Matatizo ya kuishi kwa ndugu, Kwanini hali iko hivi? Kitaalamu hutokana na nini hasa?

Matatizo ya kuishi kwa ndugu, Kwanini hali iko hivi? Kitaalamu hutokana na nini hasa?

Raphael Mtui

Member
Joined
Nov 26, 2024
Posts
78
Reaction score
204
Moja ya vitu sitasahau katika maisha yangu ni pamoja na kipindi nilichoishi kwa mtu ambaye ni almost ndugu yangu.

Ilikuwa miezi mitatu tu lakini nilihisi ni milenia tatu!

Na mwisho wa siku sikulipwa mishahara yote!

Nakumbuka nilivyokuwa nikilazimika kumwibia ili nisife njaa. Hiyo inaniuma sana. Wizi wenyewe ni kuiba vyakula, kupika kwa siri, au kuiba matunda ili nisije 'kukata moto'.

Haya yalitokea miaka zaidi ya ishirini iliyopita, lakini nikikumbuka huwa sio poa kabisa.

Ukisoma stori nyingi za wana JF walio-share na sisi stori za maisha yao, ni nadra kukosa vipande vya hadithi za mateso mhusika aliyopata akiwa anaishi kwa ndugu fulani.

Kuishi kwa bro mjini, kuishi kwa dada, kwa mjomba, baba mkubwa/mdogo, shangazi, nk.

Kundi ambalo nimeona likisulubika zaidi ni pamoja na mabinti wanaoishi kwa dada zao mjini.

Naam, dada wa kuzaliwa tumbo moja. Awe ameolewa au hajaolewa, ila unaishi kwake. Kumekuwa na hadithi za mateso sana.

Vijana waliofikia kwa ndugu mjini kusaka maisha, wengi wameteseka sana si kwa sababu ya ugumu wa maisha, bali kwa sababu za kimanyanyaso!

Nisitilie mkazo mjini tu, hata vijijini pia.

Kwa nini ipo hivi? Kwa nini watu wengi wameteswa na ndugu zao hasa waliotangulia mjini?

Kuna siri gani katika hizi familia? Wanaowatesa ndugu zao wanakuwa wanajua wanachokifanya?

Ni ile hali ya mashindano ya kuhakikisha ndugu yako 'hatoboi' awe mtumwa wako tu?

Kuna nini hasa cha kufundishana katika hizi familia zetu?

Karibu kwa mawazo yako, lakini ni vizuri uka-share stori yako kama uliwahi kusulibiwa na ndugu.

Nzuri zaidi, kama unajua uliwahi kumtendea visivyo ndugu yako uliyeishi naye, na sasa umegundua na inakuuma, share nasi hiyo toba yako hapa.
 
Nimeishi kwa ndugu Dar kwa baba zangu wadogo , nashukuru sana kwa vile ni watu wa dini wanaishi pamoja ...Mke wa uncle ni mbondei wa Muheza aisee Mungu ampe maisha marefu mpaka kesho namtumia zawadi .

Roho safi kabisa tabia yake ilipekelea watu wengi kwenda Muheza kuoa wadogo zake wawili , alikuwa makini sana .Mm nilikuwa najiongeza muda mwingine nanunua , vitu kama vile mchele, maharage hata sabuni kwa vile nilikuwa nasoma chuo miaka hiyo.

Sina complications zozote na ndgu mpaka kesho. Sisi wenyewe tumezoea kuishi pamoja nyumba moja.​
 
Kila mmoja ana lugha tofauti ya kuzungumza namna alivyo pata shida kwa ndugu aliye wahi kukaa kwake.

Zaidi sana mimi naona sababu kuu ni ubinafsi na kujipendelea, kupenda walio wako na wasio wako liwakute lolote.

Kwa jinsi hio kwa kadri miwezavyo watoto wangu wasiishi kwa ndugu , hata likizo, na nikiwa nasafari kuliko kulala kwa ndugu heri ni lale standi kama nyumba za wageni hamna kwenye huo mji.
 
Nimeishi au kufikia kwa ndugu upande wa baba yangu, niseme tuu ahsanteni sana kwa ukarimu wenu!

Najua hakuna aliye mkamilifu, mlikuwa na nilikuwa na makosa kama binadamu yeyote anavyokosea sina Cha kulaumu! Barikiweni
 
tunayo mengi ila tumeyaacha yapite itoshe kusema kuishi kwa ndugu ni utumwa masimango mateso hasa akiona hata umevaa raba mpya...jibu ni kwamba unamuibia sitamani kizazi changu kipitie uko
 
Nimekulia kwa ndugu,sina cha kusema zaidi ya kuwashukuru.
Ukiwa mchapa kazi na mtu mwenye tabia nzuri kwa ndugu utakaa vizuri japo nasikia kuna wanawake wana roho mbaya.
 
Hizi nyuzi ni nyingi sana humu,ziunganisheni.
Wengine hushindwa kukaa kwa ndugu zao kutokana na tabia zao mbaya hasa ndugu wa mume huona nipo kwa kaka yangu,nipo kwa baba yangu hiyo huwapelekea kuwa na viburi.
Kwa kuwa upo kwa kaka yako hutaki kusaidia kazi za nyumbani,hutaki kujigusa,una tabia chafu nani atakutaka sasa?
 
Hizi nyuzi ni nyingi sana humu,ziunganisheni.
Wengine hushindwa kukaa kwa ndugu zao kutokana na tabia zao mbaya hasa ndugu wa mume huona nipo kwa kaka yangu,nipo kwa baba yangu hiyo huwapelekea kuwa na viburi.
Kwa kuwa upo kwa kaka yako hutaki kusaidia kazi za nyumbani,hutaki kujigusa,una tabia chafu nani atakutaka sasa?
 
Sikupata shida kuishi kwa ndugu sababu nilikuwa nachapa kazi kama house boy. Nakumbuka nikiwa chuo bado niliweza kufua nguo za wenye nyumba, kushika fagio nk
Changamoto yangu kubwa ni baadhi yao kufanya kama waliwekeza. Ukidhibiti hilo unakuwa mbaya. Usimuweke mwanao kwa ndugu bila sababu za msingi.

Mimi kwangu ndugu akataa kwa malengo, kama kusoma, amepata ajira amekuja kuegesha. Sio kukaa tu
 
Kama bongo muvi na story za mama wa kambo.....wamezongwa zongwa mitume na manabii na hawalalamiki kwenye maandiko yao. Muwe na shukurani pia.
 
Moja ya vitu sitasahau katika maisha yangu ni pamoja na kipindi nilichoishi kwa mtu ambaye ni almost ndugu yangu.

Ilikuwa miezi mitatu tu lakini nilihisi ni milenia tatu!

Na mwisho wa siku sikulipwa mishahara yote!

Nakumbuka nilivyokuwa nikilazimika kumwibia ili nisife njaa. Hiyo inaniuma sana. Wizi wenyewe ni kuiba vyakula, kupika kwa siri, au kuiba matunda ili nisije 'kukata moto'.

Haya yalitokea miaka zaidi ya ishirini iliyopita, lakini nikikumbuka huwa sio poa kabisa.

Ukisoma stori nyingi za wana JF walio-share na sisi stori za maisha yao, ni nadra kukosa vipande vya hadithi za mateso mhusika aliyopata akiwa anaishi kwa ndugu fulani.

Kuishi kwa bro mjini, kuishi kwa dada, kwa mjomba, baba mkubwa/mdogo, shangazi, nk.

Kundi ambalo nimeona likisulubika zaidi ni pamoja na mabinti wanaoishi kwa dada zao mjini.

Naam, dada wa kuzaliwa tumbo moja. Awe ameolewa au hajaolewa, ila unaishi kwake. Kumekuwa na hadithi za mateso sana.

Vijana waliofikia kwa ndugu mjini kusaka maisha, wengi wameteseka sana si kwa sababu ya ugumu wa maisha, bali kwa sababu za kimanyanyaso!

Nisitilie mkazo mjini tu, hata vijijini pia.

Kwa nini ipo hivi? Kwa nini watu wengi wameteswa na ndugu zao hasa waliotangulia mjini?

Kuna siri gani katika hizi familia? Wanaowatesa ndugu zao wanakuwa wanajua wanachokifanya?

Ni ile hali ya mashindano ya kuhakikisha ndugu yako 'hatoboi' awe mtumwa wako tu?

Kuna nini hasa cha kufundishana katika hizi familia zetu?

Karibu kwa mawazo yako, lakini ni vizuri uka-share stori yako kama uliwahi kusulibiwa na ndugu.

Nzuri zaidi, kama unajua uliwahi kumtendea visivyo ndugu yako uliyeishi naye, na sasa umegundua na inakuuma, share nasi hiyo toba yako hapa.
Mi ningependa simulizi yako ndiyo iwe somo la kujifunza, maana shuhuda zitakazotolewa hapa zipo katika mfumo mmoja, tofauti ni mazingira pamoja na wahusika.

Sasa waje wataalamu wa saikolojia watusaidie kuliweka vizuri jambo hili, huwa inatokeaje umekubali kwa hiari kumpa hifadhi mtu ili kesho naye aweze kusimama kwa kujitegemea, kisha unaanza kumnyanyasa?

Ama umemwajiri beki tatu au H/boy unaanza kumtesa, why!

Huwa nikifika kwenye sherehe na kuona namna watu walivyokusanyika kwa furaha na bashasha nyusoni mwao, utadhani wameumbwa hivyo kwa ukarimu, lakini ukifika majumbani mwao ni mashetani halisi namna wanavyowatendea wategemezi wao.

Wataalamu waje watuambie, ni nini kisababishi cha hali hiyo kisaikolojia?
 
Tumebeba watoto wa ndugu mpaka wanafanikiwa ila haji kukukumbuka hata mia kuipata kwake mpaka utumie lugha zote.
Hapo ndio mnapokosea, tofautisha kusaidia na kuwekeza. Ndugu wengine wanakaba mpaka mtu anakata chain. Unakuta ndio kaanza maisha kapata kazi juzi tu,tayari anaanza kuzogwa na kupewa majukumu. Hapo ni kumtia umasikini
 
Back
Top Bottom