Matani

Matani

Mwembamba mpaka ukisimama kituo cha daladala na abiria wenzio konda anasema hatupakii miwa
 
Kwenu mezaliwa wengi mpaka baba yenu akirudi kazina anawasalimia habar zenu wananchi
 
Jamani nilipokuwa mdogo hii ndo ilikuwa hobby yangu maana kwa umbo langu dogo sikuweza kupigana ila ukinikosea kidogo..nitakupa neno utakaa kimya mwenyewe!
Najikumbushia tu...(usinichukie...)

Unataka matani..

Nyani Ngabu
, una bichwa kubwa mpaka shuleni ulikuwa unaitwa Headboy! twende twende..
Fidel80, wewe umekonda mpaka ukisimama kwenye ukuta unakaa kama crack...
Mzee Mwanakijiji demu wako amekonda mpaka akivaa t-shirt ya bluu anafanana na sim card ya tiGO..

Asprin
unamashavu kama mimba ya panya..

Na wewe TUKUTUKU uso kama shamba la matuta...

Unataka unataka..

Mwangalie kwanza, wewe Bigirita yaani wewe ni mbaya mpaka hutumia lotion inayoitwa 'why bother!'..teh teh..

Zak wewe ni mweusi mpaka ukirushiwa jiwe linarudi kuomba tochi...
watu8 wewe ni mshamba hadi mara ya kwanza kupanda daladala ulianza kutandika vitambaa kwenye siti.


PS: On a light touch...
Unashangaa nini!!! kashangae mikumi chui wanavaa bahama bahama
 
Last edited by a moderator:
kwenu mko wengi mpaka dingi yenu akiingia ndani anasalimia wananchi hamjambo
 
Mweusi mpaka ukibeba mtoto analala akidhani usiku umeingia
 
wewe uliyefufua uzi huu nasikia kwenu pananuka hadi magari yanayobeba taka yanaogopa kupita mitaa yenu.
 
Unashangaa nini!!! kashangae mikumi chui wanavaa bahama bahama

Ndo maana chupi yako uliivaa mda mrefu bila kufua siku ulipoivua ikaanguka chini ikapasuka!

kwenu mko wengi mpaka dingi yenu akiingia ndani anasalimia wananchi hamjambo

Mbwa wenu ni wavivu hata wakija wezi wao huwatemea mate badala ya kubweka!

Mweusi mpaka ukibeba mtoto analala akidhani usiku umeingia

Nasiki simu yako ni kubwa badala ya kuwa na pin mumber yenyewe ina msumari number.

demu mwenyewe ------ yamenyauka kama kitabu cha ushuru!

Ndo maana una kipara hadi ukivaa yale masweta ya 'polo neck' unakuwa kama 'roll on'

Mentor una mindevu imekaa vibaya ka ufagio wa kutolea tandabui

Wewe ni mzee kiasi kwamba wakati unazaliwa OLD TESTAMENT ilikuwa inaitwa TESTAMENT
 
wewe uliyefufua uzi huu nasikia kwenu pananuka hadi magari yanayobeba taka yanaogopa kupita mitaa yenu.

Umenikumbusha....TV yenu ni nzee mpaka kwenu mkij.amba watangazaji wa habari wanafunika pua!!!!
 
Umenikumbusha....TV yenu ni nzee mpaka kwenu mkij.amba watangazaji wa habari wanafunika pua!!!!

Hivi wewe si ndo ulitoa ushuzi pale mahakama ya kisutu wakati wa kusikiliza kesi ya ditopile kesi ikahamia kwako kwakusababisha mauaji ya watu watatu waliokufa kwa harufu mbaya ya uvundo? Kesi yako iliishia wapi?
 
Back
Top Bottom