Matokeo Kidato cha Sita yatangazwa rasmi

Status
Not open for further replies.
humu si kuna madogo wa Tambaza humu,tatizo ni nini madogo

tatizo descipline......... ninaowasikitikia ni wale ndugu zangu wanaotoka kwenye familia za ugala na mguu wa kuku... wazazi wamejitahidi myoto anaishia kupata zero ya kujitakia.......
angalau basi hata ukapatakadegree kako ukakosa kazi hilo jambo jingine........ big up kwa wote mliofaulu brothers and sisters.........
 
General Studies ilikuwa unawekea S,sasa hv watu wanagonga A,B,C,D,E,S kama masomo mengine,kweli BRN iko kazini,asante mtoa post kwa kutupa matokeo.
kwasasa hamna S kama grade vilevile hzo g.s na bam hazhesabiwi kwnye divsn.
 
Haloo wadau hivi Ndalichako alijiuzuru au alibadilisha kitengo? Nipo kijijini na sijapata taarifa zake nina takribani mwaka sasa.

Mkuu ana likizo ya mwaka ila anahusika na hiyo Top down hasa No 8.
 
Imekuaje hizi Tech ziwe kwenye list ya kumi bora mkiani? Kweli Iyunga, Mtwara Tech, nini kimewapata hawa?

Ukiangalia hii BRN ni kwa arts tu science pamoja na kubebwa shule zote zenye div 3 na 4 ni zile za michepuo ya science.. sijui tutakija kuwa na mainjinia gani na madaktari gani r.i.p elimu ya bongo
 
# HABARI MATOKEO YA KIDATO CHA 6 2014
YATANGAZWA!
Matokeo ya mtihani wa kidato cha 6
yaliyofanyika tarehe Mei 5 - 21, yametoka na
jumla ya watahiniwa 30,225 sawa na asilimia
85.73 wamefaulu katika madaraja ya I- III.
Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia
95.98 ya watahiniwa waliofanya mtihani
kidato cha 6 wamefaulu. Wasichana
waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu
ni 26,825
- Watahiniwa waliopata division IV ni 4,420
sawa na asilimia 12.54
- Watahiniwa waliopata zero (0) ni 612 sawa
na asilimia 1.74.
- SHULE 10 ZILIZOONGOZA
1. Igowole
2. Feza Boys
3. Kisimiri
4. Iwawa
5. Kibaha
6. Marian Girls
7. Nangwa
8. Uwata
9. Kibondo
10. Kawawa
- SHULE 10 ZA MWISHO
1. Ben Bella
2. Fidel Castro
3. Tambaza
4. MuhezaHigh School
5. Mazizini
6. Mtwara Technical
7. Iyunga technical
8. Al- falaah Muslim
9. Kaulia
10. Osward Mang'ombe
 
acsee 2014 nna 3 ya 10.phys C,chem B na biology B.je naweza pata nafasi ya kusoma pharmacy muhimbili?.na kama haiwezekani unanshauri nikasome course gani?

maybe ujaribu DDS au environmental healthy science...pharmacy sidhani
 
jamani hiyo ya kumi mkiani ndo imejitahidi katika za mwisho au ndo ya mwisho
 
Imekuaje hizi Tech ziwe kwenye list ya kumi bora mkiani? Kweli Iyunga, Mtwara Tech, nini kimewapata hawa?
Hizo ni shule za. Sayansi.......so usiogope wanaoongoza wote ni masomo ya arts(sanaa)
 
hatari huu ni mpango wa matokeo makubwa sasa... Je, wajua kuwa Waziri asipofikisha malengo anatakiwa ajiuzuru? Nilijua tuuu watachezesha matokeo... Bahati mbaya mimi nimefundisha shule moja mkoani manyara lakini naangalia hata wale mazuzu wamefaulu... kweli ni BIG RESULTS NOW not Tomorrow!
 
Mkuu ana likizo ya mwaka ila anahusika na hiyo Top down hasa No 8.

Mkuu mimi huko sihusiki na sitaki kuhusika, namuulizia tu dada yetu Dr. Joyce Ndalichako, ni mtu mwenye msimamo ktk mambo ya msingi na aliisimamia vzr sana NECTA kabla ya kuja haya ma miradi ya big rizat nao. Namkumbuka sana, bora arudi asimamie utendji wa zamani wala sio huu wa big rizat.
 

Watu walikuwa hawamwelewi mama Joyce Ndalichako lakini kwa hali ilivyo sasa wameshaanza kumkumbuka kabla hata hajamaliza mwaka tangu alipong'oka pale NECTA. Ukweli kama una mapenzi mema na nchi hii huwezi kufurahia hata chembe kinachoendelea kwenye sekta ya elimu eti kwa kivuli cha BRN
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…