Hivi kweli tuko tayari kuongozwa na Mtu anayesema Uraisi ni Suala la Kifamili?
Nomba majibu hasa kutoka kwa wana CCM na mashabiki wa Kikwete Pale wanafamilia wanapofanya mambo bila ya idhini ya vikao vya chama, wanapoingilia shughuli za serekali tutapata matunda gani?
CHadema hii ni Agenda nzuri sana, waelezeni watanzania jinsi hii familia inavyoingia kwa kasi kwenye kuendesha nchi! Tunapoenda kunaweza kutokea machafuko kuanzia ndani ya CCM, mana nina uhakika wengi wananung'unika tu na kuwa WANAFIKI kwa kufikiria Kikwete ni mzuri kwao. 2005 alikuwa karibu na Mafisadi, huu ni muhula wake wa mwisho anataka kuwa karibu na Familia yake...huyu mpindisha Sheria anaweza kubadili katiba ili aweze kurithisha URAIS kwa familia yake!!!
Hafai kabisa kuogoza nchi!!
Inauma sana mkuu wa mkoa anapoamriwa kumfuata mtoto wa raisi, au mtoto/mke wa raisi kudai report kutoka kwa mkuu wa mkoa au kiongozi wa serekali!
Wana CCM msione aibu kumkataa Kikwete. Mkimkataa itakuwa ni kwa manufaa yenu, familia zenu na taifa kwa Ujumla!