Mathias Mnyampala: Nguli wa fasihi aliyeanza shule ya msingi akiwa na mke tayari

Mathias Mnyampala: Nguli wa fasihi aliyeanza shule ya msingi akiwa na mke tayari

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Ni ngumu kuzungumzia fasihi ya kiswahili bila kumzungumzia Mathias E. Mnyampala. Mnyampala alizaliwa mwaka 1917 huko Dodoma akiwa ni Mgogo. Baba yake alikuwa ni mfua chuma na alimiliki ng'ombe wengi ambao Mathias ndiye alikuwa mchungaji. Mwaka 1931. Akiwa kama na miaka 14-15 aliozwa mke!

Baadaye shule ilianzishwa kijijini kwao. Naye akaomba kuandikishwa. Waalimu wakamwambia wewe tayari una mke, hatuwezi kukupokea. Lakini hakukata tamaa. Kila darasa(la chini ya mwembe) lilipoendeshwa naye alihudhuria. Siku moja mwalimu alijaribu wanafunzi wake kusoma habari fulani, wengi walibabaika. Akamwambia na Mathias naye asome maana amekuwa akihudhuria kila siku. Mathias akasoma vizuri sana, basi mwalimu akaamua kumuingiza rasmi.

Baadaye akaenda shule ya misheni kujifunza elimu na dini. Alienda na mkewe. Ilipotakiwa kuendelea mbele akachaguliwa, lakini alishindwa kwenda sababu mke wake alikataa kubaki akiishi misheni.

Basi hapo akaendelea kujitafutia elimu yeye mwenyewe huku akifanya 'tempo' za kufundisha. Akaanza na kujifunza kiingereza huku akilipa watu wamfundishe.

Elimu hii ilimuwezesha kufanya kazi nyingi sana. Lakini mara nyingi alipata changamoto maana hakuwa na vyeti vyovyote vilivyomuonyesha kuwa kasoma. Lakini kazi yake nzuri ilikuwa inamfanya agombaniwe kila kona na mabosi wa kikoloni wakati huo. Alifariki mwaka 1969.

Mathias E Mnyampala ni shujaa wa Elimu.

Mathias_E._Mnyampala (1).jpg


Mnyampala cover-1.png
 
Baadhi ya vitabu alivyoandika.

1. Diwani ya mnyampala
2. Historia, mila na desturi za wagogo wa Tanganyika
3. Ugogo na Ardhi yake
4. Kisa cha mrina asali na wenzake wawili
5. Wasifu wa Sheikh Amri Abeid Kaluta
6. Vitabu vingine vingi vya mashairi na ngonjera
7. Maisha ni kugharimia ambacho ndicho hicho juu kinachozungumzia maisha yake.
 
Baadhi ya vitabu alivyoandika.

1. Diwani ya mnyampala
2. Historia, mila na desturi za wagogo wa Tanganyika
3. Ugogo na Ardhi yake
4. Kisa cha mrina asali na wenzake wawili
5. Wasifu wa Sheikh Amri Abeid Kaluta
6. Vitabu vingine vingi vya mashairi na ngonjera
7. Maisha ni kugharimia ambacho ndicho hicho juu kinachozungumzia maisha yake.
Weka basi angalau kimoja maana najua unavyo!
 
Miaka hiyo ncvhi ilikuwa na waandishi wazuri sana. Siku hizi nchi yeote ni ya makajanga na chawa tu. Ningali mtoto, nilipata kusoma kitabu kimojawapo cha Mathias Mnyampala na kweli kama walivyokuwa waandishi wa wengi wakati huo akina Katalambula, Shaffi, Kezilahabi na wengine, jamaa huyu alikuwa nguli sana katika uandishi
 
Wazee wetu wa zamani walisoma katika mazingira magumu sana, just imagine shule ipo chini ya mwembe, lakini walifanya vitu vikubwa sana vya kukumbukwa.
Vingine ni vipaji tu pyua. Fikiria Shaaban Robert aliishia sijui darasa la 4 lakini ona alivyokuwa anaimudu lugha. Nikichoka huwa narudia tena kusoma Wasifu wa Binti Saad. Jinsi anavyomweleza huyo mwanamke yaani mpaka unafurahi....
 
Ni ngumu kuzungumzia fasihi ya kiswahili bila kumzungumzia Mathias E. Mnyampala. Mnyampala alizaliwa mwaka 1917 huko Dodoma akiwa ni Mgogo. Baba yake alikuwa ni mfua chuma na alimiliki ng'ombe wengi ambao Mathias ndiye alikuwa mchungaji. Mwaka 1931. Akiwa kama na miaka 14-15 aliozwa mke!

Baadaye shule ilianzishwa kijijini kwao. Naye akaomba kuandikishwa. Waalimu wakamwambia wewe tayari una mke, hatuwezi kukupokea. Lakini hakukata tamaa. Kila darasa(la chini ya mwembe) lilipoendeshwa naye alihudhuria. Siku moja mwalimu alijaribu wanafunzi wake kusoma habari fulani, wengi walibabaika. Akamwambia na Mathias naye asome maana amekuwa akihudhuria kila siku. Mathias akasoma vizuri sana, basi mwalimu akaamua kumuingiza rasmi.

Baadaye akaenda shule ya misheni kujifunza elimu na dini. Alienda na mkewe. Ilipotakiwa kuendelea mbele akachaguliwa, lakini alishindwa kwenda sababu mke wake alikataa kubaki akiishi misheni.

Basi hapo akaendelea kujitafutia elimu yeye mwenyewe huku akifanya 'tempo' za kufundisha. Akaanza na kujifunza kiingereza huku akilipa watu wamfundishe.

Elimu hii ilimuwezesha kufanya kazi nyingi sana. Lakini mara nyingi alipata changamoto maana hakuwa na vyeti vyovyote vilivyomuonyesha kuwa kasoma. Lakini kazi yake nzuri ilikuwa inamfanya agombaniwe kila kona na mabosi wa kikoloni wakati huo. Alifariki mwaka 1969.

Mathias E Mnyampala ni shujaa wa Elimu.

View attachment 2545736

View attachment 2545737
Toleo hilo ni bandia na lnaeneza habari isiyosahihi kabisa la toleo la kwanza mwaka 1968. Hakuna kitu kama hicho kabisa wakati Mathias E. Mnyampala alikufa bila kumaliza kitabu chake. Toleo la kwanza ni 2013 baada ya kazi ya watafiti wa Vyuo Vikuu. Maisha ni kugharimia na Ugogo na ardhi yake vinapatikana mtandaoni kwenye archive DOT org na Google Books. Bora kusoma vitabu vya kweli !
 
Back
Top Bottom