Maswali na ushauri kwa Malinzi

Maswali na ushauri kwa Malinzi

Ungejibu hoja za Saleh Ally ukaonyesha udhaiifu wake tungekuelewa vizuri hoja ya ko kuwa Saleh ana lake jambo. Kwa kutokufanya hivyo tumeelewa kuwa we ndo unamatatizo. Say the truth shame the devil ungezingatia hilo ungeeleweka. Istoshe kuwa na maadui haikwepeki kwa binadamu kama Malinzi ana maadui wake basi ndo afanye vizuri wazibe midomo akishindwa wataongezeka wapya na wazamani waatapata nguvu kubwa. Kwa hiyo asionyeshe madudu
hata kama hujui kusoma na picha huoni? saleh ally anamsifia tenga na kumponda malinzi, sasa ni kipi alichofanya tenga kwenye mpira wetu leo hii tunaweza kujivunia? tenga amekaa miaka nane tff iweje leo umsifie na kumlinganisha na mtu aliyekaa mwaka mmoja? kumbuka kipindi tenga anaingia madarakani watu wote tulikuwa tumechoka na madudu ya fat ndo maana wengi mnahisi tenga kafanikiwa, la muhimu malinzi apewe muda tu.
 
Jamali mimi ninaomba kuuliza hivi timu za vijana huwa zinateuliwa kuangalia uwezo wa wachezaji au ni kuchukua wa Dar es Salaam pekee?
Pili unalishughulikiaje suala la kudanganya umri kwa wachezaji wa Tanzania?
Tatu kwanini mashindano ya kuibua vipaji kwa vijana yanapoisha hatuwaoni wakiendelezwa au kuitwa kwenye timu za vijana?

Jumamosi kwenye mkutano kati yangu na vilabu vya ligi kuu kocha wa timu ya Taifa Maart Nooij alitangaza program ya kitaifa ya kuboresha Taifa stars.Kuanzia mwezi Novemba kila mwezi atakuwa anaweka kambi ya siku mbili vijana umri chini ya miaka 23,lengo ni kuandaa timu itakayoshiriki CHAN june mwakani.Wengi wa vijana hawa wametoka program ya maboresho lakini pia wanatoka timu za madaraja ya chini kama Kahama FC.Scouting inaendelea kuboresha kikosi hiki.
Kudanganya umri ni kosa kubwa sana,majuzi Gambia walifungiwa na CAF miaka miwili,mwaka 2005 tulifungiwa na CAF juu ya Nurdin Bakari kudanganya umri.Sasa hivi bila kipimo cha MRI mchezaji haruhusiwi mashindano ya vijana.Anayedanganya umri ajue anajidanganya maana katika ngazi ya kimataifa atakamatwa tu,mashine hazidanganyi.
 
hata kama hujui kusoma na picha huoni? saleh ally anamsifia tenga na kumponda malinzi, sasa ni kipi alichofanya tenga kwenye mpira wetu leo hii tunaweza kujivunia? tenga amekaa miaka nane tff iweje leo umsifie na kumlinganisha na mtu aliyekaa mwaka mmoja? kumbuka kipindi tenga anaingia madarakani watu wote tulikuwa tumechoka na madudu ya fat ndo maana wengi mnahisi tenga kafanikiwa, la muhimu malinzi apewe muda tu.

nguvu do not waste your breath on the likes of Saleh Ali,i know what is going on.Tenga alitujengea taasisi nzuri,kazi kaikamilisha,tunamshukuru,kazi iliyoko mbele yetu sasa ni kujenga mifumo thabiti ya mpira wa watoto na wa vijana grassroot na youth football.Kujenga misingi hii maana yake ni ku train coaches,referees,doctors and adminstrators.Pia tunajenga mfumo imara wa soccer academies tukianza kwa kuziongezea uwezo hizi zilizopo kwa kutrain makocha wao na kuwapa vifaa.Tunataka tuhakikishe kila mkoa mpira wa vijana unachezwa kwa kuwezesha mikoa na kuanzisha michuano ya vijana ya mikoa.It is expensive inabidi tutafute vyanzo madhubuti vya fedha za kuendeshea program hizi.Tujipange tutafanikiwa.
 
Last edited by a moderator:
Ningekuwa mm ni Jamal Malinzi tungebadili katiba ya TFF ili kila kilabu kiwe na team za vijana!Jumamosi kama Yanga na Simba zinacheza kwenye game ya ligi basi Ijumaa Yanga na Simba vijana lzm zicheze!Jumatano kama Azam anacheza na Stand ya Shinyanga huko Mwadui basi teams zao za vijana lzm zicheze siku moja kabla ya mechi ya wakubwa!!

Haya ya TFF kusimamia eti teams za watoto hayana maana yyt ile na yanakupotezea muda tu!Kuendeleza soka la TZ linahitaji ubunifu na wala sio kazi kubwa kama akina Malinzi wanavyo taka tuamini!Malinzi na wenzake hawapendi ushauri na ukiwashauri wanahisi kama umewaonea!

Uingereza FA kuanzisha programmes za watoto hali inaruhusu maana wana gym zao,wana academies zao,wana viwanja vyao,wana bajeti kubwa na wana wataalam wao!!Uanzishe soka la vijana kwa kocha Madadi?Bajeti ipo wapi?Gym na academies je?

Natumaini unaelewa vyema mfumo wa uendeshaji wa vilabu vyetu.Ukiondoa Azam bila shaka unajua nini kinaendelea kwingine kuhusu youth football.Kama unaelewa kwa undani nini kinaendelea bila shaka utaona kwa nini TFF tumeamua kusema sasa basi something must happen.Tunaanza na program ya kitaifa umri chini ya miaka 23 kujiandaa na CHAN qualifiers,tunaanza na program ya kitaifa umri chini ya miaka 14 kujiandaa na Africa U17 qualifiers 2016,tunaanza na program ya kitaifa umri chini ya miaka 13. Kujiandaa na Fainali za Afrika U17 mwaka 2017,wale U17 waliotolewa mashindanoni mwaka huu tumewatafutia tayari ligi za madaraja ya chini wakomae,muda wa kuzungumza tuzungumze lakini na vitendo viwepo.
 
Last edited by a moderator:
hata kama hujui kusoma na picha huoni? saleh ally anamsifia tenga na kumponda malinzi, sasa ni kipi alichofanya tenga kwenye mpira wetu leo hii tunaweza kujivunia? tenga amekaa miaka nane tff iweje leo umsifie na kumlinganisha na mtu aliyekaa mwaka mmoja? kumbuka kipindi tenga anaingia madarakani watu wote tulikuwa tumechoka na madudu ya fat ndo maana wengi mnahisi tenga kafanikiwa, la muhimu malinzi apewe muda tu.
Saleh hajalinganisha watu hawa katika hoja yake kataja mapungufu ya Malinzi hivyo kimantiki ulitakiwa upinge au utoe utetezi kuonyesha kuwa hoja ya\ Saleh ni dhaifu. Lakini kusematu huyo ni team Nyamlani hakumfanyi Malinzi awemsafi. Two wrongs canot make it right
 
Jumamosi kwenye mkutano kati yangu na vilabu vya ligi kuu kocha wa timu ya Taifa Maart Nooij alitangaza program ya kitaifa ya kuboresha Taifa stars.Kuanzia mwezi Novemba kila mwezi atakuwa anaweka kambi ya siku mbili vijana umri chini ya miaka 23,lengo ni kuandaa timu itakayoshiriki CHAN june mwakani.Wengi wa vijana hawa wametoka program ya maboresho lakini pia wanatoka timu za madaraja ya chini kama Kahama FC.Scouting inaendelea kuboresha kikosi hiki.
Kudanganya umri ni kosa kubwa sana,majuzi Gambia walifungiwa na CAF miaka miwili,mwaka 2005 tulifungiwa na CAF juu ya Nurdin Bakari kudanganya umri.Sasa hivi bila kipimo cha MRI mchezaji haruhusiwi mashindano ya vijana.Anayedanganya umri ajue anajidanganya maana katika ngazi ya kimataifa atakamatwa tu,mashine hazidanganyi.

Asnte kwa majibu yako ingawa umekwepa kueleza kwanini timu ya vijana kujaa sura za Dar es Salaam.

Mimi naomba nishauri kuwa mpira haswa kwa vijana haukui kwani umewekewa msisitizo Dar peke yake, na hata hizo sports center zinajengwa Dar tu Je kwanini msipeleke maeneo ya nyanda za juu na ambazo zina hali ya hewa nzuri na mazingira mazuri kama Iringa, Mbeya, Arusha, Mwanza, Manyara nk kwani naona Dar siasa ni nyinyi kuliko maendeleo halisi ya mpira tunyo yataka.
Mwisho naomba muanzishe utaratibu wa lazima kwa vilabu vikubwa na mikoa ambayo kuna timu za ligi kuu au hata daraja la kwanza kujenga vituo vya mpira ili vijana waweze kukaa katika hivyo vituo wasome na kujifunza mpira
 
Saleh hajalinganisha watu hawa katika hoja yake kataja mapungufu ya Malinzi hivyo kimantiki ulitakiwa upinge au utoe utetezi kuonyesha kuwa hoja ya\ Saleh ni dhaifu. Lakini kusematu huyo ni team Nyamlani hakumfanyi Malinzi awemsafi. Two wrongs canot make it right
nimekuelewa saleh,
 
Kitendo cha kumfungia Ndumbaro kimeonesha jinsi gani uongizi wako ulivuo ba mapungufu, kiutendaji na kifikra, inaonekana uongozi webu hauhitaji challenges (changamoto) na hii ipo kuanzia kuanzia ngazi ya vilabu hadi TFF kwenyewe... Tunaona watu wanafungiwa kwa sababu tu ya kukosoa au kupingana na baadhi ya masuala na uongozi, which is not fair... Everywhere kuna challenges utafungia wangapi? Fanyia kazi changamoto jibu hoja za ndumbaro kwa hoja bora kabisa uone kama kuna atakae kua against... Ubabe wa kutumia Rungu la madaraka kumdhibiti wanao question utendaji si uadirifu... Jamal tulikutegemea, na naamin ukirekebisha tutaendelea kukutegemea kwenye maendeleo ya mpira hapa kwetu... #Advise
 
Jamal Malinzi umeanza kuwafungia wale wasio kuunga mkono?Umeanza kuwafungia walr wanao kuhoji?

Hatukuyaona haya wkt wa Tenga na pls usiturudishe kwenye migogoro kama enzi za Ndolanga!Yaani hamna solution itakayofikiwa na mahasimu wako ila kufungiwa?

punguzeni mahaba jamani, kipindi cha tenga kuna watu hadi walifungiwa maisha au umesahau? bila jk kuingilia kati kuna watu tungewasahau kabisa kwenye mpira wetu
 
Last edited by a moderator:
punguzeni mahaba jamani, kipindi cha tenga kuna watu hadi walifungiwa maisha au umesahau? bila jk kuingilia kati kuna watu tungewasahau kabisa kwenye mpira wetu
Sifa kubwa ya Tenga ni kwamba ametuachia mfumo mzuri (structures) za uendeshaji wa mpira wetu.Tuheshimu mfumo tuliojiwekea,penye malalamiko tufuate taratibu kuelezea ambalo hatujaridhika nalo,good governance.
 
Kitendo cha kumfungia Ndumbaro kimeonesha jinsi gani uongizi wako ulivuo ba mapungufu, kiutendaji na kifikra, inaonekana uongozi webu hauhitaji challenges (changamoto) na hii ipo kuanzia kuanzia ngazi ya vilabu hadi TFF kwenyewe... Tunaona watu wanafungiwa kwa sababu tu ya kukosoa au kupingana na baadhi ya masuala na uongozi, which is not fair... Everywhere kuna challenges utafungia wangapi? Fanyia kazi changamoto jibu hoja za ndumbaro kwa hoja bora kabisa uone kama kuna atakae kua against... Ubabe wa kutumia Rungu la madaraka kumdhibiti wanao question utendaji si uadirifu... Jamal tulikutegemea, na naamin ukirekebisha tutaendelea kukutegemea kwenye maendeleo ya mpira hapa kwetu... #Advise
Mimi na kamati yetu ya utendaji hakuna mwoga wa changamoto,i cherish a good healthy debate,lakini utaratibu ufuatwe.
 
Sifa kubwa ya Tenga ni kwamba ametuachia mfumo mzuri (structures) za uendeshaji wa mpira wetu.Tuheshimu mfumo tuliojiwekea,penye malalamiko tufuate taratibu kuelezea ambalo hatujaridhika nalo,good governance.

Wajua shida ya viongozi wengi hivi sasa ni mwataka kutawala na si kuongoza.

Kiongozi mzuri ni mwenye kuketi na waongozwa wake ambao ndo kwa haki viongozi wake wampe namna ya vile watakavyo wao walio mchagua naye afanze mashauriano nao.

Sasa hizo taratibu uzisemazo kimaandishi ni kweli hivyo ndo ipasavyo, walaakin sie tulopembeni yenyu twakuoneni maneno yenyu tofauti kabisa kabisa tena kabisa na matendo yenyu.


Haya we are waiting good governance by actions not by writing and reading in the office and media.

Ahsanta na nipo kipembeni hapa nakufuatiza yako majawaba.
 
Mimi na kamati yetu ya utendaji hakuna mwoga wa changamoto,i cherish a good healthy debate,lakini utaratibu ufuatwe.
Seriously? Wewe na kamati yako mnafuata utaratib? Mnamfungia mtu 7years kwa ku advocate wateja wake?? No wonder hakukua hata na nafasi ya natural justice... B'se mtuhumiwa yuko Usa... Tena kama ni maamuzi ya kamati i sniff rat on our football fate... Collective measures?? Sio decision ya mtu mmoja? Basi hatuna viongozi trust me....
Nakupa mfano... Hans Pope alitoa msimamo wa Wamiliki wa malori ya mafuta kugoma kodi za WAZIRI tena mkorofi... Serikali/Wizara haikumfungia Pope unajua kwa nn? He is just a representative (chairman) wa Wamiliki wa malori ya mafuta...
Lean between the line brother mpira na maendeleo yake ni manufaa ya Taifa/África... Ndio maana hua tunaishangilia Cameron, Nigeria.
Nafasi bado ipo rekebisha io... Kutereza si kuanguka..
 
Mh. Malinzi juzi wewe na uongozi wako mmetimiza mwaka mmoja tangu mliposhinda uchaguzi mkuu TFF,
BIRTHDAY itakuwa wapi tukate keki??
 
Seriously? Wewe na kamati yako mnafuata utaratib? Mnamfungia mtu 7years kwa ku advocate wateja wake?? No wonder hakukua hata na nafasi ya natural justice... B'se mtuhumiwa yuko Usa... Tena kama ni maamuzi ya kamati i sniff rat on our football fate... Collective measures?? Sio decision ya mtu mmoja? Basi hatuna viongozi trust me....
Nakupa mfano... Hans Pope alitoa msimamo wa Wamiliki wa malori ya mafuta kugoma kodi za WAZIRI tena mkorofi... Serikali/Wizara haikumfungia Pope unajua kwa nn? He is just a representative (chairman) wa Wamiliki wa malori ya mafuta...
Lean between the line brother mpira na maendeleo yake ni manufaa ya Taifa/África... Ndio maana hua tunaishangilia Cameron, Nigeria.
Nafasi bado ipo rekebisha io... Kutereza si kuanguka..

Simbajr kwa mfumo wa kimahakama tuliojiwekea si vyema adminstrators tukazungumzia maamuzi ya judicial commitees,nikuhakikishie haki ilitendeka.
 
Last edited by a moderator:
Hehehehehe... I trust u bro!!
All the best.... Kama unaona la kukufaa naamini utachukua... Kama hamna achana nalo... My bad.
 
Back
Top Bottom