Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Uhuru Kenyatta: Maafisa watakaohusishwa na ufisadi watatimuliwa serikalini
Unapotajwa katika kesi ya ufisadi na kupelekwa mahakamani utalazimika kuondoka serikalini , amesema rais Uhuru Kenyatta.
''Nitachukua hatua ya kumuondoa afisa yeyote wa serikali atakayekuwa na kesi ya kujibu mbela ya mahakama'', aliongezea.
Akizungumza wakati wa hotuba kwa taifa siku ya Alhamisi Uhuru amesema kuwa amekuwa katika shinikizo ya kuwafuta maafisa wa serikali.
Hakutakuwa na afisa atakeysazwa katika vita dhidi ya ufisadi .
Hatahivyo amesema kuwa serikali itafuata njia za kisheria katika kuwashtaki wahusika.
Ufisadi serikalini
Amesema kuwa vita dhidi ya Ufisadi havitafanywa kupitia pingamizi na taarifa za vyombo vya habari.
"Vitendo vyetu havitakuwa vya shutuma...demokrasia yetu inafuata sheria hivyobasi mchakato wa kuwachukulia hatua wanaofanya makosa ni muhimu katika kutekeleza wajibu huo''.
Mapema Uhuru Kenyatta alifutilia mbali uteuzi wa jaji Joseph Mutava. Hii ni baada ya mahakama ya juu kupendekeza kuondolewa kwake kutokana na uovu aliotenda.
Aidha Amesema kuwa watu matajiri kupitia kiasi ambao maisha yao haiendani na kodi wanayolipa watalazimishwa kusema ni wapi walikotoa fedha ama mali hiyo, alisema katika machapisho yake katika mtandao wa Twitter.
''Haturudi nyuma katika mapambano dhidi ya ufisadi kwasababu tumejitolea kuhakikisha vizazi vijavyo vinarithi Kenya iliyo imara inayoheshimu utawala wa sheria.
Alisema kuwafunga jela au kuwatoza faini watu waliyoba mali ya umma haitoshi, lazima warudishe mali hiyo.
''Suala la uadilifu linatarajiwa kuwa jambo la kawaida siku za usoni'' alisema Bw. Kenyatta.
Sent using Jamii Forums mobile app
BBC
Unapotajwa katika kesi ya ufisadi na kupelekwa mahakamani utalazimika kuondoka serikalini , amesema rais Uhuru Kenyatta.
''Nitachukua hatua ya kumuondoa afisa yeyote wa serikali atakayekuwa na kesi ya kujibu mbela ya mahakama'', aliongezea.
Akizungumza wakati wa hotuba kwa taifa siku ya Alhamisi Uhuru amesema kuwa amekuwa katika shinikizo ya kuwafuta maafisa wa serikali.
Hakutakuwa na afisa atakeysazwa katika vita dhidi ya ufisadi .
Hatahivyo amesema kuwa serikali itafuata njia za kisheria katika kuwashtaki wahusika.
Ufisadi serikalini
Amesema kuwa vita dhidi ya Ufisadi havitafanywa kupitia pingamizi na taarifa za vyombo vya habari.
"Vitendo vyetu havitakuwa vya shutuma...demokrasia yetu inafuata sheria hivyobasi mchakato wa kuwachukulia hatua wanaofanya makosa ni muhimu katika kutekeleza wajibu huo''.
Mapema Uhuru Kenyatta alifutilia mbali uteuzi wa jaji Joseph Mutava. Hii ni baada ya mahakama ya juu kupendekeza kuondolewa kwake kutokana na uovu aliotenda.
Aidha Amesema kuwa watu matajiri kupitia kiasi ambao maisha yao haiendani na kodi wanayolipa watalazimishwa kusema ni wapi walikotoa fedha ama mali hiyo, alisema katika machapisho yake katika mtandao wa Twitter.
''Haturudi nyuma katika mapambano dhidi ya ufisadi kwasababu tumejitolea kuhakikisha vizazi vijavyo vinarithi Kenya iliyo imara inayoheshimu utawala wa sheria.
Alisema kuwafunga jela au kuwatoza faini watu waliyoba mali ya umma haitoshi, lazima warudishe mali hiyo.
''Suala la uadilifu linatarajiwa kuwa jambo la kawaida siku za usoni'' alisema Bw. Kenyatta.
Sent using Jamii Forums mobile app
BBC