SI KWELI Mate hubeba VVU hivyo kubusiana kunaweza kuwa chanzo cha maambukizi

SI KWELI Mate hubeba VVU hivyo kubusiana kunaweza kuwa chanzo cha maambukizi

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Mdau mmoja wa Jamiiforums ameonesha wasiwasi wake baada ya kwenda hospitalini kupima VVU ambapo tofauti na namna alivyotarajia, daktari wake alimpima kwa kutumia mate yaliyotolewa kwenye fizi ya juu na chini.

B45B01F2-0095-41C5-99CA-383DB6325280.jpeg

Jambo hili limemfanya atoe ushauri kwa watu kuwa makini wanapokuwa wanabusiana kwa kuwa tendo hilo linaweza kusababisha maambukizi ya VVU kupitia mate.

Ukweli wa jambo hili upoje?
 
Tunachokijua
Ni kweli kuwa maambukizi ya VVU yanaweza kupimwa kwa kutumia majimaji yanayopatikana kwenye sehemu ya ndani ya kinywa cha mtu ambayo mara nyingi huchukuliwa kwenye fizi.

Kipimo hiki cha haraka kinachotoa majibu baada ya dakika 20 hufanya kazi kwa kutambua uwepo wa kinga mwili (Antibodies) anazozalisha mtu baada ya kupatwa na maambukizi ya VVU. Hata hivyo, ni muhimu kuweka sawa kuwa kipimo hiki hutumia majimaji ya kinywa ambayo hupatikana baada ya kusugua sehemu ya fizi na siyo mate halisi kama hoja ya mtoa mada ilivyo.

Je, mate yanaweza kubeba VVU?
Mate huwa na vimeng’enya vyenye uwezo wa kuharibu virusi kabla havijasambazwa na kuanza kushambulia, hivyo hayawezi kusababisha maambukizi ya ugonjwa huu.

Kwa upande mwingine, damu pamoja na mazao yake yanaweza kusambaza VVU. Ikitokea mtu mwenye virusi hivi akawa na damu kinywani inayotokana na uwepo wa michubuko au vidonda, kisha akabusiana na mtu mwingine mwenye michubuko au vidonda kinywani, mtu huyo anaweza kuambukizwa VVU.

Kwa ujumla wake, kuhusu maambukizi ya VVU kwa njia ya kubusiana, tafiti za kisayansi zinathibitisha mambo yafuatayo-
  • VVU haiwezi kuambukizwa kupitia mate.
  • Kubusiana siyo tendo baya, haliwezi kusababisha maambukizi ya VVU ikiwa wahusika hawatakuwa na vidonda au michubuko kinywani.
  • Ikiwa mtu aliyeambukizwa VVU atabusiana na mtu asiye na ugonjwa huku wote wawili wakiwa na michubuko au vidonda, ugonjwa huu unaweza kuambukizwa. Hata hivyo, chanzo kitakuwa ni damu iliyovilia kwenye mate kutoka kwenye vidonda na michubuko na siyo mate yenyewe.
Kushiriki tendo la ndoa, kupokea damu na masalia yake, uchangiaji wa vifaa vyenye ncha kali pamoja na maambukizi ya mama kwa mtoto wakati wa ujauzito na (au) wakati wa kujifungua ni baadhi ya njia zilizothibitishwa kuwa na uwezekano usiotia shaka katika kusababisha maambukizi ya VVU.
Umeeleweka lakini kila siku tunapiga miswaki, kuna michubuko mingine haionekani kwa macho...nadhani ukubwa wa kirusi ni mdogo sana.

But asante kwa analysis nzuri
 
Vijana wanakula bata ndiyo maana wanakufa sana kama nzi kwenye glass ya bia - Fiq Q

Starehe mnazipenda ila mwisho wake mbaya wengi wameteketea kwa kuendekeza umalaya - Prof Jay.
 
Back
Top Bottom