Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Rais mkutano mkuu wa kawaida utafanyika lini?
Kombe la Fa limepotelea Wapi?
Jamal Malinzi
mashindano ya vijana U20 ngazi ya vilabu yatafanyika na hayatafanyika dar es salaam.Punde atatangazwa mdhamini mpya wa mashindano haya ya vijana umri chini ya miaka 20Jamal Malinzi nasikia mashindano ya VIJANA ya TIMU B za vilabu hayatakuwepo mwaka baada ya alikua akisaidia na si kudhamini kampuni ya SSB kupitia UHAI na kuitwa UHAI CUP kujitoa....hii unaizungumziaje ukizingatia ulikuwa ukitambulisha kama muumini wa SOKA la VIJANA inakuaje tunakosa UDHAMINI wa hayo MASHINDANO?...je tutaunda timu bora ya taifa kwa mtindo huu?...TFF mlipotangaza kuwa mnataka kuwa wenyeji wa mashindano ya VIJANA africa mlikua mnajua hao vijana pakuwapata...
Achana na Malinzi, yeye anajali maslahi yake tu si mpira as such, hata akitoa povu kuwa anataka kuendeleza mpira wa vijana. Ndiyo hao hao wakina James Rugemalila, utapeli tu
Achana na Malinzi, yeye anajali maslahi yake tu si mpira as such, hata akitoa povu kuwa anataka kuendeleza mpira wa vijana. Ndiyo hao hao wakina James Rugemalila, utapeli tu
MWANGUKU amanyise ninakuomba ufuatilie kwa karibu programu zetu za vijana,kwa mfano fuatilia:
- mpango wa kuunda kikosi cha Taifa cha watoto umri chini ya miaka 13 kitakachokua pamoja kuelekea fainali za Afrika umri chini ya miaka 17 mwaka 2019.
- mpango wa kuunda kikosi cha taifa umri chini ya miaka 14 mwaka huu,kikosi kitakachokaa pamoja LordBaden school kujiandaa na Africa qualifiers under 17 mwaka 2016
- mpango wa Taifa wa kuhakikisha kila mkoa unakuwa na youth football centre kwa ajili ya age group 8-17
- uanzishwaji wa kombe la Taifa la wanawake Desemba mwaka huu
-uanzishwaji wa Federation cup (kama kombe la FA) mwakani
-Fuatilia kwa karibu training kubwa ya makocha leseni za CAF,such a massive training programme for coaches has never happened in Tanzania. Tumefanya hivi baada ya kung'amua bila walimu wa kutosha nchii hii mpira hautafundishika
- Tunao watoto wanakaribia mia moja Dar,Moro,Mwanza ambao wana umri kati ya miak 11-15 wanafundishwa uamuzi wa mpira,30 kati yao wamekwisha fanya kozi ya FIFA,hawa ndo waamuzi wa baadae ambao tunaamini kwa programu tuliyowatengenezea watakuja kuwa marefa Afcon na world cup finals.
Ndugu zangu yote yanawezekana kikubwa ni mshikamano.Pamoja tutajenga.
Suala la CEO wa bodi ya ligi ni nyeti,litajadiliwa wiki ijayo kwenye kikao cha kamati ya utendaji.Kwa sasa ligi imesimama hivyo shughuli za bodi si nzito sanarais baada ya kumaliza muda wake aliyekuwa mkurungenzi wa bodi ya ligi tumeshuhudia ofisi hiyo akikaimishwa katibu muhitasi hapa unasemaje?
ikumbukwe ofisi hii ni nyeti sana hasa namna ya kutafuta wafadhiri juu ya kubaoresha ligi daraja la kwanza na ligi kuu, pale ofisini naona kuna baadhi ya vijana wana elimu ya kutosha iweje waachwe achukuliwe mtu kama huyo napata mashaka sana RAIS
Rais wakati unaingia madarakani ulitwahidi kuwa mpira utachezwa nchi nzima hapa unasemaje?
Pia Rais ulisema umeagiza vifaa vya michezo kwa ajili ya watoto hasa kuanzia miaka 12 na kuendelea mashuleni na ukasema umepakia kwenye makontena viatu used na mipira size 2,3,4 hapo unasemaje?
Rais naomba nikuulize swali dogo,
Mkuu vipi kuhusu ziara zako za kutembelea wanachama wako ili kujionea utendaji kazi wao imeishia wapi? ikumbukwe ni mikoa miwili tu ninayojua umeisha enda nayo ni Songea na Kilimanjaro.
swali lingine ni kuhusu deni mnalodaiwa na PUNCHLINE lakini nashangaa amekamata basi lako lakini bado unampa kazi kulikoni?
Jamal Malinzi, umefungwa hata na Burundi tena kwenye sherehe za Uhuru, inabidi uachie ngazi haraka sana.
cc Bushoke