Matokeo halisi kwa Yanga yanaanza kudhihirika

This is...

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
5,050
Reaction score
5,204
Matokeo wanayopata Yanga kwa Sasa Ni matokeo halisi ya mpira kwasababu kwa hapa ligi ilipofikia bahasha hazifanyi kazi tena.

Kil timu ukiondoa mbili au nne za juu yeyote anaweza kushuka daraja , hivyo kila timu inapambana kujinasua na hilo balaa. Mipango ya nje ya uwanja haina nafasi.

Kilichobaki ni kusingizia uchawi kwa sasa.

Mashabiki wa Yanga walishajiaminisha kwamba wao lazima kushinda mechi, kwasabab wao ni bora sana. Na hata wachezaji wanaingia uwanjani na mentality hiyo. Yanga itakuwa ktk presha kubwa kwa mechi zijazo kwa sababu pia walishajiaminisha wao tayari ni mabingwa msimu huu.

Timu zitakazokutana na Yanga pia zimeshajifunza kuwa kumbe inawezekana kuizuia Yanga isifunge na inawezekana.

Kuna wale wanaomlaumu Cedric Kaze, lakini hata mechi ya jana na Prison Nabi alikuwepo na timu imedroo.

Mashabiki wanasahau kuwa ikiwa timu inatengeneza nafasi na washambuliaji hawafungi basi Hilo Ni tatizo la wachezaji na si kocha.Kama nafasi zinakuwepo na wachezaji hawafungi mnataka kocha aingie akacheze?

Ni mtazamo wangu, hebu tusubiri tuone itakuwaje. Muda utaamua.

BTW kila mtu ashinde mechi zake. Huu ndiyo mpira.
 

Kaze kafurahi sana Jana
 
Kwahio prison wangepewa bahasha penalty isinge paa? unasema wachezaji wanakosa magoli wenyewe sasa hapo bahasha ina husika vipi?
 
Yaani kwa mpira ule wanaocheza yanga aisee kimataifa wataisoma namba .
Mpira wa kimataifa unachezwa angani? wabongo kwa ujuaji, kama Namungo na Biashara waliweza ku challenge Yanga washindwe nini?
 
Usisahau pia matokeo ya simba kabla ya kuifunga Ruvu amesuluhu na hawa tena mfululizo
Simba vs Polisi
Vs Yanga
Vs Namungo
Kwa mtiririko huu una uhakika gani wa kushinda viporo vyako?
 
Wakipoteza point mechi ijayo lazima watafutane na kufukuzana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…