1. Mfugo hauna amri mbele ya mchunga.Hivi FIFA ina uwezo gani kuingilia hata ofisi?
Hivi FIFA ina uwezo gani kuingilia hata ofisi?
Wadau nimeiona hii kwenye Facebook page ya mwanaspoti
FIFA imeitaka TFF kuanza mchakato wa kuhamisha ofisi katikati ya Jiji na kurudi Ilipokuwa awali na ndani ya masaa 24 mchakato huo uwe umeanza
hata Ofisi nae mpaka FIFA WATUAMLIE
Kwa muda wa siku saba kuanzia tarehe 10/aug TFF tulipokea na kuwa na ujumbe wa wataalam sita toka FIFA.Wataalam hawa walikuwa ni wa ufundi,utawala,masoko na maendeleo ya mpira.Jukumu kubwa la ujumbe huu ilikuwa ni kutathmini muundo na utendaji wa shirikisho lengo likiwa ni kutafuta namna bora ya kuongeza ufanisi katika utendaji wa shirikisho.Wadau mbali mbali walikutana na ujumbe huu akiwemo Mh Waziri mwenye dhamana ya michezo,wadhamini wa sasa na wa zamani,vyombo vya habari,vilabu vya ligi kuu,viongozi wa TFF wa mikoa,watendaji wa TFF n.k.
Baada ya kukutana na wadau kadhaa kikao cha pamoja kilikaa kati ya kamati ya utendaji ya TFF na ujumbe wa FIFA na kufanya mapitio ya kile FIFA walichokiona.Maeneo makuu yaliyopitiwa ni pamoja na utawala na fedha,maendeleo ya mpira,mashindano na timu za Taifa.Mwisho wa kikao maazimio yalipitishwa juu ya mpango endelevu wa shirikisho na moja lilikuwa ni kuboresha mazingira ya utendaji kazi na usimamizi wa maendeleo ya mpira.Katika kipengele hiki ilionekana ni busara TFF irudi Karume lakini iboreshe mazingira ya ofisi ili yakidhi mahitaji ya kufanyia kazi .Aidha kwa kuzingatia mahitaji ya kiuchumi ya shirikisho FIFA wamekubali kushirikiana na TFF ,kupitia miradi yake mbali mbali, katika kuanzisha na kujenga miradi ya kiuchumi Karume.TFF itahakikisha hili linafanyika.
Hon. Eng. President Jamal Malinzi pamoja na mapungufu yako uliyonayo kama binadamu mwingine, you are the man of this time.
Asante kwa kuliweka sawa hili jambo la kurejesha ofisi za TFF pale Karume.
Vema na huu ndio uongozi kuwa mwepesi wa kujibuKwa muda wa siku saba kuanzia tarehe 10/aug TFF tulipokea na kuwa na ujumbe wa wataalam sita toka FIFA.Wataalam hawa walikuwa ni wa ufundi,utawala,masoko na maendeleo ya mpira.Jukumu kubwa la ujumbe huu ilikuwa ni kutathmini muundo na utendaji wa shirikisho lengo likiwa ni kutafuta namna bora ya kuongeza ufanisi katika utendaji wa shirikisho.Wadau mbali mbali walikutana na ujumbe huu akiwemo Mh Waziri mwenye dhamana ya michezo,wadhamini wa sasa na wa zamani,vyombo vya habari,vilabu vya ligi kuu,viongozi wa TFF wa mikoa,watendaji wa TFF n.k.
Baada ya kukutana na wadau kadhaa kikao cha pamoja kilikaa kati ya kamati ya utendaji ya TFF na ujumbe wa FIFA na kufanya mapitio ya kile FIFA walichokiona.Maeneo makuu yaliyopitiwa ni pamoja na utawala na fedha,maendeleo ya mpira,mashindano na timu za Taifa.Mwisho wa kikao maazimio yalipitishwa juu ya mpango endelevu wa shirikisho na moja lilikuwa ni kuboresha mazingira ya utendaji kazi na usimamizi wa maendeleo ya mpira.Katika kipengele hiki ilionekana ni busara TFF irudi Karume lakini iboreshe mazingira ya ofisi ili yakidhi mahitaji ya kufanyia kazi .Aidha kwa kuzingatia mahitaji ya kiuchumi ya shirikisho FIFA wamekubali kushirikiana na TFF ,kupitia miradi yake mbali mbali, katika kuanzisha na kujenga miradi ya kiuchumi Karume.TFF itahakikisha hili linafanyika.
Hivi zilihamia wapi..
Mheshimiwa Jamal Malinzi,
Idea ya kuinvest eneo la TFF Karume lilikuwa zuri sana hata mimi nakuunga mkono nafikiri tatizo lilikuwa ni approach tu,ukweli kwenda PPF ilikuwa ni expensive sana mngeweza kupata ofisi nafuu kuhusu hilo.Kama mwandishi anavyosema inawezekana wewe sio tatizo ila hao waliokuzunguka wanakuangusha inabidi uwe makini sana.Ulivyoingia uliwapa watu matumaini makubwa sana lakini hadi sasa unazidi kuwakatisha tamaa
Belo usipoteze matumaini,ninaongoza mpira katika mazingira magumu,lipo kundi dogo linataka niongoze mpira kwa kutatua crisis badala ya kuhangaika na mpango kazi wa maendeleo,usitishie shaka nina uwezo wa kulikabili,tutashinda na mpira utasonga mbele.Wanaodhani Malinzi atakata tamaa wajue hawatafanikiwa.Karume complex tutaijenga,youth development programme tutaijenga,mpira wa wanawake tutaujenga na Tanzania itang'ara kimataifa.