Masikini wapigwe marufuku kunywa kulewa?

Masikini wapigwe marufuku kunywa kulewa?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Pombe na sigara ni kati ya bidhaa zinazoingizia nchi hela nyingi kwa njia ya kodi. Ingawa ni bidhaa iileteayo Serikali ukwasi mkubwa, ina madharabhasi kwa baadhi ya watu hasa masikini.

Ilishawahi kutokea, na hata sasa hali inaweza ikawa hivyo kwa baadhi ya maeneo, ambapo:

1. Mwanaume anaenda kufurahia bia baa wakati watoto wake wana utapiamlo

2. Wengine hushindwa kufanyq kazi kwa sababu ya ulevi

3. Maeneo mengine unaweza ukamkuta mtu kalala njiani kwa sababu ya ulevi. Kwamba, pengine alikuwa na hela ya kulewea tu lakini ya usafiri wa kumfikisha kwake hakuwa nayo

4. Masikini anapokuwa mlevi ni familia yake ndiyo inayoteseka

5. Wengine wakishakuwa waraibu wa pombe huwa radhi kutokula ili hela ya chakula aitumie kwa pombe

Labda inaweza ikawa msaada endapo utaratibu utawekwa kuwa watu wa kipato fulani pekee ndiyo watakaoruhusiwa kunywa pombe? Itasaidia? Huo utaratibu unaweza kuwahamisha masikini kufanya kazi kwa bidii ili hatimaye na wao wapewe leseni ya kunywa pombe?
 
Kwahiyo masikini unamshauri anywe kinywaji Gani as to keep his or her life safe
 
Nchi ambayo unauziwa pombe ya 43% kwa elfu 2, ni nchi ambayo imekosa kabisa tumaini kwa masikini ila kuwalewesha wasahau shida zao.

Nikikumbuka viroba vilifungiwa halafu kwa sasa kuna double kick,smart ginn,valuer,jobo nachoka kabisa.

Kuna katazo la mitandao ya video za ngono ila sio vipombe vikali.
 
Pombe na sigara ni kati ya bidhaa zinazoingizia nchi hela nyingi kwa njia ya kodi. Ingawa ni bidhaa iileteayo Serikali ukwasi mkubwa, ina madharabhasi kwa baadhi ya watu hasa masikini.

Ilishawahi kutokea, na hata sasa hali inaweza ikawa hivyo kwa baadhi ya maeneo, ambapo:

1. Mwanaume anaenda kufurahia bia baa wakati watoto wake wana utapiamlo

2. Wengine hushindwa kufanyq kazi kwa sababu ya ulevi

3. Maeneo mengine unaweza ukamkuta mtu kalala njiani kwa sababu ya ulevi. Kwamba, pengine alikuwa na hela ya kulewea tu lakini ya usafiri wa kumfikisha kwake hakuwa nayo

4. Masikini anapokuwa mlevi ni familia yake ndiyo inayoteseka

5. Wengine wakishakuwa waraibu wa pombe huwa radhi kutokula ili hela ya chakula aitumie kwa pombe

Labda inaweza ikawa msaada endapo utaratibu utawekwa kuwa watu wa kipato fulani pekee ndiyo watakaoruhusiwa kunywa pombe? Itasaidia? Huo utaratibu unaweza kuwahamisha masikini kufanya kazi kwa bidii ili hatimaye na wao wapewe leseni ya kunywa pombe?
Mtoa post analogic lakini jinsi ya uwasilishaji ndio tatizo lakini pombe inapozidi ni hatari kati ya watu 10 ambao ambao wanaweza kunywa kias au kupangilia mambo yao wakiwa wamekunywa ni 1
 
India pombe huuzwa sehemu maalumu Tu kiingilio ni buku 5 ndo uingie haiuzwi hovyo2 kwa kila mtu
 
Back
Top Bottom