Maswali na ushauri kwa Malinzi

Maswali na ushauri kwa Malinzi

Tutaandaa lini mashindano haya
1.CHAN
2.Mataifa ya Africa(Africon)
3.Kombe la mataifa ya Africa kwa vijana
--------------------------------------------------------
1.Mataifa ya Africa kwa wanawake
-Wakubwa
-Vijana(wasichana)
Au tuombe kuandaa kombe la dunia la akina mama
 
Malinzi,

Rejea mjadala kuhusu timu ya Taifa, mawazo yangu ni kama ifuatavyo

1) kwanza ili kujua ni mfumo au utaratibu gani tuufuate katika kuijenga timu yetu ya taifa, mimi nakuomba kwa kuwa umemteua mtu mfulani kuwa msaidizi au mshauri wako wa mambo ya mpira, hivyo natumaini huyu mtu analipwa na TFF. sasa huyu mtu nakuomba umpe kazi afanye utafiti yakinifu wa nchi zote za Taifa za Africa, ambazo timu zao zimekuwa na mafanikio. Aaandike ripoti na kuiwakilisha kwako, na wewe kama itawezekana uishushe hapa, hii itatusaidia kutupa mwanga na kujua ni mfumo upi tunaweza kutumia. Pia hapa unawezaq kupata watu ambao wanaweza kufanya kazi na huyu jamaa kwa kupeana malengo, nani ashughulikie nchi hii, na mwingine hii.

Tujiulize nchi kama Rwanda, Burkina farso, na Uganda mbona zimeweza kuwa na timu nzuri katika muda mfupi? Hata Zimbambwe , tumeona juzi walivyoweza kufanya vizuri achilia mbali Libya pamoja na matatizo yote.

2) Idadi ya wachezaji wa kigeni.
Hili swala ni kweli limeathiri kwa kiasi kikubwa nchi kama UK, lakini kwa upande mwingine hakuna ukweli, tujiulize ni tangu lini wachezaji wa kigeni wameanza kufurika kwenye timu za England? Na je kabla ya hapo timu ya Taifa za UK , na hasa England zimekuwa na mafanikio? Jibu utakuta si kweli. Tatizo la UK, na England per se, mfumo wa ufundishaji kutoka academy ni dhaifu mno, hebu tazama tu vipaji ambavyo huzalishwa na academy ya Ajax amsterdam ulinganishe na wachezaji wa Engaland, wengi wao ni media tu ndo imekuwa ikiwakuza.

Tukija kwa hapa kwetu, wachezaji hawa wa kigeni wameongeza saana ushindani na kuifanya ligi yetu kuwa kivutio hata kwa jirani zetu. Kitu kinachoweza kufanywa ni kuwa timu iruhusiwe kusajiri si zaidi ya wacheza 5, lakini uwanjani isichezeshe zaidi ya wachezaji watatu kwa wakati mmoja.

Yombayomba umenipa wazo zuri sana kufanya a comprehensive research ya programme za wenzetu.Hapa ningependa kuongeza ghana,senegal,ethiopia ,cape verde nanigeria,itatusaidia kwa mipango yetu ijayo.Nalifanyia kazi immediately.
La wachezaji wa nje ninaomba huu mjadala uendelee ili msimu 2014/2015 ndio tufanye mabadiliko ,kama ikibidi,baada ya utafiti wa kina.
 
Last edited by a moderator:
MKUU MALINZI

VIPI KUHUSU ITC YA GEORGE MTEMAHANJI tangu mwaka jana mpaka leo kimya ameshindwa kujiunga na timu na kuanza kucheza mpira ITALY na USWISSI, Vipi mkuu au ndio mpaka ailipie hapo TFF ndio atapewa ITC

kwamekwax naomba details zozote kuhusu hii ITC ili nifuatilie,nitumie kwa email jamalmalinzi@yahoo.com
 
Last edited by a moderator:
Jamal Malinzi

kwahili twende taratibu,
tuongeze zifike 16 then 18 then 20. na sio haraka haraka.

pia isije ikawa mambo ya kuwa mwaka huu hakuna kushuka daraja, hatutaki kusikia hili ni bora kuboresha ligi daraja la kwanza na kuhakikisha badala ya kupanda watu wawili wapande wanne lakini kushuka wawili kila mwaka ni lazima.
Ni kweli,ukipanua ligi ghafla ubora wa ligi kwa maana ya ushindani nao utashuka ghafla,ni jambo la kwenda kwa hatua.
 
Last edited by a moderator:
Tutaandaa lini mashindano haya
1.CHAN
2.Mataifa ya Africa(Africon)
3.Kombe la mataifa ya Africa kwa vijana
--------------------------------------------------------
1.Mataifa ya Africa kwa wanawake
-Wakubwa
-Vijana(wasichana)
Au tuombe kuandaa kombe la dunia la akina mama
Tumeamua kuanza na fainali za afrika wavulana umri chini ya miaka 17 mwaka 2019,hii itatupa uzoefu wa kuandaa mashindano makubwa zaidi.Rwanda nao walianza na under 17 sasa 2016 wananda CHAN
 
Mkuu malizni habari Ok asante kwa majibu yakoAnyway nimempa kijana GEORGE MTEMAHANJI namba yako pamoja na e mail yako so nazani atawasiliana na wewe katika wiki chache zijazo, He has a lot of things to talk with you please Mpe support na positive response mr presidentOtherwise Nakutakia kazi njema
kwamekwax naomba details zozote kuhusu hii ITC ili nifuatilie,nitumie kwa email jamalmalinzi@yahoo.com
 
Malinzi,

Nilikuwa naomba kuchangia kuhusu mambo haya:

1) Mmiliki mmoja kuwa na zaidi ya timu moja kwenye ligi yetu
Rejea kicha hiki, nadhani wengi tumejikita kwa kutazama wenzetu wa Ulaya kupitia UEFA, ambapo mmiliki mmoja haruhusiwi kumiliki zaidi ya timu moja kwenye ligi. Sabu kubwa ni kuwa biashara ya mpira kubwa saana sasa hivi na nia ni kutaka kuzuia mtu mmoja kuwa na monopoly katika biashara, kwa mfano mapata kutokana na biashara ya soka katika Italy ilikuwa ni namba 3 katika kuliingizia pato la taifa, hata kwa England sitashangaa kwa sasa kuwa katika nafasi hiyo.

Sasa ukija hapa kwetu nyumbani, tulikuwa na timu za kiraia zikimilikiwa na wananchi kama ilivyo kwa Yanga na Simba, hizi timu zilikuwa kama Balimi(Kagera), Toto (Mwanza), Lake Tanganyika(Kigoma), Sugura (Tabora), Nyota Afrika na Mseto (Morogoro) na nyingine nyingi tu.

Wachezaji wa timu hizi walikuwa wakicheza bila kuajiriwa na vilabu, yaani kipato ni kile utapewa mapato yakipatikana ya mlangoni, na walikuwa waajiriwa wa mashirika mbali mbali, sasa baada ya muda mashirika yakaanzisha timu zao, na kuwalazimisha wachezaji wachezee timu zao. Hapo ndo timu zikafa, kwani hazikuwa na uwezo, hapo utaona Pamba ya Mwanza ikaiua Toto, Tumbaku Tabora ikaiua Sungura, the same Tumbaku Morogoro ikaziua hizi Mseto na Nyota.

Leo hii tumeshuhudia haya mashirika yanaendeswha kibiashara zaidi, yamekuta hayana uwezo wa kuhudumia timu, hivyo yakazifunja hizi timu.

hivyo tunapaswa kuishukuru serikali kwa kuruhusu timu za majeshi yetu, kumiliki timu, na pia kutoa ajira kwa wachezaji ambao ni raia.

nadhani wote mtakuwa mmeona utaratibu wa mwenyekiti wa Yanga wa kutoa mapato na matumizi ya timu. Utaona kabisa ni jinsi gani kwa sasa ni vigumu kuendesha timu, pamoja na Yanga kuwa na wapenzi wengi na ambao wanajaa inapocheza.

Leo hii ukiwambia Azam FC, watoe mahesabu yao, I mean hesabu za uendeshaji timu, utashangaa kuwa inaendeshwa kwa hasara kubwa. Tumeshuhudia baada ya mzunguuko wa kwanza, Mbeya City, ilikuwa ya tatu kwa kuingiza pesa nyingi za mlangoni kuliko Azam.

Na pia nguvu ya wapenzi wa Yanga tumeiona kwenye promotion ya Mtani wa Jembe, ni kiasi gani walipata na Simba kiasi gani. Natumaini hilo viongozi wa Yanga watalitumia katika mazungumzo kuboresha ufadhili kutoka kampuni ya bia, na hata kutafuta wafadhili wengine.

kwa kuhitimisha mimi nadhani, hizi timu za majeshi ni muhimu saana na wala hili lisiwe swala la kuumiza kichwa.

2) Uwezo wa waamuzi katika mechi za watani,
Umeongelea kuwa deby ya Yanga na Simba, ni moja ya deby 6 kubwa katika bara la Afrika. Hili nalikubali kabisa, miaka mingi tumeshuhudia uamuzi wa ajabu kabisa katika mechi hizi. Sasa kwa kuwa hizi mechi zinaingiza pesa nyingi saana na hata kuwa na makato ya ajabu saana. Hivi kwa nini tusitumie mechi hizi kutangaza utalii wetu?

Hapa naamanisha kwenye mechi hizi tulete waamuzi kutoka nje, na baada ya mechi tuwape fursa kwenda kutembelea mbuga zetu, nina uhakika kwa mipango mizuri, TTB, TANAPA na wafadhili wa Yanga na Simba (kampuni ya Bia) wanaweza kuligharamia hili.

Tutanyenyua mpira wetu, na tutautangaza nje, mimi ningependekeza marefa kutoka Scandinavia, hawa hawana makuu saana. Mashirikisho ya mpira ya nchi hizi nina uhakika yatafurahi kutusaidia.
 
Yombayomba umejenga hoja nzurisana kuhusu umuhimu wa timu za majeshi kwa mustakabali wa mpira wetu.FIFA club licencing regulations na tuliambiwa lazima iwe kwenye katiba zetu na tulifanya hivyo.Hii kanuni kama ulivyosema inapiga marufuku umiliki wa timu zaidi ya moja kwa mmiliki mmoja.Jambo hili mimi naona ni la kisheria,vyema kamati yetu ya sheria kwa kushirikiana na wadau wengine ikaliangalia kwa kina.
Wazo la kuleta marefa wa nje yanga vs simba ni la siku nyingi,ngoja tuzidi kulifanyia kazi.Lakini je lazima wawe wazungu?
 
Last edited by a moderator:
Tumeamua kuanza na fainali za afrika wavulana umri chini ya miaka 17 mwaka 2019,hii itatupa uzoefu wa kuandaa mashindano makubwa zaidi.Rwanda nao walianza na under 17 sasa 2016 wananda CHAN

Ahsante kwa majibu
 
Nakushaur

lig ya TZ iendeshwe kwa mfumo wa EPL

mashabiki wathbitiwe kuisapot tm ya nyumban
 
Mkuu Habari

Mkuu malizni nimeona tff imetoa kamati na majina ya wajumbe ok ni sawa

Il mbona naona kamati za tff zimekuwa nyingi na wajumbe wa hizo kamati wengi . hii uoni kama inakuwa mzigo mkubwa kwa tff hasa kwenye malipo ya wajumbe kwenye vikao na shughuli zingine uoni umuhimu wa kupunguza kamati au na idadi ya wajumbe kwenye kila kamati
 
JM kwanini Azam hawaruhusiwi kutumia uwanja Wa chamaz wanapocheza na simba na yanga?hii c saw a kabisa..
 
Yombayomba umejenga hoja nzurisana kuhusu umuhimu wa timu za majeshi kwa mustakabali wa mpira wetu.FIFA club licencing regulations na tuliambiwa lazima iwe kwenye katiba zetu na tulifanya hivyo.Hii kanuni kama ulivyosema inapiga marufuku umiliki wa timu zaidi ya moja kwa mmiliki mmoja.Jambo hili mimi naona ni la kisheria,vyema kamati yetu ya sheria kwa kushirikiana na wadau wengine ikaliangalia kwa kina.
Wazo la kuleta marefa wa nje yanga vs simba ni la siku nyingi,ngoja tuzidi kulifanyia kazi.Lakini je lazima wawe wazungu?

Sababu ya kupendekeza wa Scandinavia, ni kuwa kuna uwezekano mkubwa gharama zikawa ndogo, na hata vyama vya huko kutupa msaada kwa kufidia gharama ili kutusaidia kunyenyua mpira wetu. Pili wafadhili nilio pendekeza wanaweza kuwa tayari, kwani kuja kwa hao waamuzi tukiwa na wabunifu wazuri wa matangazo ya biashara , tunaweza kutumia kutangaza utalii, na vipaji vya vijana wetu.

Think loud Mr President
 
by Jamal Malinzi:
Dark City hakuna haja ya kuhangaika na jambo ambalo halina tija.Mambo ya msingi ya kujadili ni vipi tucheze Afcon Morocco mwakani,ni vipi tunaanda timu zetu za vijana na za wanawake,TFF ipate wapi vyanzo mbadala vya mapato ili yatumike kwenye miradi ya youth,tunazibaje mianya ya wizi wa mapato,tunajengaje mahusiano na vyama vya nchi zilizoendelea,ni mtaala upi utumike kufundisha mpira Tanzania,Academies zetu tunaziongezeaje uwezo wa kukuza na kulea vipaji na kadhalika.Tuachane na mambo ya personality tuhangaike na issues.Anayengang'ania ukabila kwa vyovyote vile ana lake jambo,tusimpuuze,tufuatilie tujue hidden behind kuna ajenda gani.

Unasema hilo swala halina tija? Alafu umejaza wahaya kwenye idara muhimu zote!

Unaboa#@
 
Jamal,
Ulipokwenda kumtembelea Lowassa yalizuka maswali mengi sana. Hata EZEKIEL KAMWAGA wa Raia Mwema aliandika kirefu kuhusu hili. Unaweza Kutufafanulia dhumuni la ziara ile hasa kwa kipindi hiki chenye harakati nyingi za Lowassa? Samahani kama swali hili limeshaulizwa hapa.

unnamed+(5).jpg



 
JM kwanini Azam hawaruhusiwi kutumia uwanja Wa chamaz wanapocheza na simba na yanga?hii c saw a kabisa..

Hofu ni usalama wa watazamaji kutokana na wingi wa watu maana capacity ya Azam complex haizidi watu elfu kumi. hata mchezo wa Azam vs Mbeya city uwanja ulifurika sana mpaka tukahofia usalama.Kimsingi TFF tumefurahia sana uwanja wa Azam complex kupewa hadhi ya CAF.
 
Mkuu Habari

Mkuu malizni nimeona tff imetoa kamati na majina ya wajumbe ok ni sawa

Il mbona naona kamati za tff zimekuwa nyingi na wajumbe wa hizo kamati wengi . hii uoni kama inakuwa mzigo mkubwa kwa tff hasa kwenye malipo ya wajumbe kwenye vikao na shughuli zingine uoni umuhimu wa kupunguza kamati au na idadi ya wajumbe kwenye kila kamati
Uundwaji wa kamati kumi na saba za TFF ni kwa mujibu na agizo la katiba ya TFF.
Wenye mamlaka ya kubadili utaratibu huu ni mkutano mkuu wa TFF.
 
Malinzi, umewasogeza watu wengi wanao jiita wadau wa mpira (wachezaji na viongozi wa zamani ) unadhani kwa upeo wao (wengi wao) wataweza kuendana na kasi ya maendeleo ya soccer kwa ngazi ya east africa, africa na dunia kwa ujumla? Pili. Hali ya kuwajaza kwenye mamlaka huoni kama unakaribisha majungu yasio na msingi? Najua unajua aina ya watu ulio wasogeza karibu yao...
 
Back
Top Bottom