Masomo matatu Advance hayana mana.

Hoja yako ni nzuri pamoja na kuwa ulipaswa kuanza mbali sana manake tatizo lipo kutokea level ya chini kabisa ya elimu yetu.
Kifupi ni kwamba mfumo wetu ungetengenezwa kwa kila mwanafunzi kujispecialize mapema kutoka akiwa level ya chini. Kama mtu anapenda udaktari, ualimu, uhandisi n.k angetengenezwa kutokea huko chini. Mimi binafsi sielewi sababu za msingi za kumbebesha mwanafunzi masomo kumi na mwishowe kuja kutumia only two katika maisha yake.
 
mwenye huu uzi inaonekana unapenda sana mteremko hao walioanzisha hayo masomo matatu sio wajinga nahc ww ni kilaza think big usipend urahisi wa mambo

Wewe umekuja na huku!!! Jamani hili akili zake si nzuri, wenzako wanatoa thread za maana watu wajadili we unatoa pumba!!!? Msibishane nalo kama mnabisha angalieni thread yake ya mambo ya heslb
 
Chamviga.
Hayo maelezo nilitoa,tena niliongelea mfumo mzima wa elimu toka shule ya msingi mpaka chuo kikuu,nilitoa mapendekezo yangu mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba,warioba kaweka kapuni,o level nako masomo ni lundo na wakati yalitakiwa masomo manne ama matano tu.
KURUTA WA MUNGU.
wewe unadhani masomo mawili hayatoi wigo mpana?Somo moja tu mfano geography linakupa wigo wa kuchagua vitu vingi zaidi sasa masomo yote mawili ni haba?Na kitu kingine unatakiwa kujua unataka nini na siyo kwenda kwenda kama ng'ombe,MATOKEO YAKE HATA WATAALAMU WETU WANAPATA WAKATI MGUMU LINAPOKUJA SWALA LA vitendo kwa sababu hawajui kiundani walikalia kumeza hata ambayo ni nje ya fani yao badala ya kutumia muda huo kujinoa kivitendo.
 
kweli kabisa.je akifaulu math na chemistry?,je akifaulu math na physics na kufeli bios utaenda udaktar@bora uwe na matatu yanakupa flexibility.kijana mambo mengne fikili kwanza ndo uandike topic

Unadhani sijafikiria,kwa hali hii leo tanzania inaweza kutoa PHD Holder wa miaka kati ya 17 na 21 ???Haiwezekani,hakuna sababu ya msingi kwa masomo matatu katika utalaamu,hata mtu anaenda kusoma diploma kutokea olevel wanaangalia masomo mawili tu.
 
yan watz ni waoga sana wamabadiliko kila kitu nikuiga tu. umefka wakati nasisi tufanye yetu kutokana na hali halis tulonayo. Huu mfumo wa elm ni mbovu lzma tuurekebshe huwez kumfndsha masomo yabiashara wkt ndoto zake nikuwa daktari.mtoto na aandaliwe kuwa mtaalam wa fani fulani toka mwnzoni na sio kumbebesha masomo kbao na ndo mana hata wataalam wetu wanalongolongo nyingi
 
Unadhani sijafikiria,kwa hali hii leo tanzania inaweza kutoa PHD Holder wa miaka kati ya 17 na 21 ???Haiwezekani,hakuna sababu ya msingi kwa masomo matatu katika utalaamu,hata mtu anaenda kusoma diploma kutokea olevel wanaangalia masomo mawili tu.

my aim is to be a generalist sio kujifunga bila kujua vitu vichache.mfano chuo hata wanaosoma engineering wanasoma unit ya economics and entrepreneuship
 

Physics ni msingi wa natural science. Unaweza kuwa na Physics bila Biology, lakini huwezi kuwa na Biology bila Physics,

Unaweza kuwa na Physics bila Chemistry, lakini huwezi kuwa na Chemistry bila Physics.

Huwezi kujenga nyumba juu kwa juu bila ya kuanza na msingi. Hence kuelewa Physics ni muhimu sana kwa mtu anayetaka kuelewa sayansi.

Kwenye udaktari kwenyewe kuna Physiology, ambayo ni Physics ya organisms. Sasa utaendaje kumfundisha daktari anatomy jinsi mifupa ya mwili ilivyokaa na ligaments zinavyofanya kazi kabla ya kumfundisha the corrosive effects of friction in Physics?
 
Wewe umekuja na huku!!! Jamani hili akili zake si nzuri, wenzako wanatoa thread za maana watu wajadili we unatoa pumba!!!? Msibishane nalo kama mnabisha angalieni thread yake ya mambo ya heslb

Hilo jamaa halina akili yani, JF siku hizi majanga tu.
 
mbona Uganda tu hapo advance ni ngoma nne pamoja na gs mkuu.... tena nahisi na kwa sie hapa bongo yangeongezwa kabisa

HII ndo nini?kwani hujui HATA HAPA TUNA GS?HUJUI KAMA PCB WANA MASOMO MATANO UKIJUMLISHA NA BAM
 
sikubalian na wewe maana ukiangalia katika PCM sio kila mtu anataka awe engineer mwingine ataenda kusomea Nuclear Physics hii inahitaji sana physics na pia kemia na maths hapo haitakiwi kukosekana. so bado yana umuhimu
HOJA YANGU NI KUSOMA MASOMO MAWILI NA MOJA BASIC,huyo wa nuclear physics si atasoma masomo mawili advance ya PHYSICS NA CHEMISTRY,na kitu kingine unatakiwa kujua stake holders ndio wanapanga nini tusome kwa hiyo wanaweza wakakaa na kutuambia tusome nini na si kila fani ya nje hata kama haina matumizi hapa tuisome
 
nimeshakwambia utasoma masomo mawili lakini la tatu lazima liwe basic ili ku-meet mahitaji ya hayo masomo mawili na mimi sikusema kuwa usisome kabisa
 

lazima tuanze kufikiria tofauti kwa mazingira ya kiafrika na hao anajitapa kuwa na skill kuliko elimu ya nje huku kila siku ugunduzi na mabadiliko yote yanatokea nje tu na sijui wao wanafanya kipi cha maana hapa
 
Jibu hoja ya msingi.
Ulitaka nikuorodheshee fucults zote za PCB na PCM?Baada ungeuliza na kombi zingine,hoja yangu ilikuwa ili uende chuo unaihitaji masomo mawili tu.SOMA TENA UJIBU HOJA YA MSINGI.na usijibu out of point.

Hoja yako ni finyu, imeangalia baadhi ya fani unazozijua tu. Ngoja nikupanue kidogo katika fani tofauti za vyuo vikuu.

1. Vipi juu ya fani hizi za Uhandisi (Engineering)- 1.Chemical engineering 2. Petrol eng. Unaweza kuzitaja kibao. Hazihitaji Chemistry. Ama sijakuelewa uliposema INJINIA ulimaanisha nini? Ndio maana nikaanza kwa kusema mtazamo wako ni finyu, kwa sababu nia ni kumpa mwanafunzi nafasi kubwa ya kuchagua kama ulivyodokezewa na aliyesema neno "Flexibility" Unaweza kuwa mwalimu wa Fizikia na Kemia au fizikia na hesabu.

Ila kama ulishadhamiria kuwa Daktari, wewe Kemia ishiti, ila uhakikishe una angalau c katika kemia na baiolojia. Udaktari hutaukosa. Ila Ksiku ya Mtihani Kemia au Baiolojia ikikaa vibaya jua umejifungia bahati, maana ukipata D ktk baioloji na kemia una point 4, hupati chuo chochote cha udaktari.
 
nimeshakwambia utasoma masomo mawili lakini la tatu lazima liwe basic ili ku-meet mahitaji ya hayo masomo mawili na mimi sikusema kuwa usisome kabisa

What is basic and what is not? Who decides? By what criteria?

Kuna watu watakwambia pretty much yote unayojifunza A Level ni basic, kama unataka kufuata nyayo za kina Dr. Gell-Mann huko.

Na yanakupa msingi wa kuamua baadaye unapoenda chuoni uwe na wigo mkubwa wa kuamua kuwa daktari, mfamasia au injinia kwa mfano ukisoma PCB/M.

Utasema nini?

Kwa nini unataka kuwapunguzia wigo watu wakati wengi hata hawajafikia kuamua wanataka kusomea "major" gani bado?
 
ndugu ya sio kweli kuwa wazungu wanaopt masomo tangu mapema mfano uingerza italy ufaransa wao advance ni masomo 3 ugeruman austria uholanzi wao advance ni masomo 5

tofauti nyingine unapotumia neno advance ama high school ni tofati kulingana na nchi na hiyo advace unayoisema haifanani na advance ya hapa tanzania JAPO NENO ADVANCE LIMETUMIKA KOTEKOTE.mfano huko uingeleza mwanafunzi wa miaka 15,16 na 17 ndo advance,wakati sisi hawa hata form fourm bado hawajamaliza kwa mfumo wetu.
 
ukiwa advance basic subject ni BAM na GS TU,MENGINE NDO MANA YANAITWA PURE japo si yote yanatumia neno pure ila waweza kuyaita pricipal subjects,HAYO HAYO MASOMO YANAYOITWA PRINCIPAL SUBJECTS YATAITWA AMA YATAJULIKANA KAMA BASIC SUBJECT KWA MWANAFUNZI ANAESOMA UNIVERSITY KWA SABABU YANASIMAMA KAMA MSINGI WA KUMWEZESHA MWANAFUNZI KUFIKIA HIYO LEVEL YA JUU,kwa hiyo usichanganye hapo mana mimi nazungumzia advance
 
(HUWEZI KUNISHAWISHI kuwa chemistry ya mtu anaetaka kuwa dakitari(PCB-physics haihitajiki sana) eti ifanane na chemistry ya mtu anaetaka kuwa injinia-with exclusion of engineering from BIOLOGY and CHEMISTRY(PCM-chemistry haihitajiki sana).HAPO KWENYE RED HUKUONA kutoka kwenye thread?natambua hizo fani,rejea kwenye mada mana umesoma nusunusu ukakimbilia kujibu kitu ulichokuwa hujaelewa kwa sababu ya uzembe wa kusoma,KWANZA TAMBUA HII NI HOJA YANGU BINAFISI AMBAYO NI YA MSINGI KABISA,kuhusu hizo fani haziwezi kushindwa kutengenezewa utaratibu,kwa sababu hoja yangu kuu ni kwamba advance watu wasome masomo mawili mawili,kwani inashindikana kusema anaetaka kuchukua CHEMISTRY NA PHYSICS NA ACHUKUE na ikajulikana kuwa vitivo unavyoweza kuchukua kwa haya masomo ni pamoja na chemical engineering,petroleum engineering nk?KIFUPI INAWEZEKANA,pia niliposema chemistry haina mana nilispecify ni kwa fani ipi ya engineering katika kujaribu kujenga hoja na sikumaanisha kila engineering na ndio maana kuonyesha kuwa nilikuwa makini kuliko wewe unaekimbilia kubisha ama kujibu ukiwa umesoma nusunu NILISEMA WITH EXCLUSION OF ENGINEERING FROM BIOLOGY mfano GENETIC ENGINEERING nk na fom CHEMISTRY ambapo mfano wa engineering from chemistry ndio kama hiyo uliyoitaja ya chemical engineering na nyingine nyingi na si lazima nizitaje zote.MASOMO MAWILI TU NA NDIO YAKUPELEKE CHUO,
 
basic APPLIED SUBJECT katika elimu ya adance ni kama ilivyo BAM ya PCB,CBA,CBG nk ambayo haifanani pure maths ya PCM,EGM,CBM,PGM nk,MSOMO YASIYO BASIC NI PRINCIPAL SUBJECTS ambayo ndo yanatengeneza mjumuiko wa hayo masomo ya katika combination,anaeamua iweje ni serikali kama walivyoamua sasa kwa kuanzisha combination mpya kama hiyo ya CBM na zingine kama tatu,
MTU ANAPOYAITA MASOMO YOTE YA ADVANCE KUWA NI BASIC HAPO ANAZUNGUMZIA KATIKA NGAZI YA JUU YAKE,mfano mtu akiwa chuo kikuu masomo ya advance ndio basic ya vitivo vya chuoni,vivyo hivo mtu anaweza kusema masomo yote ya o leve ni introduction kwa masomo hayo akimaanisha mtu akiwa Advance masomo ya o level yalisimama kama introduction kwa yeye kuweza kuyasoma masomo hayo ya advance
 

Hujajibu swali langu la msingi.

Kama haya masomo yote ni basic kwa mwanafunzi anayesoma university, kama ulivyoandika mwenyewe, kwa nini unataka kupunguza wigo wa basic subjects za kuingilia university wakati mwanafunzi bado yupo A- Level ?

While at it, kwa nini utake masomo mawili A Level na sio moja kabisa? What is your criteria? What makes you say 3 is too much 2 is just enough and 1 is not sufficient?

Wewe hujajua netiquette na kwamba writing in all caps is a faux pas that makes you appear that you are shouting in hysterics halafu unataka kufundisha watu wabadili mfumo wa elimu bila sufficient reasons?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…