Masoud djuma ..na kiatu kisichomtosha..

Masoud djuma ..na kiatu kisichomtosha..

Its Pancho

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
15,966
Reaction score
26,404
Miaka yote huwa naamini adui yako hatoki mbali... yaani yupo karibu yako..
ndo kinachomkuta masoud djuma.. kocha msaidizi wa simba sc.. ni kipenzi cha mashabiki. anapendwa na wengi ,lakini viongozi hawana imani nae tena, alikuja kocha mfaransa akashindwana nae.. na pia huyu mbelgiji wamegombana.. moja kwa moja utagundua tatizo ni masoud djuma mwenyewe.. kwanini??
mara nyingi huko ulaya kocha msaidizi anahusika na pg za mazoezi.. ila kikosi anapanga kocha mkuu.. hii inazuia kutoingiliana majukumu... inasaidia kila mmoja kuona anawajibika.... sasa palé simba masoud anaona kama hasikilizwi, so njia anayotumia ni kuwashawishi wachezaji Kuwa upande wake.. masoud anautaka ukocha mkuu.. lakini inabidi akubali Kuwa yeye bado sana yaani Viatu bado havimtoshi.. akiwa kocha mkuu kwa muda.. alipoteza final sportpesa kisha akaja kapoteza final kagame na azam na ilionekana wazi kabisa djuma ni mzito wa kufanya sub zenye macho, kiufupi masoud aendelee kupata uzoefu...

"mchizi kichizi "
 
Yeye ndio mchawi wetu pale ,haina cha kipenzi wa mashabiki wala nini aondoke tu maana sio mzalendo kwa timu yetu pendwa Simba sport club mabingwa wa kihistoria

Nakumbuka wakati anakuja alifanya interview yake ya kwanza alisema ukiwa kocha wa club kubwa hizi huwezi kufungua begi lako lote so technically alikuja akijua yeye ni mpitaji hivyo anafanya lolote ili mradi anufaike yeye bila kuangalia club inaathilika vipi

Ukiangalia timu yetu unaona kabisa amewagawanya wachezaji na kwa vile ni rafiki yao wanaonesha wazi wazi kumsapoti katika kusimamia kile anachohitaji

He is a traitor na traitor adhabu yake ni hanging
 
Simba ni club kubwa inahitaji kocha mwenye CV na sio mdomo mwingi kama Masudi

Namuheshimu sana Masudi lakini hapa amenichefua kwa vitendo vyake vya uzandiki
 
Tangu Mtibwa wawe apeche alolo sioni timu nyingine ya kushabikia hapa Tanzania.

Timu zinafukuza makocha kama zimetumwa!!! Eti mchezaji anakua mfungaji bora msimu huu na timu yake inachukua ubingwa, msimu unaofuata analetwa kocha mpya halafu anasema huyo mchezaji (aliyekua mfungaji bora msimu uliopita) hana stamina hivyo hamtaki anamuuza.

Hii ligi yenyewe na TFF yote utumbo (Bora enzi za Leodgar Tenga), ukipata gazeti la leo ukaangalia msimamo wa ligi utakuta kuna timu zimecheza mechi 6 nyingine 7 nyingine 3 nyingine 4. Ligi za wenzetu utakuta nyingi zimecheza 7 halafu zilizobaki timu nne zimecheza 6 na weekend ndiyo wanakamilisha.

Rais alitaka kuhamia Posta akapange jengo wakati TFF ina jengo lake. Na yule jamaa akaulizwa kwanini Taifa Stars tunabanwa michezoni, bila aibu akajibu tatizo ni jezi.

Kufuatilia mpira Tanzania ni kujichosha.
 
Tangu Mtibwa wawe apeche alolo sioni timu nyingine ya kushabikia hapa Tanzania.

Timu zinafukuza makocha kama zimetumwa!!! Eti mchezaji anakua mfungaji bora msimu huu na timu yake inachukua ubingwa, msimu unaofuata analetwa kocha mpya halafu anasema huyo mchezaji (aliyekua mfungaji bora msimu uliopita) hana stamina hivyo hamtaki anamuuza.

Hii ligi yenyewe na TFF yote utumbo (Bora enzi za Leodgar Tenga), ukipata gazeti la leo ukaangalia msimamo wa ligi utakuta kuna timu zimecheza mechi 6 nyingine 7 nyingine 3 nyingine 4. Ligi za wenzetu utakuta nyingi zimecheza 7 halafu zilizobaki timu nne zimecheza 6 na weekend ndiyo wanakamilisha.

Rais alitaka kuhamia Posta akapange jengo wakati TFF ina jengo lake. Na yule jamaa akaulizwa kwanini Taifa Stars tunabanwa michezoni, bila aibu akajibu tatizo ni jezi.

Kufuatilia mpira Tanzania ni kujichosha.
Tatizo ni jezi? Daah bongo nyoso
 
Yeye ndio mchawi wetu pale ,haina cha kipenzi wa mashabiki wala nini aondoke tu maana sio mzalendo kwa timu yetu pendwa Simba sport club mabingwa wa kihistoria

Nakumbuka wakati anakuja alifanya interview yake ya kwanza alisema ukiwa kocha wa club kubwa hizi huwezi kufungua begi lako lote so technically alikuja akijua yeye ni mpitaji hivyo anafanya lolote ili mradi anufaike yeye bila kuangalia club inaathilika vipi

Ukiangalia timu yetu unaona kabisa amewagawanya wachezaji na kwa vile ni rafiki yao wanaonesha wazi wazi kumsapoti katika kusimamia kile anachohitaji

He is a traitor na traitor adhabu yake ni hanging
Kabisa yaani kuna mgawanyo mkubwa..
 
DJUMA, BORA UKWELI MCHUNGU, KULIKO UONGO MTAMU.

-Rafiki yangu Masoud Djuma amepeana mkono wa kwaheri na mabosi wa Simba. Muda wowote kutoka sasa ataenda Uwanja wa Ndege kuianza safari ya kurudi kwao Rwanda. Simba haina inachomdai na Djuma mwenyewe hana anachoidai Simba.

-Djuma anaondoka, huku nyuma akiwaacha vinywa wazi baadhi ya manazi wa Simba wanaompenda. Ameiacha sumu hii na ameipakaza sehemu kubwa. Manazi hao wanaamini kaondolewa kwa kuonewa.

-Sio kificho tena. Maneno ya Try Again jana asubuhi yamehitimisha safari ya Djuma kama kocha msaidizi wa Simba. Kama Try Again Rais wa Simba alisema wanatumia nguvu kubwa ya usuluhishi baina ya Djuma na Mbelgiji, lakini mambo yamekuwa magumu, hapa tunapaswa kutumia akili ndogo ya 2 + 2 = 4 kuelewa Djuma hana chake Msimbazi. Try Again alikuwa muwazi.

-Lakini ninachokiamini kuwa kuna siku Djuma atarudi nchi hii kufundisha soka. Kama si msimu huu, msimu ujao. Au msimu mwingine, ila atarudi. Zimwi likujualo, halikuli likakwisha. Djuma hajaondoka kama walivyoondoka makocha wengi wa Simba walioondoka hivi karibuni. Ameondoka kama dume la Nyani linalotembea kwa madaha katikati ya kundi kubwa la nyani wa kike.

-Djuma kama wanadamu wengine ana mapungufu yake. Lakini anajua kufundisha. Anajua kuifanya timu ikacheza anavyotaka. Ana identity yake ya mpira. Ni Guardiola fulani hivi wa 'bei rahisi'. Ana sex football. Anajua kumfunga mpinzani na kumtawala. Hapa ndipo Djuma alipowashika wanaompenda. Hajawashikia kwingine, ni hapa tu.

-Hawa mashabiki wa Simba waliowehuka nae sio wajinga. Kuna kitu wanakiona katika kichwa chake. Simba imewatimua Omog, Mayanja, Lechantre, sababu ni yeye, lakini hii haijafanya manazi hao waache kumuona kama Djuma mwanadamu wa ajabu, ndiyo kwanza wamemuweka vizuri katika mioyo yao na ilichokifanya Simba wanahisi kaonewa. Huu ndiyo 'uchawi' wa Djuma.

-Mashabiki hawa waliamini hata sare yao na Ndanda Fc pale Mtwara na kipigo chao cha Mbao kule Mwanza ilitokana na Djuma kutokuwepo katika benchi lao. Kuna imani fulani wameiweka kwake. Tutakapoona amerejea nchini iwe kufundisha Simba au timu nyingine tusishangae.

-Katika kipindi hiki ambacho Simba inaenda katika uchaguzi, si ajabu wagombea wakatumia jina lake kuombea kura kwa wanachama. Ni mwanachama gani asiyetaka kusikia ngoma za masikio yake likipenya neno urejeo wa Djuma kwa mara nyingine? Ni wengi, wasiomtaka ni wachache wanaohesabika kwa vidole vya miguuni, mkononi. Wengi watataka.

-Wakati mwingine inakanganya na kuleta maswali magumu unapoona Djuma huyu anayekubalika hivi, ameifanyia nini Simba? Inashangaza kidogo.bHiki kiburi chake kilipaswa kuwepo kwa Selemani Matola aliyefanyia makubwa Simba, lakini msimu wake mmoja tena kama kocha msaidizi amekuwa star. Anasifiwa kuliko inavyosifiwa Simba yenyewe.

-Narudia tena iko siku Djuma atarudi nchi hii. Naamini hivi. Siamini vingine. Ni ngumu tembo kupenya tundu la sindano, lakini ni rahisi Djuma kurudi nchini. Iwe Simba. Iwe Yanga. Kokote kule, lakini atarudi tu! Si ajabu viongozi hawa waliopeana nae mkono wa kwaheri ndiyo watakaomtumia tiketi ya ndege kumtaka arudi nchini. Hupaswi kuwaamini sana viongozi wetu wa soka. Nao wana mihemko yao.

-Tumewahi kushuhudia kwa Partick Phiri. Miaka ya hivi karibuni huyu anakuwa kocha aliyetimuliwa mara nyingi na Simba na hapo hapo kuwa kocha aliyeifundisha mara nyingi katika vipindi tofauti. Phiri anatimuliwa mchana, jioni anarejeshwa. Nasikia mwenyewe ameizoea hali hii, haimpi shida.

-Sitashituka Djuma akiwa Phiri mwingine. Kunataka moyo wa Hawafu mwenye nguvu kuachana moja kwa moja na Djuma. Djuma si Omog, Djuma si Mayanja, Djuma si Lechantre, Djuma ni Djuma tu. Yuko mmoja kama alivyo.

-Mwisho kabisa namtakia kila la kheri rafiki yangu Djuma. Safari njema my friend na fika salama, ila wacha nikunong'oneze kitu hakikisha simu yako inakuwa na chaji muda wote. Burundi na Tanzania sio mbali. Bon Voyage my friend Djuma.
 
Simba ni club kubwa inahitaji kocha mwenye CV na sio mdomo mwingi kama Masudi

Namuheshimu sana Masudi lakini hapa amenichefua kwa vitendo vyake vya uzandiki
Hivi Mkuu unaweza ukaweka wazi huo Uzandiki wa Masoud Djuma?
 
...
.. alipoteza final sportpesa kisha akaja kapoteza final kagame na azam na ilionekana wazi kabisa djuma ni mzito wa kufanya sub zenye macho, kiufupi masoud aendelee kupata uzoefu...

"mchizi kichizi "
Lakin timu ilifika fainali Mkuu,
Kagame Simba ilikua ikijaribu kikosi kipya, ndio maana hukuwaona kina Bocco, Kichuya, Mkude, Manula etc,
Sasa unapojaribu kikosi kwenye mechi kubwa kama zile lolote linaweza kutokea,
Labda tujiulize wazo la kuchezesha kikosi kipya ambacho hawajawahi kucheza pamoja lilikua lake au la Uongozi?
 
DJUMA, BORA UKWELI MCHUNGU, KULIKO UONGO MTAMU.

-Rafiki yangu Masoud Djuma amepeana mkono wa kwaheri na mabosi wa Simba. Muda wowote kutoka sasa ataenda Uwanja wa Ndege kuianza safari ya kurudi kwao Rwanda. Simba haina inachomdai na Djuma mwenyewe hana anachoidai Simba.

-Djuma anaondoka, huku nyuma akiwaacha vinywa wazi baadhi ya manazi wa Simba wanaompenda. Ameiacha sumu hii na ameipakaza sehemu kubwa. Manazi hao wanaamini kaondolewa kwa kuonewa.

-Sio kificho tena. Maneno ya Try Again jana asubuhi yamehitimisha safari ya Djuma kama kocha msaidizi wa Simba. Kama Try Again Rais wa Simba alisema wanatumia nguvu kubwa ya usuluhishi baina ya Djuma na Mbelgiji, lakini mambo yamekuwa magumu, hapa tunapaswa kutumia akili ndogo ya 2 + 2 = 4 kuelewa Djuma hana chake Msimbazi. Try Again alikuwa muwazi.

-Lakini ninachokiamini kuwa kuna siku Djuma atarudi nchi hii kufundisha soka. Kama si msimu huu, msimu ujao. Au msimu mwingine, ila atarudi. Zimwi likujualo, halikuli likakwisha. Djuma hajaondoka kama walivyoondoka makocha wengi wa Simba walioondoka hivi karibuni. Ameondoka kama dume la Nyani linalotembea kwa madaha katikati ya kundi kubwa la nyani wa kike.

-Djuma kama wanadamu wengine ana mapungufu yake. Lakini anajua kufundisha. Anajua kuifanya timu ikacheza anavyotaka. Ana identity yake ya mpira. Ni Guardiola fulani hivi wa 'bei rahisi'. Ana sex football. Anajua kumfunga mpinzani na kumtawala. Hapa ndipo Djuma alipowashika wanaompenda. Hajawashikia kwingine, ni hapa tu.

-Hawa mashabiki wa Simba waliowehuka nae sio wajinga. Kuna kitu wanakiona katika kichwa chake. Simba imewatimua Omog, Mayanja, Lechantre, sababu ni yeye, lakini hii haijafanya manazi hao waache kumuona kama Djuma mwanadamu wa ajabu, ndiyo kwanza wamemuweka vizuri katika mioyo yao na ilichokifanya Simba wanahisi kaonewa. Huu ndiyo 'uchawi' wa Djuma.

-Mashabiki hawa waliamini hata sare yao na Ndanda Fc pale Mtwara na kipigo chao cha Mbao kule Mwanza ilitokana na Djuma kutokuwepo katika benchi lao. Kuna imani fulani wameiweka kwake. Tutakapoona amerejea nchini iwe kufundisha Simba au timu nyingine tusishangae.

-Katika kipindi hiki ambacho Simba inaenda katika uchaguzi, si ajabu wagombea wakatumia jina lake kuombea kura kwa wanachama. Ni mwanachama gani asiyetaka kusikia ngoma za masikio yake likipenya neno urejeo wa Djuma kwa mara nyingine? Ni wengi, wasiomtaka ni wachache wanaohesabika kwa vidole vya miguuni, mkononi. Wengi watataka.

-Wakati mwingine inakanganya na kuleta maswali magumu unapoona Djuma huyu anayekubalika hivi, ameifanyia nini Simba? Inashangaza kidogo.bHiki kiburi chake kilipaswa kuwepo kwa Selemani Matola aliyefanyia makubwa Simba, lakini msimu wake mmoja tena kama kocha msaidizi amekuwa star. Anasifiwa kuliko inavyosifiwa Simba yenyewe.

-Narudia tena iko siku Djuma atarudi nchi hii. Naamini hivi. Siamini vingine. Ni ngumu tembo kupenya tundu la sindano, lakini ni rahisi Djuma kurudi nchini. Iwe Simba. Iwe Yanga. Kokote kule, lakini atarudi tu! Si ajabu viongozi hawa waliopeana nae mkono wa kwaheri ndiyo watakaomtumia tiketi ya ndege kumtaka arudi nchini. Hupaswi kuwaamini sana viongozi wetu wa soka. Nao wana mihemko yao.

-Tumewahi kushuhudia kwa Partick Phiri. Miaka ya hivi karibuni huyu anakuwa kocha aliyetimuliwa mara nyingi na Simba na hapo hapo kuwa kocha aliyeifundisha mara nyingi katika vipindi tofauti. Phiri anatimuliwa mchana, jioni anarejeshwa. Nasikia mwenyewe ameizoea hali hii, haimpi shida.

-Sitashituka Djuma akiwa Phiri mwingine. Kunataka moyo wa Hawafu mwenye nguvu kuachana moja kwa moja na Djuma. Djuma si Omog, Djuma si Mayanja, Djuma si Lechantre, Djuma ni Djuma tu. Yuko mmoja kama alivyo.

-Mwisho kabisa namtakia kila la kheri rafiki yangu Djuma. Safari njema my friend na fika salama, ila wacha nikunong'oneze kitu hakikisha simu yako inakuwa na chaji muda wote. Burundi na Tanzania sio mbali. Bon Voyage my friend Djuma.
Umeandika kwa emotion na uelewa mkubwa wa soka la simba, nampenda masoud namtakia kila la kheri, Bado sijaona kama kuna kipya mbelgiji atakileta msimbazi na bado naamini kwa masoud.

Thanks Djuma
 
Hivi Mkuu unaweza ukaweka wazi huo Uzandiki wa Masoud Djuma?
Kama mpaka sasa ujui uzandiki wake sina sababu ya kukwambia maana wewe tayari upo upande wake

Simba ni taasisi kubwa lazima imfanye mtu aitegemee na wala sio yeye ndio ategemewe na Club ukiangalia hiyo mgogoro inayoibuka kila mara baina yake na makocha wakuu huoni kama ni conflict zinazoipa panic club
 
Hela wanayo ya kubadilisha makocha. Nyinyi komaeni na wakongo nadhani baada ya mwaka mmoja Club itabadilishwa jina na kuwa Sebene band
Migambo inaruka na kuķanyagana[emoji441][emoji444][emoji445]

Hii timu ina makombe ya kufukuza makocha
 
Hela wanayo ya kubadilisha makocha. Nyinyi komaeni na wakongo nadhani baada ya mwaka mmoja Club itabadilishwa jina na kuwa Sebene band
Hela ya kupiga dili timu imejaa watakatisha pesa na wapiga dili tu. Ndo mana vìongozi wote waliochaguliwa kwa kura wapô jela na wengine wamekimbia nchi
 
Lakin timu ilifika fainali Mkuu,
Kagame Simba ilikua ikijaribu kikosi kipya, ndio maana hukuwaona kina Bocco, Kichuya, Mkude, Manula etc,
Sasa unapojaribu kikosi kwenye mechi kubwa kama zile lolote linaweza kutokea,
Labda tujiulize wazo la kuchezesha kikosi kipya ambacho hawajawahi kucheza pamoja lilikua lake au la Uongozi?
ni kweli mkuu.. lakini kocha aliyekomaa anapata matokeo hata akitumia team b..
 
Hela wanayo ya kubadilisha makocha. Nyinyi komaeni na wakongo nadhani baada ya mwaka mmoja Club itabadilishwa jina na kuwa Sebene band
Halafu inasaidia nini?? kufukuza makocha kati kati ya msimu??
 
Kama mpaka sasa ujui uzandiki wake sina sababu ya kukwambia maana wewe tayari upo upande wake

Simba ni taasisi kubwa lazima imfanye mtu aitegemee na wala sio yeye ndio ategemewe na Club ukiangalia hiyo mgogoro inayoibuka kila mara baina yake na makocha wakuu huoni kama ni conflict zinazoipa panic club
Kila mtu ana mtizamo wake..
 
Back
Top Bottom