Massey Ferguson 290 4WD na FORD 8210

Inategemea na aliekulimia pia, unaweza kulimia hata new holland ya horse power 90 na ikatoka ujinga na mwingine akalimia swaraj ya horse power 60 na akalima shamba vizuri sana. Japo kuna facts nyingine zinachangia shamba kulimwa vizuri au vibaya. Na watu wengi wanasahau uwezo wa dereva
Cheki na New Holland pia iko vizuri. Nililima na Massey vs New Holland, New Holland inafunika mpaka raha jani lotee linazikwa
 
Kati ya hiyo massey na ford. Zote ni imara sana, ila chukua massey. Kwa Tanzania na kwa sisi wakulima wadogo tukitaka kununua trekta lazima tuangalie uimara ikifuatiwa na upatikanaji wa spare afu ndo yatakuja mambo mengine. Spare za trekta ni ghali bila kujali ni ya kampuni ipi(natumaini umejipanga kwa hilo), ila za massey ni rahisi kuzipata kuliko za hiyo ford. Ila kama unataka uonekane unamiliki trekta la gharama basi chukua ford. Massey likiharibika katikati ya msimu wa kulima linaweza kupona ndani ya siku 2 tu maana unapanda bodaboda au basi fasta unaingia dukani unarudi na spare. Ila ford ikiharibika katikati ya msimu wa kulima, upatikanaji wa spare unaweza kupanda ndege kufuata[emoji16] au kuingia alibaba, amazon na ebay kuitafuta(hapa namaanisha spare za ford ni ngumu kupatikana kidogo ndani ya Tz japo zinapatikana). Na kumbuka msimu wa kulima haukusubiri kamwe. Mwisho, trekta ni matunzo kama unavyoitunza gari yako au pikipiki kwa kumwaga oil kwa wakati, kubadili filters, coolant na mengineyo. Ukilitunza litakutunza.
 
Je unahitaji kulima mahindi na hauna muda wa kusimamia? Au unataka upate mavuno mengi zaidi? Njoo ofisini kwetu.

Ofisi ya YAD yenye wataalamu wabobezi wa kilimo sasa inakuletea mpango wa kusimamia shughuli zote za shambani. Mkulima utatukabidhi shughuli zako pale shambani kwako sisi tutafanya kila kitu kwa utaalamu zaidi na kukukabidhi mazao yako yakiwa yamekomaa. Gharama zetu ni nafuu sana na tunakuhakikishia kwa ekari moja kuvuna mahindi zaidi ya gunia 30. Usihangaike sasa, sisi tupo kwa ajili yako, Kwa Wale ambao hawana mashamba tutakuwezesha kupata mashamba ya kukodi kwa elfu 40 tu na mashamba ya kununua kwa elfu 60 tu hata ukihitaji ekari 100 za kununua utazipata kwa bei hiyo hiyo.

Kwa maelezo zaidi fika ofisini kwetu.
Jengo la NSSF SONGEA
Ghorofa ya 3 chumba no. 317
Simu. 0621133117
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…