Matokeo chanya kwa Simba

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258
https://www.facebook.com/video.php?v=947174105411801

Napongeza wachezaji mashabiki wanachama na wanazi wa timu zote mbili kwa mechi ya leo na kushukuru kwamba hakukua na maafa makubwa, Kipekee niwapongeze sana simba kwa kupigana hadi dk ya mwisho na Blagnon kweli amewakosa goli lawazi kabisa la ushindi tena kizembe kwa kuamini katika woga na kumtegemea mwamuzi

Licha ya kuwepo na changamoto kwenye mchezo wa Yanga vs Simba wa October 1 bado kuna wachezaji walionesha uungwana ndani ya dakika 90 huku makocha pia wakiwa mfano katika hilo.


Masuala ya Refa na kadi tuyaache kama kwamba yamepita kwani maamuzi yake hayabadiliki na yeye ni Binadamu, kuona mpira umeshikwa au la si kazi rahisi sana kwa watu 3 kati ya 22 uwanjani na off side ni moja ya sheria ngumu sana katika mchezo wa soka.

Naangalia mahali aliposimama refa na tukio la mpira kushikwa ................na hata iweje ile high ball ya Twite kuiwahi hadi alipokua Tambwe labda uwe na mabawa na wewe......na rahisi kuthibitisha kwa kuangalia marudio ya video, japo pia mwamuzi msaidizi alitakiwa kuliona lile tukio lakini pia ni kama alipewa mgongo na Tambwe


Ima ni refa mzembe tu atakuachia umsukumesukume na matusi juu na akuachie tu bila ya kukupa kadi

Nalaani sana fujo zilizofanywa na washabiki wa simba kung'oa ili kesho waje wadai HAKUNA viti, huu unaweza kuufananisha na utashi nje ya mwanadamu kwani si akili ya kawaida sana HII, pamoja na kugubikwa na jazba lakini NI UJINGA TU KUAMINI KWAMBA KUVUNJA VITI KUTAPOZA JAZBA YAKO





Nikiwa nasubiri kwa hamu mapato ya mecho ya leo kwa kutumia teknolojia, bado nina wasiwasi na kugubikwa kwa hujuma, kwamba zoezi limtewaliwa na vitimbi vya ugumu wa kupatikana kwa tiketi ili 'isije kuonekana jinsi wajanja wanavyopiga kwenye hizi mechi'

Matokeo ya leo yamekuwa muhimu sana kwa Simba, nilikua nikiwaambia watu kwamba kwa msimu uliopita simba alikua na matokeo kama haya na hata wakajiamini kiasi cha Kiiza Kuonesha kwamba bado muda tu, lakini tukumbuke jinsi ambavyo baada ya kipigo, Simba ilisambaratika, so kipigo cha leo huenda kingetutoa kwenye RELI kabisa,

Hii maana yake ni kwamba kwa pengo la pointi sita na kwa mtiririko wa matokeo kwa Simba licha ya kudumisha mshikamano miongoni mwa wachezaji, pia unachchea morali wa kufanya vizuri zaidi na kutafutwa kuungwa mkono na washabiki

KWA UPANDE WA YANGA...........ZITAFAKARINI NJIA ZENU.....ILA NIMEMKUBALI SANA DANTE NI EXIT STRATEGY NZURI SANA KWA UKUTA WA YANGA KWANI NAIONA NYOTA YA KIJANI KWA MABEKI NGULI


Ila dhahiri shari, kiuongo kinahitaji marekebisho makubwa, hakuna uelewani kabisa na hivyo kuifanya safu ya ushambulizi kushuka kuchukua mipira, na tatizo hili nililiona tangu mechi ya Stand United


Simba ikiwa pungufu imeizidi Yanga kwa kumiliki mpira na mbaya na hii ilikua inajidhihirisha kwa mwenendo wa mechi kwani Yanga iliyokua inaongoza kumiliki iliendelea kupungua kadri ya mchezo ULIVYOYOYOMA na hatimaye kuzidiwa kabisa mwishoni mwa mchezo dhahiri kuonesha kwamba Timu inachoka ......zaidi kuonesha kwamba YANGA dhaifu ni idadi ya rafu walizocheza mara mbili zaidi ya simba (22/12) na Kadi TATU ZA NJANO dhidi ya moja ya Simba huku Simba ikipiga mashuti mengi na kona nyingi zaidi ya YANGA....





 

Attachments

  • IMG_0181.jpg
    352.3 KB · Views: 94
ni kweli unachosema lakini mechi kama hizi zenye ushindani mkubwa refa anatakiwa kuwa makini na mwenye busara. fikiri anakataa goli halali halafu anakubali goli haramu na kadi juu vitu vingine hata kama ni sheria hekima pia itimike.
 
MWENYE VIDEO YA GOLI LA SIMBA LA OFFSIDE NA LA YANGA LA MKONO
 
ni kweli unachosema lakini mechi kama hizi zenye ushindani mkubwa refa anatakiwa kuwa makini na mwenye busara. fikiri anakataa goli halali halafu anakubali goli haramu na kadi juu vitu vingine hata kama ni sheria hekima pia itimike.
ukipata video niwekee humu maana nipo mbali
 
Sanya hana uwezo na pambano la simba na yeboyebo.Bora kutafuta marefa kutoka nje kuliko hawa ambao hata level za kimataifa hawawezi kufika.
 
TABIA YA KUNG'OA VITI IMEFANYA VITI VYA SHAMBA LA BIBI KUWA VYA ZEGE
 
simba si watu wa mchezo mchezo hata kidogo!
 

Attachments

  • 14485070_1055303067919635_5387086984100143786_n.jpg
    25 KB · Views: 84
Toa ushauri je wangemfanya nini huyu aliyewaudhi, wampige wote waliochukia?
Huu mchezo hauhitaji hasira mkuu, so kwa kung'oa viti wametatu tatizo? maamuzi duniani yako ya aina mbili kuna maazui ya akili na ya jazba haya yalikua ya JAZBA tu, ndio maana nasema ni hali nje ya UTASHI WA BINADAMU......haijawahi kutoke maamuzi ya refa yakabadilishwa kwa kung'oa viti
 
napiga picha simba ingefungwa leo, sababu ya kwanza ingekua ni refa ya PILI ni kocha kumpanga Lufunga
 
Mechi ya simba na yanga inaingiza pesa nyingi lakini tff na vilabu wanakuwa bahili wanashindwa kuchukua marefa bora toka nje wanahangaika na hawa wetu wabovu matokeo take fujo zinatokea wajifunze mechi za jadi za misri marefa wanatoka had I ufaransa
 
Mechi ya simba na yanga inaingiza pesa nyingi lakini tff na vilabu wanakuwa bahili wanashindwa kuchukua marefa bora toka nje wanahangaika na hawa wetu wabovu matokeo take fujo zinatokea wajifunze mechi za jadi za misri marefa wanatoka had I ufaransa
Jivunie chako mkuu ....haina maana kwamba marefa wa nje hawakosei kama unafuatilia sana mechi
 
Goal la Ajib la wazi kabisa
Goal la Tambwe la basketball [emoji119][emoji114]
Inauma sana japo najua hata wanajua waziwazi kuwa refa alikuwa kwao!
Ila wataenda kusimulia hadi msimu unaisha !!!
 
Goal la Ajib la wazi kabisa
Goal la Tambwe la basketball [emoji119][emoji114]
Inauma sana japo najua hata wanajua waziwazi kuwa refa alikuwa kwao!
Ila wataenda kusimulia hadi msimu unaisha !!!
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Yanga kumbe walikua kumi na tano taifa duuh hii futbol au????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…