Maskini hawakujuaaaaaaaaaaaa

Maskini hawakujuaaaaaaaaaaaa

Poleni sana , nashauri waendelee kulea mimba then ndoa hapo hakuna namna nyingine, ukimwi noma bora tu wasonge mbele hivyo hivyo !
 
Poleni vijana.

LA VIE EST DIFFICILE LA-BAS.
[TABLE="class: Corpus"]
[TR="class: Headerrow"]
[TD="class: Headerarea"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Poleni sana kijan na bintikatika suala kama hilo.

kuna umuhimu wa kulaumu kidogo wazazi kwa kutowapa watoto wao at least background ya vizazi angalau viwili au vitatu nyuma. ngewasaidia kidogo. Nadhani haya ni mambo ya msingi ambayo watu wanaoanza mahusiano huwa wanayazingatia. Naamini wagelijua hilo na kwa sababu ya utamaduni wao wa kichaga hawangefanya hivyo.

Hata hivyo kwa ufahamu wangu mdogo hapa tz ndoa za mtu na binamu yake zinafanyika kama wana jf wengi walivyotangulia kusema. i was not aware about it in the chaga land.

Hata katika zama za biblia mzee Yakobo alioa mabinti wawili watoto wa mjomba wake Laban (Lea na Rachel). Mzee yakobo alilazimika kumtumikia mjomba kwa muda wa miaka saba kama mahali kwa kila binamu.

sisemi kwamba jambo hili linakubalika lakini nasema siyo zito la kulipotezea usingizi.

kabla sijaendelea ni wakristo au waislamu?
 
kama ni wakristo warejee maandiko yao wapate busara za humo pia. especially kumbukumbu latorati 27:13-26
 
Wapwa habari za leo. Tulizika salama salmin.
Vikao kadhaa vimekaa kuhusu hawa vijana wawili. Siku ya jana ilikuwa ya vikao pande zote.
Upande wa kijana hataki kusikia kabisa kuwa haruhusiwi kumwoa huyu binti. Amekataa kwa madai anampenda sana huyu binti kiasi kwamba kuachana naye kunaweza kuathiri utendaji wake na hata mustakabali wa maisha yake. Anadai ana ndoto nyingi sana kuhusu familia yake. Anadai kuwa anajua kuwa sio rahisi huyu binti aaache kuolewa na mtu mwingine (anavyodhani) hivyo asingependa kuona mwanae analelewa na baba mwingine. Mwisho akapigia msumari kuwa yuko tayari kwa chochote lakini kuachana na binti hawezi.
Upande wa binti wao wako vuguvugu. Wamemwachia binti aamue. Binti amekuwa bubu hajasema msimamo wake mpaka sasa ingawa yuko depressed sana.
Pande zote zimekubaliana kuwa kwa sasa wawaache hawa vijana walee kwanza mimba mpaka pale huyu binti atakapojifungua. Wazazi wanaamini kuendelea kulishupalia hili suala linaweza kuleta madhara na mimba ya huyu binti kuharibika.
 
Tupo msibani! Kijana kafiwa na baba yake. Katikati ya maombolezo anafika binti mmoja hivi mtanashati ingawa tumbo kubwa lakini huachi kuona uzuri wake, anajiunga upande wa wamama asalimiana wanaendelea na maongezi. Pamoja na majozi alokuwa nayo kijana anapata faraja ya haja. Mara akawa kama amechangamka hivi. Tunamuuliza kulikoni kijana?

Anasema da angalao mchumba wangu kaja maana nilikuwa nasikitika kumwacha mwenyewe mbali. Anha kumbe! Mjomba yupo hapa na unajua tena huku uchagani hawakopeshi.

We Lelo unasemaje! Nyie watoto wa siku hizi mafirauni sana! Yaani unathubutu kulala na mtoto wa shangazi yako unakuja hapa unatwambia mchumba wako! Jamaa jasho likaanza kumtoka! Da kumbe kijana keshamvimbisha binti wa wenyewe na sasa ni mtoto wa shangazi!

Ilikuwaje: Familia ya kijana wa kiume ilikuwa ikiishi nje ya Tanzania kwa kitambo kidogo. Ni mara chache sana walikuja Tanzania ingawa wazazi wote ni watanzania. Kwa kujua kuwa huyu mzee atastaafu mapema akaanza kumtanguliza mwanaye wa kiume aje Tanzania na akapata chuo cha kufundisha pale Dodoma.

Akiwa hana hili wala lile akakutana na binti mrembo yuko idara moja na yeye. Mazoea yakajengeka! Upendo ukachanua! Wakajikuta watupu,,,,,,,,,,,hatimaye mmoja akawa amebeba kiumbe cha muunganiko wao. Tuongeapo sasa mimba ina miezi 6 na ushee.

Maskini mzee wa watu hata hakustaafu bali kaugonjwa kakapita akaona wacha aje nyumbani akasalimie. Huku akazidiwa zaidi akalazwa pale KCMC. Mvulana akaomba likizo ya dharura pale chuoni aende kumuuguza mzee. Siku chache baadae baba akaaga dunia. Akamtaarifu mchumba wake kuwa baba mkwe wake mtarajiwa kafariki. Binti naye akaona ni vyema akajumuika msibani. So ikawa pia awatembelee wazazi wake huku kijijini.

Kumbe naye msiba unamhusu kwa njia nyingine bila kujua. Mama wa huyu binti akamwambia kuwa mjomba wake kafa hivyo wakasalimie. Maskini hakujua kuwa huo ndo msiba aloujia! Wakati anaingia hakumwona Kijana hivyo alijua tu kuwa angewasliana na mchumba wake ili amwelekeze msiba uko wapi. Sasa mambo yameharibika!

Mjomba najua na binti hajajua kuwa kule ndo kwa kijana mchumba wake kipenzi. Mimba hii ni kubwa sana inaweza ikaleta madhara! Maskini hawakujua kama ni ndugu! PANDE ZOTE ZIAMBIWE AMA TUACHE MPAKA MSIBA UPITE!

Ni ushauri wako tu. Kama unahisi kuwa unataka kukashfu ni bora uasiweke bandiko iache tu ipite!


UPDATES
Wazazi wa huyu binti wameelezwa habari hizi. Wamehuzunika sana kwa kweli. Binti na kijana wameitwa na kuelezwa ukweli.
  1. Kijana amekataa kuamini amedai atatoa maoni yake baadaye.
  2. Binti ameondoka na ndugu zake hakuweza kusema chochote alibaki kushangaa tu.
  3. Hakuna hata mtu mmoja keshajua linaloendelea zaidi ya sisi ndugu wa karibu
  4. Wazee wameshauri hili suala lizungumzwe baada ya kuvunja tanga
  5. Focus now ni mazishi tu
Nitawajulisha maendeleo ya hii kitu.

Ewe eeka mangi mbon nyei nya dede?kwekio kijana nyalesemba nfamaaye?
 
Asante mangi kwa kutuletea updates.
Haya mambo siyo mara ya kwanza kuyasikia kwa hawa marafiki wawili.
Kwa hili naomba nirudi kwenye msimamo wangu wa leo asubuhi kwamba sio la kulipotezea usingizi.
Niwaongezee maandiko kidogo ya biblia ambayo yanatuwekea mipaka katika familia zetu juu ya mambo ya ndoa au kufunuana tupu. Nayo ni ya kitabu cha Mambo ya Walawi 18:6-23. Kwa machache hayo nilipitia naona hakuna mahali anatajwa binamu kuwa mtu ambaye hatuwezi kumuoa.
Kwa kisa kizima na kwa upeo wangu mdogo nashauri hao vijana waendelee hata milele. Mwenyezi Mungu anisamehe pale ambapo nitakuwa nimeshauri kinyume na matakwa yake. Amen!
 
Ewe eeka mangi mbon nyei nya dede?kwekio kijana nyalesemba nfamaaye?

Arawa deda mboong'uo wandu walesye! Ya kuda kiwa ndeyako. Kindo kya dede kuchu. Kolola muna eto okika nooriwe kumira made. Kimuna kicha deeya tata.
 
Back
Top Bottom