Masikini Azam FC, nini hiki kinatokea msimu huu?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Nashuhudia hapa game ya Azam FC na Namungo. Dakika ya 91 Azam ikiwa mbele kwa goli 2-1. Zikiwa zimeongezwa dakika nne Namungo wakapata kona. Dakika ya 94 Kikoti anapiga kona maridadi kabisa Steven Seyi anasawazisha. Sey anakera sana, anachomekea halafu anawapungia mkono.

FT Azam Fc 2- 2 Namungo

Namuona Nado analia, wachezaji wa Azam FC wamelala chini hawana nguvu. Mpaka nimeshikwa simanzi kwa huruma. Ikumbukwe Azam Fc toka wafungwe na Utopolo Le Dera. Hawajashinda mechi yeyote. Biashara, Gwambina na leo Namungo zote droo.

My Take
Bado Utropolo
 
Ni sawa wako kwenye form mbovu kwa sasa, lakini bado wana nafasi ya kufuta makosa na kurudi vizuri tena kama walivyoanza msimu... Pole kwao ndio mpira ulivyo.
 
Kwa heri azam umekata tamaa endelea kufanya mazoezi kwa ajili ya msimu ujao na usishuke daraja,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…