuwa nje ya taifa lao huwa wanaenda wapi na wanaonana na nani.

Monitoring diaspora activities. To be honest kazi za idara za ujasusi huwa ni nyingi sana. It might take more than 5 hours to give detailed explanations on this
 
Upo sawa
 
Tanzania hakuna Shirika la Kijasusi kuna Idara ya Ujasusi inayofanya kazi chini ya Taasisi ambayo ni Ofisi ya Raisi.
Kivitendo hiyo Idara ya Usalama wa Taifa inawajibika kwa Raisi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hivyo CCM na Raisi Magufuli wakiamua kufutilia mbali hao Usalama wa Taifa wanaweza na hakuna atakayewazuia Kisheria. Sema kiuhalisia CCM hawezi kufanya hivyo kwasababu huo ndiyo utakuwa mwisho wao pamoja na familia zao.

Hili hata Nyerere aliliweka bayana: "The Government is an Instrument of the Party" hapa alijumuisha vyombo vya Serikali kama Bunge, Mahakama na hata Jeshi. Tena mshukuru siku hizi mambo yamebadilika sanaa, miaka ya nyuma unaweza kukuta mwana-CCM kama Mzee Philip Mangula au Mzee Makamba anawaamrisha na kuwatumia hawa TISS hovyo kabisa.

Kuna miaka ya nyuma huyu Mzee Kingunge na Marehemu Mzee Siyovelwa pamoja na TISS walitendaga madhambi kule Iringa sitaki hata kukumbuka. Yaani mfumo huu uliopo ni mbaya na unachangia kurudisha taifa nyuma. Wamechukua mifumo ya:
  • Communist Party of the Soviet Union (CPSU) na The KGB.
  • Communist Party of China (CPC) na Ministry of State Security.
  • Communist Party of Cuba na Direccion General de Inteligencia.
Sasa kwenye hii mifumo Chama kikivamiwa na mamluki basi Intelijensia ya nchi lazima iharibike tu.
Mfano Mzuri kabisa kuwahi kutokea:
Urusi ya Kisovyeti na Ujanja wake wote ule walikuja Wanachama wa hovyo hovyo wa CPSU wakina Mikhail Gorbachev na Boris Yeltsin wakaharibu kila kitu mle ndani. KGB iliparanganyika vibaya sana kisa tu ilikuwa inaripoti kwenye Politburo ya Chama cha Kikomunisti cha Urusi.
 
Duuuh sikuwezi
 
Sasa kwenye hii mifumo Chama kikivamiwa na mamluki basi Intelijensia ya nchi lazima iharibike tu.


Malcolm Lumumba katika ubora wako.. One of the best comment regarding on the so called watu wasiyojulikana hata kama kila mtu kamuona mchana kweupe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…