Elections 2010 Maswali Magumu: Kikwete wa mtandao kageukia familia?

Elections 2010 Maswali Magumu: Kikwete wa mtandao kageukia familia?

Kuhangaika kwao kwa ashiria wanajua mwisho wao umewasili lakini wafanyaje?
 
Mtoto wa rais in action, Ridhiwani akemea majigambo, kejeli

Wednesday, 06 October 2010 20:06 newsroom


Na Mwandishi Maalumu, Mkuranga

WAGOMBEA kwa tiketi ya CCM na wapambe wao, wametakiwa kuacha majigambo, kejeli na matusi, ili kuondoa msuguano kati ya makundi yaliyoshinda na yaliyoshindwa kura ya maoni. Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM, Ridhiwani Kikwete, alisema hayo juzi, alipozungumza na viongozi wa Chama wilayani Mkuranga.
Alisema hivi sasa si wakati wa kuendeleza makundi, kwani wanaweza kukizamisha Chama. Ridhiwani alisema kazi iliyopo ni kuungana kuingia vitani kusaka ushindi wa CCM kwa kuiwezesha kupata kura za kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwishoni mwa mwezi huu. "Majigambo, kejeli na matusi si mahali pake sasa. Tuwe pamoja, tukipiganie Chama na tuhakikishe tunapata ushindi unaofanana na sura ya CCM. Tuachane na mambo yasiyo na tija kwetu, kwani yaliyopita si ndwele bali tugange yaliyopo na yajayo," alisema. Alisisitiza umoja na mshikamano ndani ya Chama utakaowezesha wagombea wa CCM wa urais, ubunge na udiwani kupata ushindi wa kishindo.
 
Historia inayaweka kwenye makabrasha yoote yanayotokea. Ipo siku watu watakimbia vivuli vyao wenyewe na siku hiyo haiko mbali sana.
 
huyo baba mkuu ni mfa maji ndo maana anatapatapa
 
Baba Rais na mgombea kutetea nafasi hiyo kupitia ssm kwa kodi zetu
Mama anapiga kampeni kutetea kile anachofaidi, ni mme wa Rais na mgombea kutetea nafasi hiyo kupitia ssm kwa kodi zetu
Riziwani anapiga kampeni kutetea wanachofaidi, ni mtoto Rais na mgombea kutetea nafasi hiyo kupitia ssm kwa kodi zetu
Huyu Miraji kikwete sijui ni ni nani lakini kama si mtoto basi ni ndugu wa Rais na mgombea kutetea nafasi hiyo kupitia ssm kwa kodi zetu, huyu nasikia anashirikiana na watu wajuzi wa computer IT kwenye NEC ili kuchakachua matokeo ya Urais, si mmesikia kuwa matokeo yatatumwa kwa njia ya internet?

kazi kwetu, mwenye zaidi aongeze, habari ndo hiyo

Ni mtoto wa nje wa JAKAYA KIKWETE, kwa mama flani wa pale kinondoni.....alikuwa mlevi sana wa pombe na huwa anafujo ukimwita kwenye paty, anapenda sana madem.
 
Hivi kweli tuko tayari kuongozwa na Mtu anayesema Uraisi ni Suala la Kifamili?
Nomba majibu hasa kutoka kwa wana CCM na mashabiki wa Kikwete Pale wanafamilia wanapofanya mambo bila ya idhini ya vikao vya chama, wanapoingilia shughuli za serekali tutapata matunda gani?
CHadema hii ni Agenda nzuri sana, waelezeni watanzania jinsi hii familia inavyoingia kwa kasi kwenye kuendesha nchi! Tunapoenda kunaweza kutokea machafuko kuanzia ndani ya CCM, mana nina uhakika wengi wananung'unika tu na kuwa WANAFIKI kwa kufikiria Kikwete ni mzuri kwao. 2005 alikuwa karibu na Mafisadi, huu ni muhula wake wa mwisho anataka kuwa karibu na Familia yake...huyu mpindisha Sheria anaweza kubadili katiba ili aweze kurithisha URAIS kwa familia yake!!!
Hafai kabisa kuogoza nchi!!
Inauma sana mkuu wa mkoa anapoamriwa kumfuata mtoto wa raisi, au mtoto/mke wa raisi kudai report kutoka kwa mkuu wa mkoa au kiongozi wa serekali!
Wana CCM msione aibu kumkataa Kikwete. Mkimkataa itakuwa ni kwa manufaa yenu, familia zenu na taifa kwa Ujumla!


I like this! Yaani ndg zangu CHADEMA msifanye kosa ktk hili. Msogezeeni Mh Slaa afunge magoli ya mwisho tena kwa kisigino!

Yaani baada ya miaka mitano familia ikiingia nakutoka ikulu wameamua kuibinafsi kuifanya taasisi ya familia? Mahali patakatifu pana najisiwa kiasi hicho? Hatujafika mahali pa taifa hiki kufanyiwa kampeni na mama, baba, na watoto. Mpaka sasa katiba inakataa mgombea binafsi kuepuka jambo kama hili la kubinafsisha nchi na juzi walikuwa wanakata keki kujifariji baada ya uchovu mwingi. Mimi na shangaa kweli watu wengine sijui wamelongwa! Nyie wanaCCm mliopigwa teke ninini kinachowafanya msipigie chama kingine kura ikawa fundisho maana hawaamini amewadharau amewapuuza, amewasusa akaamua wanael na mke ndio wawe forward naamini hata kinana na makamba anawalia chabo tu

Ila jamani kwakweli mtu huyu akashika tena uraisi itaimaliza nchi hii na atafanya hivyo makusudi maana niwavisasi na nikama anaona CCM wenzie wamemsusa na watanzania wamemsusa kwahiyo atvuruga kila kitu moja kuikomoa CCM na pili watanzania walioonyesha kumkataa.
 
guys tusiishie kupiga sound tu tukaacha kwenda kupiga kura.
 
guys tusiishie kupiga sound tu tukaacha kwenda kupiga kura.

Kupiga kura muhimu! Nyumba yangu tu chadema wanazo kura nne za nguvu na Kijijini wanazo kura za uhakika maana nimetwanga kampeni ya kutosha ccm wataponea wapi?
 
Nasikitika sana kuona watu hawa jinsi wanavyofanya kampeini na vyombo kama Tume ya uchaguzi vimeangalia tu kana kwamba hii ni nchi ya hii familia,Duuh hata nashindwa kujiproud kuwa Mtanzania kwa kuwa nimetembea nchi kadhaa na nimeshuhudia chaguzi na kampeni mbalimbali na nimesoma kampein za nchi za dunia hii sijapata kuona kama familia hii aibu tupu agghhhhah!!
Pili nataka kuwauliza wanawake hivi UWT ni umoja wa wanawake wa CCM au ni umoja wa wanawake wa Tanzania awe na chama au hana?Naomba jibu jema.Huu mpango wa kukusanya wanawake na kuwapa somo ati wachague CCM na nyie wanawake mnamsikiliza Salma Kikwete anawapigia uongo then mnashangilia,kumbukeni huyo anawadanganya by the end f the day hamtamuona tena huko vijijini kwenu,angalieni nyie mnaodanganywa ile mikopo inatoka mjini tu pia wanaangalia yule ni mke wa FISADI flani mpe,yule anayevaa vitenge vya wax mpe,yule mwenye Hotel ya kitalii mpe,Ss cha kushangaa wakati huu anakuja kwenu na haendi kwa wale waliopata mikopo,Angalieni nyie kina mama mnaouza bidhaa zenu sokoni mkipigwa na jua siku nzima,Mpeni Slaaaaaaa Dr real (PhD) mtatoka
 
Ha ha haaaaaa Hebu nikumbuke visuri.......... Hakuna ntu aliwahi kupata kura moja tu,
ktk umati ambao hata mkewe alikuwepo ?..... Ningojeni kesho nikishaamka,nitatathmini hali ile....... Labda jambo lilizua jambo pale !
 
Back
Top Bottom