Matakwa ya Spika Ndugai kuhusu Kamati za Bunge kufuatilia mchakato wa ajira za walimu. Je, Serikali inafanya udanganyifu?

Baada ya mama kusema bunge lijadili mambo yenye yenye tija kwa taifa, Ndugai kachukia, saa hii anajifanya anaibana serikali! Kwa taarifa yake bunge hili kibogoyo halina nguvu hiyo.
Ndugai na nyi Chadema wote si watoto wa baba mmoja?
Hivi bado mnataka bandari ya bagamoyo?
 
Huyu spika haaminiki, ameshindwa hata kulinda katiba ya nchi...
 

Pale Shetani anapogeuka Malaika.
Ndugai ni nafiki sana.

Hili tatizo limeanza siku nyingi sana, likachochewa zaidi awamu ya Mwendazake Kwa upendeleo wa waziwazi Kwa Kanda ya Ziwa, yeye Kwa nafasi aliyonayo hakupaswa kulalamika Bali kuchukua hatua ya kuitaka Serikali kuondokana na huu Urasimu.

Kama yeye anaona ni sahihi kulalamika pekee basi hafai kuwa Spika.
 
Baada ya mama kusema bunge lijadili mambo yenye yenye tija kwa taifa, Ndugai kachukia, saa hii anajifanya anaibana serikali! Kwa taarifa yake bunge hili kibogoyo halina nguvu hiyo.
Hata wananchi hawafuatilii kama vile siyo kipindi cha budget
 
Huyu mama na mwendezake bado ni kitu kimoja. Ubaguzi ni uleule. Kaangalie teuzi za wakuu wa mikoa, hakuna hata raia moja ametokea kanda ya kaskazini yaani Manyara, Arusha, Kilimanjaro wala Tanga. Ina maana hakuna wenye uwezo kutoka pande hizi wakati mpaka Kafulila ni mkuu wa Mkoa? Alisababisha matatizo ya ajira has ya walimu ni Magufuli, majanga haya yote ya watoto wasomi wa kitanzania kudhalilika laana iwaendee uzao wake wote. Huyu mama km ana nia ya kuwasaidia walimu serikali ipange mpango maalum wa kuajiri kwa mwaka angalau mara mbili na ianze na alikoishia JK, yaani mwaka 2015. Ajira isiwe ya kuomba majina yachukuliwe vyuoni kuondoa uonevu, ubaguzi na rushwa.
 
So, unataka kusema hapa tulipo fikia ni dhaili kanda ya ziwa wanapendelewa?

Lakini tambua RC na DC haina qualification kuwa kiwango fulani ndio anaitajika bali anateuliwa kutokana na matakwa ya Rais.

Na hili la Ajira sidhani kama kuna ukweli, je hao wakanda ya ziwa sio qualified? Au wamebebwa tu?
 
Mhe. Spika ameona kitu ndani ya mfumo wa serikali hakipo sawa nacho ni taratibu za ajira ktk utumishi wa umma na Uteuzi ktk nafasi mbalimbali, mamlaka zinazo husiana na uteuzi hazizingatii mseto unao akisi taswira ya Taifa letu, tuache unafiki, kuna tatizo na hivyo linapaswa lirekebishwe haraka ili kujenga na kuimarisha umoja na mshikamano wa Taifa letu.
 
Unafiki tu, alikuwa wapi kumwambia mwendazake? Tumeshawajua rangi zao hawa wanasiasa uchwara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…