awali ya yote ningependa kuwapongeza wanafunzi waliokuwa kwenye seminari za kikristo kwa kufanya vizuri, hii sio kwamba waliosoma kwenye shule hizo ni wakristo peke yao humo kuna waislam, wahindu na wabudha pia , so mafanikio ni ya taasisi na wanafunzi bila kujali dini zao
ni ukweli usiopingika kuwa ili mwanafunzi aweze kufanya vizuri kuna mazingira yanayohitajika ili aweze kufaulu kama vile, uwepo wa walimu wa kutosha na wenye ubora na walio na morali ya kazi, uwepo wa vitendea kazi/zana za elimu k.v vitabu vya ziada,kiada na rejea,uwepo wa maktaba, uwepo wa maabara, mazingira rafiki ya elimu, standi za kufundishia, na kadhalika wa kadhalika
kitu kimoja kizuri kwenye shule za kikristo ni mfumo wao wa kutoa elimu kwani bahati nzuri nyingi ya shule hizi huwa wana karibu vitu vyote vilivyotajwa hapo juu, maana aidha shule hizi huanzishwa na makanisa yenye sadaka kubwa, misaada toka nje ya nchi au huwa wanatoza ada kubwa kwa ajili ya kumudu gharama za uendeshaji na pia idadi ya wanafunzi katika shule hizi huwa haizidi 100 kwa kidato aghalabu 50 hivi. bahati mbaya kwa shule za kiislamu huendeshwa kwa shida zikikabiliwa na changamoto nyingi za uendeshaji na ukosefu wa fedha,lakini hili hutokea zaidi kwa kuwa shule hizi zinatoza ada ambayo ni kidogo sana ukilinganisha na shule za kikristo maana zinafahamu hali ya maisha ya watanzania na kwa kuwa ada huwa ndogo hupelekea wanafunzi kuwa wengi kwenye shule hizi kitu ambacho hukompromise ubora wake
pamoja na hayo tujiulize mbona kuna seminari au shule zenye majina ya 'watakatifu' wa kikiristo na bado zafanya vibaya?zingine zipo dar hapohapo na zingine zipo huko mikoani? mtu aangalie shule mfano ST PAUL'S LIULI, DAR ES SALAAM CHRISTIAN SEMINARY, DAR ES SALAAM BAPTIST SECONDARY, BANGALA LUTHERAN JUNIOR SEMINARY, ANGALIA SHULE KAMA HII
S0983 TUMAINI LUTHERAN SEMINARY <H3>DIV-I = 0 DIV-II = 3 DIV-III = 3 DIV-IV = 44 FLD = 30
SASA tatizo hapa ni nini? ni ubora wa wanafunzi au kukosekana kwa mazingira bora ya kielimu? maana hii pia ni shule ya kanisa
binafsi watanzania tuache kulumbana na kujisifu kwamba eti shule ya dini/dhehebu fulani ni nzuri kuliko ya dini/dhehebu jingine ilhali wanaosoma kwenye shule hizo wengi wao ni watoto wa watanzania wenye kipato cha kati na sio watanzania wenye kipato cha chini, hivi tujiulize mwanafunzi kutoka kule interior kabisa nkasi, nachingwea, kibondo, ludewa, ikunguluyabashashi, kilolo, kieto huko zoisa banyibanyi, kilosa kule ureling'ombe au tanganganyika masagati ifakara je anaweza mudu shule hizo mnazojisifia nazo? ndio maana serikali imekuwa ikiwaomba wamiliki wa shule wapunguze ada. kumbukeni wanaosoma shule hizi ni watanzania na wanaofeli ni watanzania wote pasi na kujali dini zao kwani wakristo kwa waislamu
lakini swali langu dogo ni kuwa kwanini seminari siku zote hazishiki namba kwenye mitihani ya kidato cha sita??? sikuzote kumi bora zimekuwa zikitawaliwa zaidi na shule za serikali kama vile ilboru, kibaha, mzumbe, kilakala, dakawa, msalato and the like?? kwa nini hawa wanaseminari huongoza kidato cha nne na hushindwa kidato cha sita? na mbona wanaseminari hawa pindi wajapo huku kwenye shule zetu za serikali huwa tunawaburuza mbaya kwenye performance darasani kama wao ni vichwa ile mbaya?
kwa hiyo mazingira rafiki huwasaidia wanafunzi wa seminari lakini haithibitishi kwamba wao ni bora sana kuliko wanafunzi walioko kwenye shule za kawaida
</H3>