Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 239
• Zacheleweshwa benki Dar zisivuruge kura Dpdoma
• Ni fedha za kifisadi katika uchaguzi wa Wazazi
Na waandishi wetu Dar na Dodoma
Raia Mwema Juni 10 – Juni 16, 2009
MAMILIONI ya fedha zilizokuwa ziingizwe kwenye harakatui za kusaka ushindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa jumuiya ya wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), wiki ilyopita zimezua utata baada ya vyombo vya dola kuhakikisha haziingii Dodoma kuharibu uchaguzi, Raia Mwema limefahamishwa.
Imefahamika kwamba fedha hizo zilizozuiwa na watu walioelezwa kuwa ni "maalumu" zilikuwa ziingizwe kwenye akaunti iliyopo benki moja maarufu nchini, tawi la Dodoma.
Zilikuwa zimepangwa kugawanywa kwa wajumbe wa mkutano wa uchaguzi. Wagombea katika uchaguzi huo walikuwa ni balozi Athumani Mhina, Abdallah Bulembo na Esther Nyawazwa.
Habari zilizopatikana zinasema baada ya kampeni kuonekana kuwa ngumu kwa pande zote, mkakati wa mwisho wa mgombea mmoja ulikuwa ni kutumbukiza pesa (Sh milioni 400) ambazo zilikuwa ziingizwe kwenye akaunti moja ya benki hiyo tawi la Dodoma ili zigawiwe; hivyo kumalizia kazi ya kuwaweka sawa wapiga kura, na hatimaye kufanikisha ushindi wa mgombea husika.
Hata hivyo, inaelezwa kuwa nyendo za kundi la mgombea husika zilikuwa zikifuatiliwa kwa karibu na vyombo vya dola vilivyohakikisha fedha hizo haziingii kwenye akaunti hiyo kutoka Dar es Salaam ili zisigawanywe kwa wapiga kura Dodoma na kuvuruga uchaguzi.
"Watu walikuwa wamejipanga vizuri sana, sijui kwa maelekezo ya nani, lakini walikuwa makini sana kuhakikisha kasi ya mbinu chafu haitawali uchaguzi. Kwa hiyo, wakajua kuwa kuna fedhazimeingizwa kutoka kwa kundi fulani linaloshirikisha wanasiasa na wafanyabiashara wenye tatizo la kimaadili… ni fedha nyingi kwa hiyo kazi ikafanyika kuwa ni lazima kuhakikisha hizo fedha hazitoki benki kwa wakati uliokusudiwa na wahusika wa kundui hilo ili kwenda kugawa rushwa," alisema mtoa habari hizo.
"Sasa hawa watu na hasa viongozi wao katika kufanikisha mkakati huo walikwenda benki kuchukuwa fedha lakini huko walikutana na kikwazo, fedha hazikutoka kwa wakati…wakahangaika lakini hawakufanikiwa.
"Wakaamua kwenda kumuona meneja kujua kuna tatizo gani, huko wakakwama wakiwa wamejibiwa kwamba kulikuwa na matatizo ya kawaida ya shughuli za kibenki hivyo fedha hizo zingechelewa kuchukuliwa," kinasema chanzo cha habari za mkakati huo uliofeli.
Habari ndani ya vyombo vya dola vimethibitisha kwamba wahusika waliotoa fedha hizo jijini Dar ves Salaam kwa kutumia uzoefu wao katika sekta ya fedha walikuwa wameweka mkakati wa kukiuka taratibu za kibenki ili fedha hizo ziwahi kuingia katika akaunti iliyokusudiwa mjini Dodoma, lakini baada ya dola kuingilia kati fedha hizo zikalazimika kupitia ‘chekeche' la kawaida la fedha.
"Kwa kawaida fedha nyingi kama hizo (milioni 400) haziwezi kupitishwa kwa haraka haraka katika mfumo wa kibenki hasa kama mmoja wa wahusika hana kawaida ya kupokea ama kuingiza fedha nyingi kiasi hicho, kwa hiyo ni lazima ufuate utaratibu wa kuzingatia Sheria ua Uthibiti wa Fedha Haramu kupitia kitengo cha Financial Intelligence Unit (FIU), na ndicho kilichowaponza hao jamaa," kinaeleza chanzo cha habari ndani ya serikali………..
………habari zaidi ziko katka Raia Mwema ya leo UK wa 3.
• Ni fedha za kifisadi katika uchaguzi wa Wazazi
Na waandishi wetu Dar na Dodoma
Raia Mwema Juni 10 – Juni 16, 2009
MAMILIONI ya fedha zilizokuwa ziingizwe kwenye harakatui za kusaka ushindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa jumuiya ya wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), wiki ilyopita zimezua utata baada ya vyombo vya dola kuhakikisha haziingii Dodoma kuharibu uchaguzi, Raia Mwema limefahamishwa.
Imefahamika kwamba fedha hizo zilizozuiwa na watu walioelezwa kuwa ni "maalumu" zilikuwa ziingizwe kwenye akaunti iliyopo benki moja maarufu nchini, tawi la Dodoma.
Zilikuwa zimepangwa kugawanywa kwa wajumbe wa mkutano wa uchaguzi. Wagombea katika uchaguzi huo walikuwa ni balozi Athumani Mhina, Abdallah Bulembo na Esther Nyawazwa.
Habari zilizopatikana zinasema baada ya kampeni kuonekana kuwa ngumu kwa pande zote, mkakati wa mwisho wa mgombea mmoja ulikuwa ni kutumbukiza pesa (Sh milioni 400) ambazo zilikuwa ziingizwe kwenye akaunti moja ya benki hiyo tawi la Dodoma ili zigawiwe; hivyo kumalizia kazi ya kuwaweka sawa wapiga kura, na hatimaye kufanikisha ushindi wa mgombea husika.
Hata hivyo, inaelezwa kuwa nyendo za kundi la mgombea husika zilikuwa zikifuatiliwa kwa karibu na vyombo vya dola vilivyohakikisha fedha hizo haziingii kwenye akaunti hiyo kutoka Dar es Salaam ili zisigawanywe kwa wapiga kura Dodoma na kuvuruga uchaguzi.
"Watu walikuwa wamejipanga vizuri sana, sijui kwa maelekezo ya nani, lakini walikuwa makini sana kuhakikisha kasi ya mbinu chafu haitawali uchaguzi. Kwa hiyo, wakajua kuwa kuna fedhazimeingizwa kutoka kwa kundi fulani linaloshirikisha wanasiasa na wafanyabiashara wenye tatizo la kimaadili… ni fedha nyingi kwa hiyo kazi ikafanyika kuwa ni lazima kuhakikisha hizo fedha hazitoki benki kwa wakati uliokusudiwa na wahusika wa kundui hilo ili kwenda kugawa rushwa," alisema mtoa habari hizo.
"Sasa hawa watu na hasa viongozi wao katika kufanikisha mkakati huo walikwenda benki kuchukuwa fedha lakini huko walikutana na kikwazo, fedha hazikutoka kwa wakati…wakahangaika lakini hawakufanikiwa.
"Wakaamua kwenda kumuona meneja kujua kuna tatizo gani, huko wakakwama wakiwa wamejibiwa kwamba kulikuwa na matatizo ya kawaida ya shughuli za kibenki hivyo fedha hizo zingechelewa kuchukuliwa," kinasema chanzo cha habari za mkakati huo uliofeli.
Habari ndani ya vyombo vya dola vimethibitisha kwamba wahusika waliotoa fedha hizo jijini Dar ves Salaam kwa kutumia uzoefu wao katika sekta ya fedha walikuwa wameweka mkakati wa kukiuka taratibu za kibenki ili fedha hizo ziwahi kuingia katika akaunti iliyokusudiwa mjini Dodoma, lakini baada ya dola kuingilia kati fedha hizo zikalazimika kupitia ‘chekeche' la kawaida la fedha.
"Kwa kawaida fedha nyingi kama hizo (milioni 400) haziwezi kupitishwa kwa haraka haraka katika mfumo wa kibenki hasa kama mmoja wa wahusika hana kawaida ya kupokea ama kuingiza fedha nyingi kiasi hicho, kwa hiyo ni lazima ufuate utaratibu wa kuzingatia Sheria ua Uthibiti wa Fedha Haramu kupitia kitengo cha Financial Intelligence Unit (FIU), na ndicho kilichowaponza hao jamaa," kinaeleza chanzo cha habari ndani ya serikali………..
………habari zaidi ziko katka Raia Mwema ya leo UK wa 3.