RUGAHIMBILA E R
Member
- Mar 5, 2009
- 95
- 32
Matokeo ya kidato cha nne yalitoka hivi majuzi 2013 shule ya sekondari PEACE inayomilikiwa na meya wa bukoba bw. Anatori amani ilishika nafasi ya pili kimkoa ambapo watahiniwa 213 walifaulu na mmoja akkifeli. Lakini wanafunzi 72 aliofikiri kwamba wangepata alama za chini aliwatoroshea huko karagwe wakafanya mtihani shule ya sekondari iitwayo Adolec. Sasa ona matokeo ya adolec,kati ya watahiniwa 95 div. 4 wapo 54. walobaki yaani 41 wamepata 0.sasa katika 95 ina maana wanafunzi halisi wa adolec walikuwa 95-72=23 . Hata kama hawa wote wamepata 0 ina maana waliobaki yaani 17 wametokea peace sec. Hii ni baada ya mwaka juzi kufanya huu uhuni mpaka wanafunzi 84 wakafutiwa matokeo na necta. Ajabu hawa vijana wana leaving certificates za peace sec na wengine wamesoma amani tokea std 3 hadi form4.
Viongozi na wahusika wanajua na wako kimya na inaonekana hagusiki.
Sasa ebu amani atueleze hizi mbinu chafu za kuwadanganya wazazi kwamba shule yake inafaulisha ili aendelee kupata wateja na kuua elimu ya hawa watoto ataiacha lini?
Na je hata kwa hili wanamwonea eti kwa sababu ya ukristo wake?
Je hayo ndiyo maendeleo anayotaka kuwaletea wananchi huku akiua elimu ya watoto wao?
Je wazazi kwa nini msimchukulie hatua za kisheria huyu bwana hamuwezi kusimama mkasema inaotosha?
?..............ama kweli elimu yetu inauawa na viongozi wetu pia! )
Viongozi na wahusika wanajua na wako kimya na inaonekana hagusiki.
Sasa ebu amani atueleze hizi mbinu chafu za kuwadanganya wazazi kwamba shule yake inafaulisha ili aendelee kupata wateja na kuua elimu ya hawa watoto ataiacha lini?
Na je hata kwa hili wanamwonea eti kwa sababu ya ukristo wake?
Je hayo ndiyo maendeleo anayotaka kuwaletea wananchi huku akiua elimu ya watoto wao?
Je wazazi kwa nini msimchukulie hatua za kisheria huyu bwana hamuwezi kusimama mkasema inaotosha?
?..............ama kweli elimu yetu inauawa na viongozi wetu pia! )