Utamaduni wa kulipa kodi kwa hiaria Tanzania ni kama umepotea hivi. Yale mabadiliko yaliyofanywa na Msuya mwaka 1986 nadhani ndiyo yamesababisha haya yote kuonekana kama kodi ni adhabu. Hapana, kodi ni ni mkataba baina ya raia na serikali popote duniani. Serikali itajenga majeshi ya ulinzi na usalama, itajenga barabara, madaraja, na minundombinu yote ya muhimu ambayo raia wanaitumia bure, halafu raia watalipa kodi serikalini! Miundombinu ni neno pana sana lakini linajumuisha pia vitu kama elimu na afya ya msingi kwa raia pamoja na mazingira yao.