Matarajio. . . . .

Utegemezi ni mbaya kuliko haya dearest, wenyewe unaweza ukampelea mtu kufanya mambo ambayo hapendi wala hakuwahi kufikiria, kubaki kwenye mahusiano/mtu asiemtendea haki ili tu asipoteze hicho anachotegemea (fedha, hisia, fikra n.k)

ndo maana nikasema tunahitaji kutokuwa na utegemezi kuanzia kwenye akili zetu...manake kama ukikuta kile ulichotarajia hakipo,then kama unajiamini na una utulivu wa kifikikra nawe utafanya kila kilicho halali na kinachokubalika mbele ya mwenzi wako na Mungu ili uweze kuyafanya maisha bora....lakini ukiona huwezi ndo maana hata wengine wanaishia kujiuza na vitu vingine vibaya..
 
mie bwana naona women shuls just have the simple expectations kama zamani...get married, have kids, kupika, kudeki na kumridhisha mwanaume....hizi kero zingine zisingekuwepo kabisa
 

Hahahaha. . . Boss unataka watumie bongo zaidi wakati wenyewe wanasema "love is blind" and that blindness is caused by emotions? Impossible.
 
Nimekusoma dearest. . .
Ila unajua kwamba kuna watu sio tegemezi ila wanaishi wakiamini wao wanatakiwa kupewa/pokea tu na sio kutoa? Mtu kama huyu hawezi kusimama aseme ngoja sasa nimsaidie mwenzangu tuondokane na matatizo tuliyonayo. Wao wanataka kupokea tu iwe kifedha, kihisia bila kutoa.
 
Hiyo siyo maana yake!!!!

Naomba unieleweshe. . .
Na usisahau kwamba "kufanya usaili" nimetumia kama kiwakilishi cha umsome/umwelewe/umdadisi ili kujua yeye ni kile unachotaka au la na sio umshikie karatasi iliyojaa maswali.
 
mie bwana naona women shuls just have the simple expectations kama zamani...get married, have kids, kupika, kudeki na kumridhisha mwanaume....hizi kero zingine zisingekuwepo kabisa
Kaaazi kweli kweli.
Alafu ikishakua hivyo expectation za mwanaune nazo zitaendana na mazingira au mwanamke tu ndio anaetakiwa kubadilika?
 
Kwahiyo mnabeba tu? Mnabahatisha kama mchezo wa kamari ehhhh? Mtakoma.

sasa ukipenda utachagua saa ngapi! Unless umewahi kupata majeraha out of love,so unaangalia next time,type ya spouse wako iwe vipi..
 
Naomba unieleweshe. . .
Na usisahau kwamba "kufanya usaili" nimetumia kama kiwakilishi cha umsome/umwelewe/umdadisi ili kujua yeye ni kile unachotaka au la na sio umshikie karatasi iliyojaa maswali.

Ushajielewesha mwenyewe.

Sasa unataka nini tena wee demu wa Nyani Abiziani?
 
sasa ukipenda utachagua saa ngapi! Unless umewahi kupata majeraha out of love,so unaangalia next time,type ya spouse wako iwe vipi..
Aisee. . .
Kwahiyo hata hamna kujulishana yale ambayo yanaweza yakawa magumu kukubalika kwa upande wa pili? Hongereni msio na kazi.
 

Ndo hivyo dearest....tumetofautiana mitazamo na matarajio....japo kuna wenzi wengine wanaharibu wenzao.....unamzoesha tu mpaka analemaa tu.
 
Aisee. . .
Kwahiyo hata hamna kujulishana yale ambayo yanaweza yakawa magumu kukubalika kwa upande wa pili? Hongereni msio na kazi.

siku hizi huenda inawezekana ukawa na qualities kicwani mwako za umtakaye.. Na unapoona propositions unaziattend zote kuangalia kama zina meet quality zako.. Zamani mtu anampenda mtu wala hachaguichagui.. Awe na kazi asiwe nayo,elimu ndogo au asiwe nayo kabisa,etc. Sijui unapata picha Lizzy..
 
Achan na hivyo vigezo ambavyo wengi wanakoroga, hapa naongelea kumfahamu. Ujue kama malengo yake na yako yataweza kufikiwa pamoja, ujue kama matarajio yake unaweza ukayafikia, ujue kama fikra zake zitawezana na zako, ujue kama tabia na mapungufu yake utaweza kuyavumilia. Penda ukiwa umefumba macho hapo kama hujarudi unalia.
 

Tuwe wakweli, ni asilimia ngapi ya wanawake wanakuwa na ndoa ku-replace bad feelings,revenge...wataka sema hatupendi?

Kuhusu kufanya maamuzi emotionally bado utakuwa unajichanganya, manake hisia ni kama vile huruma,upendo,huzuni,hasira etc....ukishasema wanawake wengi wana unrealistic expectation kama maisha bora, kutopanda daladala tena au matarajio mengine...hizo si emotions bali ni akili inavyomtuma atarajie....emotions ni kama kuolewa kwa hasira,huzuni au huruma ambayo wanawake wengi hawako hivyo tena,wanaangalia uhalisia wa maisha na partner ambaye pamoja wanaweza kumudu maisha.....!
 
Ndo hivyo dearest....tumetofautiana mitazamo na matarajio....japo kuna wenzi wengine wanaharibu wenzao.....unamzoesha tu mpaka analemaa tu.

Dearest wewe na akili zako/tabia yako ya kujitegemea/uelewa wako/ujanja wako kuna mtu anaweza akakulemaza? Kama jibu ni hapana basi wakulaumiwa ni anaelemaa na sio anaemrahisishia maisha.
 

okay hapo nimekuelewa.. Naomba niongezee tu kwamba... Kwa research yangu isiyokuwa na takwimu rasmi.. Mwanamke na mwanaume ambao waliachana na wenzi wao hasa waliokuwa wa kudumu,kisha wakakutana wao kwa wao.. Zoezi la kupima matarajio ya mwenza na namna ya kuyavumilia linakuwa jepesi sana,na mara nyigi, inakuwa happy couple..
 
Dearest wewe na akili zako/tabia yako ya kujitegemea/uelewa wako/ujanja wako kuna mtu anaweza akakulemaza? Kama jibu ni hapana basi wakulaumiwa ni anaelemaa na sio anaemrahisishia maisha.

Dearest, ninajitegemea tu vile inabidi na nachukia kuomba....ila kusema ukweli nikapata mtu tu wa kunipa mahitaji yangu na kunisomeshea vile vitoto vyangu, kazi kubwa itakuwa usafi,upishi na kwenda gym....sipendi shida kabisaa na kuchoka choka!!
 
Hhhhmm. . . inawezekana.
Kuna watu wasio na shukrani, hata wakipata mtu mzuri baada ya kunyanyasika sana bado wanakua viguu na njia , maneno kila saa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…