Ushimen
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 40,828
- 99,523
Sitaki kukataa kwa hayo uyasemayo mkuu.Hata sisi wote! mimi sitaki kumuhukumu Diamond wala Baba yake, sababu na kuna cha ufa baina yao wanazijua wao, ila sisi wengine tutafakari na tujipime tungefanya nini kama hali hii ingetukuta sisi? Je ningefunga macho, masikio na mdomo na kupandisha vioo tukanyamaza au tungejiongeza tukasamehe na kusonga mbele?! Maana No situation is parmanent; leo Diamond yuko hivi, rich and famous! je kesho tunajua Diamond atakuwaje?
Lakini ebu tujaribu kulitazama hili la Diamond kwa upana na katika ngazi ya kifamilia.
Pili tusiwe wepesi wa kumlaumu Diamond kwamba hajamsamehe baba yake.
1- Kwani nani ajuaye kwamba Diamond hampi baba yake msaada?
2- Je uliwahi kusikia tuhuma za kwamba mzee ni mtumiaji mzuri wa vilevi na totoz kila pale anapo pewa pesa?
3- Je uliwahi kusikia Diamond akisema hampendi au ana uadui na baba yake?
4- Je uliawahi kusikia baba wa Diamond akisema kosa alilo mkosea mwanae hata aombe kusamehewa na mwanae?
5- Je uliwahi sikia baba wa Diamond akimtaja Queen Darlin kwamba hamsaidii pia?
6- Je kwanini baba Diamond anakimbilia kwenye media kujieleza au kutaka kuzungumzia mambo ya kifamilia kwa kujifanya yeye anaonewa au yeye ni msafi?
7- Je kila akiugua na kwenda hospital waandishi wa magazeti ya shigongo huota ndoto na kumfuata huko ili wamchukue picha?
Mwisho naomba niseme kwamba hapa hakuna la kujifunza kupitia huyu baba wa Diamond. Na ninaweza sema kwamba mzee anatumika na Shigongo ili kutengeneza habari.
Pia kwa baba mwenye hekima na busara hawezi kwenda tatua matatizo ya kifamilia kwenye media.[emoji135] [emoji135] [emoji135]