Maswali na ushauri kwa Malinzi


mkuu hivi unaelewa unachoandika mi naona unabwabwaja tu kwa akili km zako ndyo unadhani tutapiga hatua ,unaongelea mark time wakati tunatafuta suluhisho la kudum
 

Strange to relate that the FA have the money, the blueprint, the site and the target: to build a production line for international players and coaches so that England can escape the time-warp of 1966.
Hiyo ni dondoo mojawapo kwenye nakala hiyo. Nani angepingana na TFF iwapo nao wangekuwa na fedha, mpango kamili, eneo na lengo kama la FA au la FFF ambako makala hiyo imedokeza kuwa ndiko FA ilikoiga mfumo huo? Nani angepinga iwapo gharama wanazojiwekea TFF zisingepindukia walizotumia TP Mazembe kumsajili Samatta? Maana ndivyo jinsi kiwango walichopanga kutumia FA kwa ajili hiyo kinavyopimika kwa vigezo vya huku, kama ninavyonukuu kutoka makala hiyohiyo:
At a modest cost, the FA are creating a symbol, a store of knowledge, a system, a haven and a control centre for the sometimes shambolic English game. All that for less than Luis Figo cost Real Madrid.
Na bado, licha ya yote hayo, linabaki kuwa ni jambo la ajabu kwa Uingereza (strange to relate)!
 
Ndugu zangu inanipa faraja jinsi mnavyochangia,hii inaonyesha ni jinsi gani mnavyojali maendeleo ya mpira wetu.Tuipongeze timu yetu ya Taifa kwa ushindi wa leo vs Benin.
 
Ndugu zangu inanipa faraja jinsi mnavyochangia,hii inaonyesha ni jinsi gani mnavyojali maendeleo ya mpira wetu.Tuipongeze timu yetu ya Taifa kwa ushindi wa leo vs Benin.
Binafsi siwapongezi kwa ushindi bali soka la uhakika waliloonyesha, kama tutaendelea vile
bila shaka mzimu wa Msumbiji hautatusumbua tena.
 
mpira wa miguu nchi hii jamali malinzi unakazi kubwa mpira unahalibiwa na vyombo vya habari ujuaji umepita kiasi hapo mimi sielewi sijui umbumbu au utoto au ujinga ushamba au njaa kwa sababu utakuta vyombo hivyo vinachochea jambo bila ya kulifikiria kwa mfano jambo la makato ya kuendeleza vijana badala ya kutoa ushauri wa makato wao wanapinga kama wao wahusika mbona vyombo hivyo havihoji wa ndumbalo kumpitisha kaburu kugombea wakati alishajiuzuru?wakati katiba inamzuia kugombea mpaka muda upite miaka minne
 

saleh ally anajulikana fika ni team nyamlani kwahiyo asituzuge hapa na tenga wake ni kipi cha ajabu ambacho tenga amefanyia mpira wetu? tenga kakaa pale miaka nane zero tupu
 
tff hiki kiwanja cha majimaji mjini songea mbona hakipo safi?
Naiomba tff wakumbusheni wamiliki wa hiki kiwanja wakihudumie.

Timu zote zinazotoka dar kuja kucheza hapa songea zinapata taabu san na hali ya huu uwanja
 
Jamal Malinzi umeanza kuwafungia wale wasio kuunga mkono?Umeanza kuwafungia walr wanao kuhoji?

Hatukuyaona haya wkt wa Tenga na pls usiturudishe kwenye migogoro kama enzi za Ndolanga!Yaani hamna solution itakayofikiwa na mahasimu wako ila kufungiwa?
 
Last edited by a moderator:

Ndani ya week tu kamati imekutana imemfungia Wakili Ndumbaro kwa MIAKA 7 asijihusishe na soka la TZ!

Uharaka wa kesi hii umenipa sana wasi wasi ukitilia maanani wkt kesi inasikilizwa Ndumbaro alikuwa USA kikazi!

Hamna kitu nisicho kipenda kama kufukuzana badala ya ku compromise! Jamal Malinzi kashindwa tayari
 
Last edited by a moderator:
hahahahahaha...acje kutufungia na sisi humu ndani...
 

TFF inapoteza muelekeo kwa kweli...
Kuna watu wanalazimisha mambo kwa hoja ya nguvu badala ya nguvu ya hoja..Wanapenda wasikie wanachotaka wao tu..
Nina uhakika tunarudi zama za Ndolanga.
 
Last edited by a moderator:
Ni kazi kubwa sana ku deal na watanzania coz wengi Wao ni vigeugeu cku zote wamekuwa wakipigia kelele suala la soka ,Sasa Leo tff wamekuja na solution inayohusisha mchango kwa wadau wote vikiwemo vilabu,cha kushangaza hao hao wanaopiga kelele khs soka la vijana Leo hawataki kuskia proposal ya tff
 
mkuu fafanua with positive fact kuhakikisha mpira wetu unapiga hatua

Mkuu komeka, nakubaliana na ww 100% kuwa mpira tz haukui. Kinachopingwa ni proposal ya tff. Wengi tunaiona siyo workable. Hata malinzi analijua hili. Ila motive mbovu ya malinzi ndiyo inayomfanya akomalie hiyo proposal. Anataka afungue mwanya wa ufisadi. Mpira wa vijana unajengwa na vilabu, siyo na chama cha mpira cha taifa. Mimi ningekuwa wa kwanza kumuunga mkono angevikomalia vilabu kuwa na projects za youth soccer development. Ana uwezo mkubwa sana wa kuvilazimisha vilabu kufanya hivyo, na ataungwa mkono na kila mpenda soccer.

Cha ajabu, toka aingie madarakani hajawahi kuviamuru vilabu vifanye hivyo! Badala yake anarukia jukumu ambalo siyo lake, simply because anajua ndani yake kuna ulaji ambao siyo rahisi kuu-monitor!!
 
Last edited by a moderator:

Jamali mimi ninaomba kuuliza hivi timu za vijana huwa zinateuliwa kuangalia uwezo wa wachezaji au ni kuchukua wa Dar es Salaam pekee?
Pili unalishughulikiaje suala la kudanganya umri kwa wachezaji wa Tanzania?
Tatu kwanini mashindano ya kuibua vipaji kwa vijana yanapoisha hatuwaoni wakiendelezwa au kuitwa kwenye timu za vijana?
 
Last edited by a moderator:
tunakusubiri
 
Ningekuwa mm ni Jamal Malinzi tungebadili katiba ya TFF ili kila kilabu kiwe na team za vijana!Jumamosi kama Yanga na Simba zinacheza kwenye game ya ligi basi Ijumaa Yanga na Simba vijana lzm zicheze!Jumatano kama Azam anacheza na Stand ya Shinyanga huko Mwadui basi teams zao za vijana lzm zicheze siku moja kabla ya mechi ya wakubwa!!

Haya ya TFF kusimamia eti teams za watoto hayana maana yyt ile na yanakupotezea muda tu!Kuendeleza soka la TZ linahitaji ubunifu na wala sio kazi kubwa kama akina Malinzi wanavyo taka tuamini!Malinzi na wenzake hawapendi ushauri na ukiwashauri wanahisi kama umewaonea!

Uingereza FA kuanzisha programmes za watoto hali inaruhusu maana wana gym zao,wana academies zao,wana viwanja vyao,wana bajeti kubwa na wana wataalam wao!!Uanzishe soka la vijana kwa kocha Madadi?Bajeti ipo wapi?Gym na academies je?
 
Last edited by a moderator:
saleh ally anajulikana fika ni team nyamlani kwahiyo asituzuge hapa na tenga wake ni kipi cha ajabu ambacho tenga amefanyia mpira wetu? tenga kakaa pale miaka nane zero tupu
Ungejibu hoja za Saleh Ally ukaonyesha udhaiifu wake tungekuelewa vizuri hoja ya ko kuwa Saleh ana lake jambo. Kwa kutokufanya hivyo tumeelewa kuwa we ndo unamatatizo. Say the truth shame the devil ungezingatia hilo ungeeleweka. Istoshe kuwa na maadui haikwepeki kwa binadamu kama Malinzi ana maadui wake basi ndo afanye vizuri wazibe midomo akishindwa wataongezeka wapya na wazamani waatapata nguvu kubwa. Kwa hiyo asionyeshe madudu
 
Sorry Mr President, this is so boring na haya yote mnayooingea siyo watanzania waliyokutuma kuyafanya. Inaonekana wazi unaoongea nao sio wapenzi wa mpira hata kidogo bali officials wa upande wako ama wapambe wako. I do not dig it, hivi kweli hapa ni pa kuongelea habari za electronic tickets? au namna ya kuziba mianya? huu ndio usanii unaolaumiwa kuwa nao. Msijifanye kupuuza swala la ukabila hapa wewe upeo wako unaanzia kanyigo na kuishia hapo. Hapa tunaongelea leadership kwenye kitu muhimu sana football, si kweli watu wenye uwezo mdogo kama huo uliouweka kwenye uongozi wa TFF ni wahaya tu. Huwezi kusonga mbele pasipo ku address ugonjwa unaoonekana kuwepo TFF yako. Unamaana Tenga hakuwa na macho ya kuwaona hawa, mpaka ulipoingia wewe? Ungekua kiongozi bora ungetumia nafasi hii kutueleza vigezo ulivyotumia kuwapata hawa na hao uliowaacha,ama kuwatoa katika nafasi zao. Swala la Angetile linaeleweka hata mimi nisingependa kumuacha mtu kwenye nafasi muhimu kama yake, ambaye najua hakunitaka wazi wazi. Lakini hao wengine?

Majibu juu ya kuhamisha ofisi:
Swala hili limeandikwa mpaka kwenye magazeti nahapa naona unajikausha hulizungumzii, yale yale ya JK kuwa kelele za mpita njia hazimnyimi mwenye nyumba usinginzi, hii kweli tu kama TFF ama urais ungekua ni wa kampuni binafsi. Sisi sio wapita njia ndio hasa wenye nyumba wewe ndio mpita njia. Jibu kisomi ni kweli FIFA walikueleza kutoridhishwa kwao na uamuzi huo? Hili ni muhimu kwa kuwa linaonyesha kukubalika kwako ama kutokukubalika kwako na FIFA jambo ambalo ni muhimu sana kwa maendeleo ya mpira wa nchi yoyote. Hujatuambia pango la Karume lilikua shilingi ngapi na wapi unakotoa hizo 20m kila mwezi kulipia ofisi za PPF. Nilifikiri ungetuambia unalipia toka kwenye kampuni yako ya Cargo Star tungekuelewa

Mgogoro wako na Vilabu vya ligi daraja ya kwanza:

Hili swala lililoandikwa na vyombo vya habari na kuonekana kuwa na upinzani mkubwa na vilabu husika wakiwakilishwa na wakili Ndumbaro, mwanamichezo na msomi wa shahada ya Phd ya mambo ya media, limefikia wapi?

Program za football ya Vijana na Wanawake:
Hizi ni nadharia zako tosha maana hata hizo program unazozizungumzia hatujui umezitoa wapi wala hujatuambia kama uliwashirikisha wadau ama kuzitengeneza ama kuzijadili, unazo kabatini au mifukoni? program sio kichwa cha habari hizi ni siasa zako na hao vilaza wako

Huwezi kutaka kuvaa vazi safi juu ya lile chafu linalonuka uvundo. Watanzania wamekuambia mwaka sasa hakuna ulichofanya, nilitegemea jukwaa hili ambalo hata wewe umeliruia rudia maana ulishafungua thread kama hii huko nyuma mara kadhaa, lingetumika kujibu hoja zinazoshushwa kwako sio kupiga siasa. Wewe unajirudia rudia lakini wakikuuliza ukabila hutaki unadai ni kujirudia rudia, nimerudi huko kwenye majukwaa yako ya nyuma unakosema ulijibu hakuna ulichojibu ni pumba tu. kama ungekua na jibu na unaoana watu hawajaelewa ungelirudia kwa maneno machache.

Mwisho:
Acha kutuchosha thread hii haina tija, kaa chini jipange upya, shirikisha wadau katika mipango yako hata hiyo ya hizo program zilizoko kichwani kwako ziweke hadharani tuzijadili, TFF sio kampuni binafsi na huwezi kuiendesha kihayahaya football ni ya wazaramo kama mimi na makabil mengine yote, inatakiwa kutuunganisha sio kutugawa kama wewe, muite Tenga bado anaheshimika maana amefanya mambo yanayoonekana, kaa nae na timu yake iliyotoka washukuru kwa kazi nzuri weka mezani program zao acha wao wawe wa kwanza kutia neno.

Swala la udhanimi na changamoto zake
Limezungumzwa hapa kama swali na ushauri lakini unaonekana hutaki kulizungumza, yale yale unayodai ukizungumzia uhaya yataleta udini, ndio hayo unayokataa kuyazungumzia unapoulizwa itakuaje habari ya Azam na Beer companies, habari za Vodacom na ukataji ticket wakati si wapenzi wote wa mpira wa miguu wanaotumia mtandao wa voda, inamaana hauna wataalamu katika kamati yako ya fund mobilization na strategy kwa kuwa hukuangalia nje ya kanyigo

Tahadhari:
Kuna dalili zote za wazi za hatari ya wewe kuwa kiongozi wa kwanza wa zama hizi kupigiwa kura ya kutokua na imani. Hali yako sio nzuri kwa kuwa pamoja na utendaji wako mbovu, hujaanza kujijengea mitandao ya kukulinda hasa kwenye upande wa media, hao unaowatumia sio wanahabari, hata hapo ndani wengi wa watendaji ambao ama sio wa kabila lako ama wa kundi lako (inamaana ambao hawajaja na watu wako wapya) hawana imani na wewe, hawajui unachokifanya) bado unanafasi ya kujiokoa ukiamua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…