matatizo ya kifua

matatizo ya kifua

Ibra6

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2013
Posts
290
Reaction score
66
Habari,mwanangu ana umri wa miaka mitatu sasa lakini amekuwa akisumbuliwa nakifua kisichopona kwa muda mrefu.tatizo lilianza akiwa na mwaka mmoja na miez mitatu alipotumia dawa za minyoo.akaanza kukohoa na dawa nyingi keshatumia za hospitali na za mitishamba lakini zinatuliza tuu tatizo kwa muda mfupi halafu linarudi upya..vipimo kama xray,fbp,allergy,kimeo,vyoote kapima inaonekana hana tatizo ila hali bdo ileile akianza kukohoa mpaka ww uliemshika unalia..na pia hili tatizo huanza pale tuu anapoanza kunenepa.nimewaelezea madaktar wengi,hospitali mbalimbali nao wakimpima wanabaki kusema hii hali itaisha tu.sasa ni rahisi kusema kama tatizo halikugusi naombeni msaada mtoto anateseka sana jamani
 
Kuna inhaler huwa wanatoa hospitali kwa Watoto

Rudi kwa doctor mwambie ampime athma, kama hana athma basi apewe hiyo inhaler ya kupulizia mdomoni na pump yake. Hilo ni tatizo la kawaida kwa watoto just see the proper doctor
 
Itakua huyo mtoto anasumbuliwa na vumbi si lazima uwe unaiona lkn either vumbi au harufu flani hivi. Jaribu kufuata ushauri wa mdau hapo juu huenda ukasaidia. Pia twanga kitunguu saumu changanya na asali kisha mpe mtoto au asali na ndimu
 
Ndugu Ibra6 Pole kwa huyo Mwananao anaye umwa na maradhi ya kifuwa fuata ushauri wa hawa wenzangu ikishindikana mtoto wako hajapona hicho kifuwa chake jaribu kunitafuta mimi ninayo Dawa ya kutibu hicho kifuwa cha mwanao na akitumia ataweza kupona na utasahau hilo tatizo lake ukiweza nitafute kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom