Elections 2010 MATOKEO ya kura za awali CCM August 1, 2010

Elections 2010 MATOKEO ya kura za awali CCM August 1, 2010

Mwakyusa anaongoza na Kasesela wa tatu ebu check online copy ya the guardian utaona
 
Watu vigeuvigeu wafaa watendwe hivi...!
Next time kama ipo atakua makini..
 
Hivi Benson Mwang'onda, aka Kibaraka vipi?
Akiangushwa nitajua Kweli Mbeya hawachezewi .......

Mwang'onda amedondoshwa vibaya na Mpesya........kweli Mbeya si watu wa kuwawekea vibaraka!!

Hongereni watu wa Mbeya, tunawaomba kura za Urais mpeni Dr. Slaa!!
 
sasa tuweke majina ambayo tunauhakika kuwa wamepita.


1. Pof. Mwandosya
2. Prof. Mwakyusa
3. Prof.Anna Tibaijuka
4.Samwel Sitta
5. Anne Killango
6. Dr. Mwakyembe
7.
8.
9.
10.
 
Kuna habari kuwa waziri mwingine ameangukia pua kwenye kura za maoni,huyu si mwingine ni Waziri Masha,mwenye detail zaidi aatuhabarishe,shigongo aibuka kidedea
 
You are joking about Shigongo right? Hivi nani anampigia kura mtu kama Shigongo?

Masha huyo it serves him right.

Speaking of Masha nimemkumbuka FMES.

Hivi mzee Malecela yeye vipi ?
 
Mbona asubui walitangaza kwamba kaibuka kidedea? Au ilikuwa bado Radio mbau?
 
Pole sana mzee shelukindo,naamini kijana ataendelea kukuheshimu na kama atapata kiti hicho cha ubunge basi udhoefu wa muda mrefu ulioupata miaka yote ya utumishi wako selikarini utasaidia kupeleka watu wa bumbuli mbele.


niliwahi kuwa katika group moja ya wazee walikuwa wanaongea na shelukindo miezi ya mwisho wa mwaka jana na alisema and i quote " nilikuwa sitaki kugombea lakini huyu makamba kanifanya nirudi, nilimshinda yeye sasa kaleta mwanae, nataka nimshinde na yeye na hata akileta ukoo mzima nitawashinda"

sasa kapigwa chini sijui atasema nini tena
 
Baada ya kuhakikisha 'vijana' wake wanapita kwenye kura za maoni ndani ya CCM, ni wazi sasa EL njia ni nyeupe kuelekea kumrithi swahiba wake wa kufa na kuzikana JK ifikapo 2015.

Kwa matokeo yaliyokwisha nifikia, karibu wabaya wote wa EL wamepigwa mweleka isipokuwa baadhi tu kama Mama Malecela na Mwakyembe ndo wamefanikiwa kushinda!

Hii inazidi kuthibitisha nguvu aliyonayo mwanzilishi wa mitandao ya 'fitina' katika siasa za Tanzania. Nazidi kuingiwa na hofu kadri pesa (rushwa) na fitina zinavyoendelea kutamalaki katika chaguzi za Tanzania!!

Hii sheria iliyosainiwa kwa mbwembwe na mikogo itasaidiaje kupambana na rushwa katika chaguzi zetu?
 
Kuna tetesi Joe Bendera nae chali korogwe huko?
 
Kuna mtu ana update za morogoro mjini yule professor wa sua na Abood imekuwaje ?
 
Wapo Selelii, Mwapachu, Masilingi
headline_bullet.jpg
Prof. Mwakyusa ana kazi nzito
headline_bullet.jpg
Sitta, Mwakyembe, Dewji wapeta
headline_bullet.jpg
Prof. Mwandosya hakamatiki


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Rais Jakaya Kikwete akipiga kura ya maoni kuchagua wana CCM wanaomba kuteuliwa kugombea ubunge na udiwani katika Jimbo la Chalinze Pwani jana. Rais Kikwete alipiga kura yake kijijini kwake Msoga wilayani Bagamoyo.



Baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana jioni walikuwa wanaongoza huku Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa, akiwa amechwa nyuma katika matokeo ya awali ya kura za maoni za uteuzi wa udiwani na ubunge zilizopigwa jana nchini kote.
Matokeo ya awali, yanaonyesha kwamba, katika Jimbo la Rungwe Magharibi, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa, alikuwa ameachwa nyuma na mpinzani wake, Richard Kasesela, aliyejizolea jumla ya kura 1,469 dhidi ya kura 840 alizokuwa amepata Profesa Mwakyusa.
Katika matokeo hayo, pia aliyewahi kuwa Mbunge wa Kigamboni (CUF) mwaka 2000-2005, Frank Magoba, alikuwa anafanya vibaya katika kinyang'anyiro hicho.
Kwa mujibu wa matokeo hayo, katika Kata ya Ikuti; Tawi la Lienje, Kasesela (44), Magoba (36), Profesa Mwakyusa (36) na Mwakandube (15); Tawi la Kiobo Juu, Kasesela (101), Profesa Mwakyusa (8), Magoba (6) na Mwakandube (1); Kiobo Chini, Kasesela (186), Profesa Mwakyusa (10), Magoba (7) na Mwakandube (1); Tawi la Ibungu, Kasesela (101), Profesa Mwakyusa (9), Magoba (5) na Mwakandube (2); Tawi la Ikuti, Kasesela (128), Profesa Mwakyusa (31), Magoba (15) na Mwakandube (3); na Tawi la Lumbe, Kasesela (81), Profesa Mwakyusa (21), Magoba (6) na Mwakandube (0).
Kata ya Malindo; Tawi la Kapugi, Profesa Mwakyusa (126), Magoba (77), Kasesela (73) na Mwakandube (15)
Kata ya Malimbo; Tawi la Ibungila, Profesa Mwakyusa (191), Kasesela (180), Magoba (20) na Mwakandube (12); Tawi la Igalamo, Profesa Mwakyusa (203), Kasesela (16), Magoba (9) na Mwakandube (0); Kata ya Kimo, Profesa Mwakyusa (102), Kasesela (455), Magoba (17) na Mwakandube (7), na Kata ya Swaya, Kasesela (101), Profesa Mwakyusa (103), Magoba (0) na Mwakandube (0).
Katika Jimbo la Kyela, mkoani Mbeya, Dk. Harrison Mwakyembe aliibuka mshindi, baada ya kuwabwaga wapinzani wake wanne kwa kujizolea jumla ya kura 7,457 na kufuatiwa na George Mwakalinga aliyepata kura 525, zili Mponda, alikataliwa kupiga kura kwa madai kuwa jina lake halikuonekana kwenye rejista ya wanachama iliyopelekwa na mjumbe wake.
Mosi mwenyewe alisema hizo ni njama za makusudi ambazo ziemefanywa na viongozi wa tawi hilo ili asipige kura kwa kuwa hampendi mgombea wanayemuunga mkono. "Huu uchaguzi wa kata ya Azimio ni kituko hakijawahi kutokea na kwa kweli kwa hili hata nikifukuzwa kwenye chama sijali, nitapigania haki yangu hadi mwisho ... haiwezekani mimi ni kiongozi na nina kadi zote kuanzia ya UWT, UVCCM nakataliwa kupiga kura kwa sababu za kijinga kabisa," alisikika akifoka kwa hasira.
"Mimi nimewasikia kwa masikio yangu wanasema watafanya kila wanaloweza kuhakikisha wanamweka mtu wao na njama zote hizo zimefanyika nyumbani kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa...wamefanya hila kila wanayeona hamuungi mkono mgombea wao wanamwondoa kwenye rejista ya wanachama na mimi jina langu lilikuwepo limekatwa mstari," alisema Mosi huku akifoka nje ya ofisi ya tawi hilo ambako kura zilikuwa zikiendelea kupigwa.
Katibu wa CCM tawi hilo, Badru Kichupa, alisema inawezekana jina la Mosi halikupelekwa kituoni hapo na mjumbe wake hivyo yeye hapaswi kulaumiwa.

CHANZO: NIPASHE
 
Na Asumpta Nshunju Mshama kamwangusha Waziri Kamala jimbo la Nkege. Pia Getrude Mongella kapita Ukerewe.
 
.....njia ni nyeupe kuelekea kumrithi swahiba wake wa kufa na kuzikana JK ifikapo 2015.

Nilidhani kumrithi Slaa.....
 
Kuna mtu ana update za morogoro mjini yule professor wa sua na Abood imekuwaje ?

nasikia aboud kampiga chini jamaa,

naomba mwenye habari za huko kondoa kwa kijana edwin sanda atupe updates, na mbarali tuone geofrey mwangulumbi vipi kampiga chini yule mama?
 
Back
Top Bottom