Hahahaa! Yaani we unasema bora asingekuwepo "commando?!" Siku moja nilimsikia Said Fella akizungumzia kwanini Ruby hakutokea kwenye video ya Yamoto! Yaani ilikuwa ukimsikiliza kwa makini, unagundua kabisa Fella kuna kitu hakutaka kukianika kuhusu Ruby... akaamua tu kutumia busara hasa ukizingatia hadi kesho Ruby yupo THT!!
Halafu nimekumbuka kuhusu suala la Ruby kwa THT isije napo ikawa ni tatizo lingine!! Unajua zamani kuna mwana-TMK wetu mmoja aliingia kwenye management fulani hivi (jina kapuni lakini unaweza kufanya maths mwenyewe)!! Sasa yule mwanetu life lake kitaa lilikuwa la kawaida sana-- c unajua watoto wa Temeke!
Alipoingia kwenye ile management, jamaa wakaanza kumpiga na pamba za kufa mtu; raba za maana na mambo mengine kama hayo! Yaani mshikaji akaanza kupata huduma! Ikawa mshikaji kila anachotaka anapata! Alivyokuwa f'ara (but sote enzi hizo tulikuwa maf'ara), hakujua kwamba jamaa walikuwa wanaandikia kila wanachompatia... kuanzia kwenye outfits hadi kwenye misosi... vyote vilikuwa vinaingizwa kwenye hesabu!!
Kuja kugonga copy sasa!! Jamaa wakaanza kupiga hesabu ya gharama walizotumia kuanzia recording, pamba, transport hadi misosi!! Ilikuwa ugomvi mkubwa... kwamba wanamdhulumu!!
Sasa huyu Ruby asije akadhani zile services anazopata pale THT ni sadaka!