Maswali na ushauri kwa Malinzi

Maswali na ushauri kwa Malinzi

Ongea na serikali hasa wizara ya elimu iteue shule moja ya sekondari na shule moja ya msingi yenye eneo la kutosha kutoka kila mkoa alafu mzitengenezee miundo mbinu ya kimichezo ili ziwe shule maalumu za kimichezo kwa soka la wanaume na wanawake yaani vijana wenyevipaji watakao kuwa wanaimbuliwa kutoka michuano mbalimbali kimkoa wanawekwa pamoja na huku wanaendelea na masomo yao. Shue hizi ndizo zitakazo kuwa mazizi ya wanamichezo lakini mkiwa na lengo la kufika ngazi ya wilaya baada ya ngazi ya mikoa kuimarika.Kwa mtazamo wangu ni kuwa tutakuwa tumelea vipaji vya lika lote kwa urahisi. Wazazi wanaweza kuchangia sehemu ya gharama za chakula na vifaa,TFF mkachangia gharama za wataalamu na michezo na serikali ikabaki na jukumu la uendeshaji kwa ujumla.

Ili wazo zuri..
Tena wanaweza hata amua Shule zenye viwanja zkapewa nafasi ya kukarabatiwa japo viwanja tu ili vikizi vigezo.
Wazo zuri kama likiwekwa chini kitaalam.
Maana mpira wa sasa unaambatana na Elimu.
hii pia itawapa nafas za kupata scholarships za michezo kwa nchi mbali mbali.
 
Kumbuka hizo ni mechi za kirafiki za kukisuka kikos cha taifa stars
Lakini pia kwa wafuatiliaji wa mpira wa afrika mashariki Burundi ya leo kimpira sio ya miaka 20 iliyopita.Burundi ya leo ina wachezaji wawili kwenye English premier league Saido na bigirimana.Burundi ya leo ina wachezaji karibia kumi kwenye ligi yetu ya VPL.Burundi ya leo ina football academies mbili na sports centres za kueleweka.Kutokana na udogo wa nchi kila jumatatu na jumanne timu yao ya Taifa ina train kwa kujumuisha wachezaji wa ndani.Kwa taarifa ya wadau wa thread hii Burundi vifaa vya michezo havilipiwi kodi hata senti tano Tanzania mpira mzuri adidas original bei yake sh laki tatu kisa kodi.Tutafakari.
 
Ongea na serikali hasa wizara ya elimu iteue shule moja ya sekondari na shule moja ya msingi yenye eneo la kutosha kutoka kila mkoa alafu mzitengenezee miundo mbinu ya kimichezo ili ziwe shule maalumu za kimichezo kwa soka la wanaume na wanawake yaani vijana wenyevipaji watakao kuwa wanaimbuliwa kutoka michuano mbalimbali kimkoa wanawekwa pamoja na huku wanaendelea na masomo yao. Shue hizi ndizo zitakazo kuwa mazizi ya wanamichezo lakini mkiwa na lengo la kufika ngazi ya wilaya baada ya ngazi ya mikoa kuimarika.Kwa mtazamo wangu ni kuwa tutakuwa tumelea vipaji vya lika lote kwa urahisi. Wazazi wanaweza kuchangia sehemu ya gharama za chakula na vifaa,TFF mkachangia gharama za wataalamu na michezo na serikali ikabaki na jukumu la uendeshaji kwa ujumla.

chibasi hili wazo kuntu nakushukuru.Pamoja na hayo TFF tumeamua to take the bull by the horn.Kuanzia January wachezaji bora umri chini ya miaka 13 kwa gharama za TFF na washirika wetu tutawasomeaha Alliance academy mwanza na wale chini ya miaka 14 tutawasomeaha Lord baden school Bagamoyo.Tutazidi kufuatilia wazo lako ili shule za kuchukua hawa watoto wenye vipaji maalum vya mpira zizidi kuongezeka.Lakini pia wakati huo huo tuzidi kusomesha makocha maana hizi programu bila makocha wa maana ni bure.
 
Last edited by a moderator:
chibasi hili wazo kuntu nakushukuru.Pamoja na hayo TFF tumeamua to take the bull by the horn.Kuanzia January wachezaji bora umri chini ya miaka 13 kwa gharama za TFF na washirika wetu tutawasomeaha Alliance academy mwanza na wale chini ya miaka 14 tutawasomeaha Lord baden school Bagamoyo.Tutazidi kufuatilia wazo lako ili shule za kuchukua hawa watoto wenye vipaji maalum vya mpira zizidi kuongezeka.Lakini pia wakati huo huo tuzidi kusomesha makocha maana hizi programu bila makocha wa maana ni bure.

Rwanda pia wana utaratibu mzuri sana...niliwahi kuongea na vicent rais wa ferwafa...kipindi cha kagame cup...iliwasaidia kupata timu iliyoshiriki world cup under 21 kule Mexico
 
Last edited by a moderator:
Rwand sasa ni ya 68 duniani tanzania ya 105,uganda ya 76...duuuuh
 
...Rwanda waliamua kwa makusudi kbs..

huwezi kuvuna pale ambapo hujapanda.Angalia leo ukanda wa afrika kusini,hivi tunavyoongea Zambia na south africa mwaka huu pekee wameingiza timu nne fainali za africa (wanawake Namibia,U17 niger 2015,U20 senegal 2015 na Afcon eq guinea 2015).Yaani correlation ni straight forward nchi zinazo perform continental youth finals zinakuwa na nafasi nzuri kucheza fainali za Afcon na WC.Bahati mbaya sponsors wanapenda finished product ambayo ni national team,za vijana wanazipa kisogo Zambia ni 100% gharama ya serikali.
 
Rwand sasa ni ya 68 duniani tanzania ya 105,uganda ya 76...duuuuh

Ukifuatilia success story ya Rwanda kimpira baada ya 1994 utajua nini maana ya youth football.Wao walikaa na kuamua na tunavyozungumza Rwanda kama nchi tayari wameandaa fainali mbili za Afrika umri chini ya miaka 17 na 20.Mwaka 2016 Rwanda ni wenyeji wa fainali za Afrika wachezaji wa ndaniCHAN.Ndio maana na sisi tumeamua 2019 tuwe wenyeji wa fainali za Afrika umri chini ya miaka 17.
 
hongera RAIS kwa nia ya kuusaidia mpira wetu usonge mbele.
RAIS lakini naona hukujipanga vizuri wakati wa uteuzi wa kamati mbalimbali maana naona wajumbe wako uliowateua baadhi hawakusaidii kuendeleza mpira na umeachwa kama mtoto yatima na kusabaisha shughuli nyingi za tff kuzifanya wewe mwenyewe je unalizungumziaje hili?
mimi binafsi simjui mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi na wajumbe wake hata sijawahi sikia wametoa ratiba ya chaguzi za MOROGORO na MARA
 
sisi mashabiki wa mpira wa miguu tunakutuma wambie watangazaji wa azamtv tabia ya kukejeri timu za simba na yanga zinapocheza hatutaki wao watangaze mpira tu kama jana simba na kagera ooh mara simba imefanya usajiri hawaoni wanachofanya na yanga vivyo hivyo mbona wale wa studio wanasema vizuri sasa hawa watangazaji ndio kujibembereza kwa bakareza wape onyo
 
sisi mashabiki wa mpira wa miguu tunakutuma wambie watangazaji wa azamtv tabia ya kukejeri timu za simba na yanga zinapocheza hatutaki wao watangaze mpira tu kama jana simba na kagera ooh mara simba imefanya usajiri hawaoni wanachofanya na yanga vivyo hivyo mbona wale wa studio wanasema vizuri sasa hawa watangazaji ndio kujibembereza kwa bakareza wape onyo

Wasipobadilika, mkataba ukiisha na wao kwishney!
 
sisi mashabiki wa mpira wa miguu tunakutuma wambie watangazaji wa azamtv tabia ya kukejeri timu za simba na yanga zinapocheza hatutaki wao watangaze mpira tu kama jana simba na kagera ooh mara simba imefanya usajiri hawaoni wanachofanya na yanga vivyo hivyo mbona wale wa studio wanasema vizuri sasa hawa watangazaji ndio kujibembereza kwa bakareza wape onyo

ahsante nitalifikisha.
 
Ndugu zangu niwatakieni kheri ya mwaka mpya,uwe wa kheri na fanaka kwa nchi yetu.
 
Mkuu kwenye soka la vijana ndo ukazie zaidi na watafutwe kila pembe ya mkoa,na mtu apate nafas kwa kpaji,c kwakuwa nduguye nan au anacheza tmu gan tutafka, hayo yakzngatiwa,
 
Ndugu zangu niwatakieni kheri ya mwaka mpya,uwe wa kheri na fanaka kwa nchi yetu.

Asante na wewe pia, mkuu vp suala la kupromote ligi daraja 2 hata tuweze kujua ratiba!! Inauma sana eti uko mjini ndo unajua kuna mechi ya chama lako
 
chibasi hili wazo kuntu nakushukuru.Pamoja na hayo TFF tumeamua to take the bull by the horn.Kuanzia January wachezaji bora umri chini ya miaka 13 kwa gharama za TFF na washirika wetu tutawasomeaha Alliance academy mwanza na wale chini ya miaka 14 tutawasomeaha Lord baden school Bagamoyo.Tutazidi kufuatilia wazo lako ili shule za kuchukua hawa watoto wenye vipaji maalum vya mpira zizidi kuongezeka.Lakini pia wakati huo huo tuzidi kusomesha makocha maana hizi programu bila makocha wa maana ni bure.

Andaeni basi na kozi za awali za ukocha kwa walimu wa sekondari na msingi, ikibidi zitangazwe kupitia Halmashaur tuko tayari kujilipia sababu hata hizi kozi kupata tu taarifa tunabaniwa.
Uwekezaji kwa walimu ni mrahisi sababu tunakaa na watoto shuleni kwa zaidi ya miaka 4 ni rahisi kwetu kunurture vipaji vyao.
Na lingine kwa nini copacoca cola ina ada kubwa ya ushiriki?? Shule zetu haziwezi kugharamia kushiriki!!
 
Last edited by a moderator:
Hongera RAIS
kwa uamuzi wako mzuri wa kufanyia marekebisho Kamati ya waamuzi. lakini bado kuna changamoto mpya iliyopo juu ya kamati uliyoiunda ya kukushauri wewe juu ya masuala ya waamuzi ambayo haipo kikatiba, je haitaleta mgongano wa kimaslahi baina ya kamati hizi mbili? na ukumbuke baadhi ya wajumbe wa hii kamati ya kukushauri walikuwa kwenye kamati ya waamuzi na walikua na element ya RUSHWA japo umemwacha mmoja,
 
Andaeni basi na kozi za awali za ukocha kwa walimu wa sekondari na msingi, ikibidi zitangazwe kupitia Halmashaur tuko tayari kujilipia sababu hata hizi kozi kupata tu taarifa tunabaniwa.
Uwekezaji kwa walimu ni mrahisi sababu tunakaa na watoto shuleni kwa zaidi ya miaka 4 ni rahisi kwetu kunurture vipaji vyao.
Na lingine kwa nini copacoca cola ina ada kubwa ya ushiriki?? Shule zetu haziwezi kugharamia kushiriki!!

Pukudu mlitozwa hela kushiriki copacoca cola? nani alifanya hivyo? naomba details nitumie president@tff.or.tz au sms/whattsup 0754815543.
Tukifungua mawasiliano nitakupa na details za kozi za ukocha.Ni kweli tuna dhamira kubwa kuwaendeleza makocha mashuleni.
 
Last edited by a moderator:
Hongera RAIS
kwa uamuzi wako mzuri wa kufanyia marekebisho Kamati ya waamuzi. lakini bado kuna changamoto mpya iliyopo juu ya kamati uliyoiunda ya kukushauri wewe juu ya masuala ya waamuzi ambayo haipo kikatiba, je haitaleta mgongano wa kimaslahi baina ya kamati hizi mbili? na ukumbuke baadhi ya wajumbe wa hii kamati ya kukushauri walikuwa kwenye kamati ya waamuzi na walikua na element ya RUSHWA japo umemwacha mmoja,

ikizu katiba ya TFF inaruhusu uundwaji wa kamati kama hizi.Tahadhari nitachukua kuhusu ulilolisema. Uchaguzi Mara na Morogoro tunaandaa.
 
Last edited by a moderator:
mkuu pole kumbe hujui mikoa inayotoza ada ya ushiriki ya copacocacola basi ni hii hapa ifanyie kazi,
1-Kigoma
2-Mwanza.
ila mkuu kwa kigoma hata jezi mnazowagawia watoto mwisho wa mashindano hunyang'anywa na kuziuza mtaani
 
Back
Top Bottom