Matatizo ya kuishi kwa ndugu, Kwanini hali iko hivi? Kitaalamu hutokana na nini hasa?

Ukiishi kwa watu kwanza jua nafasi yako. Yani ukijua nafasi yako basi itakupunguzia matatizo na expectations
 

Kwa Sababu asilimia kubwa ya watu tumetoka kwenye familia zisizo na Upendo.

Upendo wa Baba na Mama huambukizwa kwa watoto.

Usione kila siku napiga kelele kuhusu mahusiano. Naelewa madhara yake kwenye sekta zingine
 
Japo sina la kumlipa ila Mungu ambariki mjomba wangu na mke wake. Waliishi na mimi vizuri na kunisapoti kwa kila hali.

Upande mwingine nimeishi na ndugu mwingine, ilikua changamoto sana ila yote kwa yote ndiyo mapito ya dunia.
 
Hii ndio point ya msingi ndugu anaweza kuwa mbaya ila hali itakuwa mbaya zaidi iwapo huyo mgeni mwenyewe hajielewi hasa tabia za uvivu, uchafu, ubinafsi na kutoa maneno kwa ndugu huyu na kuyapeleka kwa ndugu yule. Ila yote kwa yote hakuna mkamilifu ni muhimu kama binadamu kuwa na subra na kuvumiliana.
 
Ukiangalia watu wanaotesa ngugu zao utagundua wengi wana IQ na EQ low sana. Sababu hiyo ndio explanation pekee ya kukosa empathy, sympathy na ustaarabu. Na automatically wanakuwa na uwezo mdogo na ulimbukeni kimaisha. Au wametoka huko. Sababu kutesa ndugu tumbo moja ni kitendo kisicholeta maana ukifikiria.

Hii ina-explain kwanini watu waliolelewa kwenye familia stable economically wengi ni wastaarabu huku ni vice versa upande wa pili. Na hiyo hierarchy inaexpand kimiji na kitaifa. At least in modern times.
 
Ila hata umasikini wakati mwingine huchangia
 
Ukikaa Kwa Mjomba haupitii changamoto Kama ambavyo utakaa Kwa shangazi ndugu wa baba yako.

Hii Ina maanisha sisi wanaume huwa tunaelewa sana maisha zaidi ya wanawake Kwa kiwango fulani.

Binafsi nimekaa Kwa uncle kila kitu kilikuwa sawa isipokuwa mke wake tu alikuwa anaonesha kutopenda ndugu wakae sana kwake .

Ila ndo hivyo utafutaji Una mengi .

Kukaa na mjomba is great
Kukaa na Baba mdogo is great Ila mama mdogo na shangazi hatari
 
Kwa maisha kama ya dar mtakosana tu na watu.ukute mtu amepanga na kula kwake ni shida halafu anaenda kukaa mwaka mzima huchangii chochote hata kusema ununue sabuni hamna na ni mtu mkubwa kabisa.Ili kuiepusha kugombana na kuchukiana unatakiwa usikae muda mrefu sana Kwa ndugu kama hakuna sababu za msingi
 
PUMBAVU/SHENZI... Ndomana TRUMPH anayafukuza, badala ya kutafuta maisha yao yanataka kuhemea/kufugwa kama Mbwa...
 
Hapo ndio mnapokosea, tofautisha kusaidia na kuwekeza. Ndugu wengine wanakaba mpaka mtu anakata chain. Unakuta ndio kaanza maisha kapata kazi juzi tu,tayari anaanza kuzogwa na kupewa majukumu. Hapo ni kumtia umasikini
Tulia huko
Wameshatusua
 
Tulia huko
Wameshatusua
Bila shaka ulisaidia, hukuwekeza kama mradi na sasa unataka kuvuna. Kama ndiyo, basi usione kama una haki ya kusaidiwa. Ana mke, watoto na wazazi ambao ni haki yao. Wengine ibaki kuwa utashi wake tu
 
Mkienda kwa watu mjitahidi kusaidia kazi sasa mgeni unakuwa huna tofauti na nyau, unataka ulale tu na kuangalia tv huku ukisubiri chakula kipikwe na hapo unakaa week mbili, Bado siku ya kuondoka hata kufua mashuka uliyolalia hutaki, hapo lazima ndugu wakuchoke
 
Ukiishi kwa ndugu jitahidi uact kama house boy/house girl, kazi yoyote unayoiona mbele yako ifanye, usitegee.

Ingawa pia unaweza kufanya yote hayo lakini bado usipewe thamani kubwa kama wazaliwa wa hapo.

Niliwahi kuishi kwa ndugu si zaidi ya mmoja, house gal akiamka naamka naye ingawa alikuwa hapendi kuniamsha lakini hofu yangu ilikuwa nikikutwa na mama mwenye nyumba nimelala itakuwaje?

Nilikuwa nikipatiwa nguo za baba mwenye nyumba kuzipiga pasi hata kama mtoto wa kiume yupo (Kwa madai najua kupiga pasi nguo) nilikuwa napiga pasi fresh tu bila manung’uniko.

Walikuwa ni msaada mkubwa kwangu, ninaamini bila wao nisingefika hapa nilipo. Walinifundisha kujitegemea na kufanya majukumu yangu pasipo kunung’unika mbona fulani hafanyi.

Mwenyezi Mungu awabariki sana na kuwapa maisha marefu Kwani hata sasa ninaweza kusimama mwenyewe na kupambana na yaliyo mbele yangu pasipo utegemezi.
 

Asante kwa balance nzuri.
 
Hakuna anayefanya kusaidia kazi kwa uaminifu na bado akakumbana na manyanyaso?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…