Maswali Kupima Ujuzi Wa Lugha Badala Ya Ujuzi Wa Somo Husika

Maswali Kupima Ujuzi Wa Lugha Badala Ya Ujuzi Wa Somo Husika

Fikra Pevu

Senior Member
Joined
Oct 13, 2010
Posts
128
Reaction score
20
Naomba kuwasilisha kero yangu hii kwa viongozi wa sekta ya elimu Tanzania. Kwa miaka kadhaa kumekuwa na tabia ya watungaji wa mitihani ya Kidato cha Nne hasa kwa masomo ya sanaa, kutumia lugha ngumu ya kiingereza katika maswali yao, hali inayopelekea wanafunzi wengi kufeli masomo hayo kwa sababu ya kujibu tofauti na swali lilivyouliza. Mfano, swali linataka mwanafunzi ajibu sababu zilizopelekea kitu fulani, mwanafunzi anajibu athari za kitu hicho na hivyo kukosa swali zima.

Ushauri wangu;

Kwa kuwa somo la kiingereza lipo, upimaji wa ujuzi wa mwanafunzi katika lugha hiyo ufanyike katika somo hilo. Kwa masomo mengine, maswali yaulizwe katika lugha nyepesi itakayoeleweka kwa wanafunzi wote. Mfano, kama swali linataka kupima ufahamu wa mwanafunzi kuhusu sababu ya kutokea kwa jambo, neno “causes” litumike badala ya kutumia maneno magumu ya kiingereza.

Kero hii imekatisha ndoto za Watanzania wengi sana hapa nchini, tuungane kusema, Inatosha.
 
Mfano wa hilo neno gumu ni lipi ? Ukizingatia mitihani mingi ni marudio tu ukicheza na past paper basi ushalenga paper, na nadhani hakuna jambo la muhimu sana kama kuelewa swali..., na sio mitihani tu hata humu huwa nashangaa watu unaanzisha post wanajibu kingine au mbaya zaidi unakuta mtu anaji contradict yaani sentensi ya kwanza anapinga alafu mwisho anakubaliana na alichokipinga...

Ushauri tu badala ya kulalamika lugha nyepesi itumike labda watu hao watumie muda kujifunza lugha..., hususan kwenye hayo masomo ya Sanaa..., sisi wadau wa physics na namba hatuna shida sababu numbers are the same in any language....
 
Mtihani ni kupima uwezo wa mtahiniwa kutegua changamoto.
Endapo utamtahini kwa maswali ya moja kwa moja maana yake utapima kiwango chake cha KUKARIRI siyo kiwango cha kuelewa...
___
Soma kwa bidii, jifunze mbinu mbalimbali za kutatua matatizo. Usikariri njia moja kama tembo!
 
Silabasi inasema kama hujui kingeredha basi wewe huna akili
Hivi, inakuwaje profesa mzima, kasoma kwa kutumia lugha ya Kiingereza kwa zaidi ya miaka 15 na bado hawezi kuitumia hiyo lugha kiufasaha?
 
Elimu bongo ni utopolo,Wacha wajue kusoma,kuandika na kuhesabu mengine watajifunza maishani.Sio lazima Kila mtu awe professional doctor, engineer au accountant.
 
Discuss the profounding amplifiers of II world war? 🤣🤣🤣
 
Walimu wa history na civics wana makusudi ya kujiona watu kumbe mabaki ya watumwa tu
 
Back
Top Bottom