Wana jf leo saa 7 mchana waziri ametangaza matokeo ya drs la 7.Kwa mujibu wa TBC-dira ya mchana kiwango cha ufaulu kimeongezeka!!Ilisemekana hali ni mbaya!Lakini hii ndio serikali ya ccm huwa hawasemi ukweli,wao ni kuchakachua kila kitu sasa hadi Elimu.
Yatabandikwa shuleni kwa mtoto wako au bomani. Hakunaga website inayoonyesha MATOKEO ya std vii.wakuu nikitaka niangalie matokeo ntayapata kwenye website gani ? msaada tafadhali
kama kweli kuamka ni kutinga jf basi karibu sana, na nimekugongea 'like' ya kwanza.Watanzania ukweli tuinuke kukemea udhalimu huu juzi tu waliotoka kusahihisha mitihani walikuwa wanasema hali ni mbaya sana lakini tumeambiwa ngoja tuangalie tena hivi kilichokuwa kinaangaliwa ni nini tena mtomto kaandika 2+2=5 sasa wameendafuta wakaandika na 4 au wamekubali kuwa na tano halafu wamefauru,watoto wa shukuru kawambwa hawapo huko jamani,wtanzania jamani tuamkeni jamani namtafuta waziri kivuli wa Elimu sijui nae yupo wapi atuambie ukweli ni upi na yeye kazi yake ni ipi,Ee Mungu sisi hatujui alietuloga ila wewe kwa kua unaona sirini tuokoe na huyo mchawi alituloga watz.
Uwezo mdogo wa kufikiri kwa watanzania ndio mtaji mkubwa wa ccm katika mafanikio yao.
Na wao ndio wasababishi! Na hii ndio sera yao kubwa,ili umtawale mtu kiurahisi mnyime elimu! Nenda vijijini uone wazee wanavyoikumbatia CCM wakati wao ndio wahanga wa elimu duni! Aargh &*¿!!