Elections 2010 MATOKEO ya kura za awali CCM August 1, 2010

Elections 2010 MATOKEO ya kura za awali CCM August 1, 2010

Naam waungwana, matokeo rasmi ya jimbo la nzega kwa wagombea wawili waliokuwa wakichuana sana ni kaam nilivyoandika hapo juu, japo najua kwa kufanya hivi nitaporomoshewa matusi ya kumwaga ila ukweli ndio huo nami binafsi nimeongoza kwa kishindo kura za maoni nafasi ya udiwani

Swali la kizushi,

Je CCM wanajua kuna ufisadi nchi hii? Ninashindwa kuamia pale ambapo mpiganani Seleli na mtizamo wana CCM kwenye hii vita ya ufisadi!
 
Na nafasi nzuri kwa Selelii kwenda upinzani kwani hana nafasi CCM kutokana na misimamo yake.
Aende Chadema kuleta mapinduzi ya kweli kwenye siasa za TZ
 
Mgombea tiketi ya Ubunge kupitia CCM jimbo la Kawe, Kippi Warioba amempita mgombea wa pili Angela Kizigah kwa kura 700. Fisadi Adamjee kaangukia pua! Eric Suma nae chali!
 
Keil,

Naliongelea kuhamia CHADEMA kwa sababu moja kubwa kuwa tayari atazoa baadhi ya watu wake na ahame nao CHADEMA. Chadema tayari watakuwa na wajumbe wengi ambao ni PRO Mwakalinga na si Pro CCM.

Hii zaidi ipo kama njia ya kusaidia KULINDA kura za Slaa kwenye uchaguz wa RAIS.

Kwa hali ilivyo sasa, sidhani kama atataka tena kurudi kwenye SIASA. Sintashangaa akirudi zake UK na kwenda kubeba Box za Kichina kama watamhitaji au abadili kazi kabisa. Kila kitu kina uzuri na ubaya wake. Familia yake itakuwa upande fulani happy kuwa baba KARUDI.
Anyway, kwenye maisha huwa kuna kushinda MAPIGANO na kushinda VITA. Only God knows nani atakuwa mshindi wa VITA. Ndiyo maana huwa wanasema "Mchekaji, ni yule anacheka wa MWISHO."

Ngoja tusubiri matokeo ya SIKONGE sasa na DR. SLAA kivumbi kikianza.

Hawezi kuja Chadema kwa sababu yeye ni CCM per se na alikuwa kwenye uzamini mzito wa Wakuu, labda atachoweza kufanya akiwa bado chini ya hao wazamini ni kumpinga DR kwa kuisupport Chadema Bila kuhama chama, pamoja na hayo DR bado anahitajika kwa hiyo ni sawa tu
 
Mgombea tiketi ya Ubunge kupitia CCM jimbo la Kawe, Kippi Warioba amempita mgombea wa pili Angela Kizigah kwa kura 700. Fisadi Adamjee kaangukia pua! Eric Suma nae chali!

Kwa nini kippi naye asiitwe Fisadi Kippi Warioba?
 
Kutoka Njombe, Makweta ameanguka vibaya, akishika nafasi kama ya tatu hivi. Matokeo ya awali yanaonyesha Deo Sanga anaongoza, akifuatiwa na Alatanga Nyagawa.
 
Sitegemei kuna mtu atashindana na Mwandosya kule kwa sasa, hata wapinzani wanakiri Mwandosya ni maji marefu. Ni sawa na kutaka kushindana na Magufuli jimboni kwake, unatakiwa kufanya miujiza. Mwandosya japo yuko DSM karibu kila mwezi anapita jimboni kwake kuhimiza maendeleo na anajitolea sana. Sio msemaji sana lakini ni mtendaji mahiri, sayansi kweli anaitumia vizuri.


Nakubaliana na wewe mkuu!

Binafsi nimeenda Rungwe kama mara mbili hivi mwaka jana kwa vipindi tofauti tofauti, nikashangaa mara zote hizo kukutana na Prof. Mwandosya akihimiza maendeleo jimboni mwake!! By then sikujua kwamba ni coincidence tu ama ndo kawaida yake ya kuwa karibu na wapiga kura.

Kuna viongozi nchi hii wangepewa nafasi nafikiri tungeweza kupiga hatua!!
 
Issue siyo ufisadi, jamaa alilisahau jimbo...it's that simple. Wanakiji wanataka maji, elimu na afya bora, mafisadi baadaye!!!!!
 
Mgombea tiketi ya Ubunge kupitia CCM jimbo la Kawe, Kippi Warioba amempita mgombea wa pili Angela Kizigah kwa kura 700. Fisadi Adamjee kaangukia pua! Eric Suma nae chali!

Du Adamjee bado yupo, and still dreaming kuwa mbunge wa Kawe? Bongo bana!!!!!!!!!!
 
Kutoka Njombe, Makweta ameanguka vibaya, akishika nafasi kama ya tatu hivi. Matokeo ya awali yanaonyesha Deo Sanga anaongoza, akifuatiwa na Alatanga Nyagawa.

Safi sana....
 
tupate matokeo yote kwa mpigo nadhan itatusaidia!
 
Kwa ujumla matokeo ya CCM primaries yametuonyesha makubwa yafuatayo

  • ukuaji wa kiujumla wa demokrasia
  • kazi bado kwani kuna watuhumiwa ambao wanahitaji August 14 iwatetee au kuwamaliza
  • baadhi ya majimbo yalikithiri kwa rushwa na rushwa sio rahisi kuisha kwa mtindo huu
  • time for change is now... tujifunze kutoka kwa tingatinga, makweta etc
  • opposition bado wanakazi kubwa sana ahead of october election
Acid
 
Naam waungwana, matokeo rasmi ya jimbo la nzega kwa wagombea wawili waliokuwa wakichuana sana ni kaam nilivyoandika hapo juu, japo najua kwa kufanya hivi nitaporomoshewa matusi ya kumwaga ila ukweli ndio huo nami binafsi nimeongoza kwa kishindo kura za maoni nafasi ya udiwani
Kwanza hongera zako kushinda udiwani, pili hongera kwa Bashe kumshinda mpiganaji Seleli hata kama ni kwa kutumia masalia/mabaki ya Kagoda.

Wapenzi wa Selelii wasiwe na shaka, hata kama Bashe angeshinda kwa asilimia 99% na Selelii asilimia 01%, bado CCM itampitisha Selelii na kumtosa Bashe, kuna secret agreement kwa wabunge makamanda waliahidiwa kupitishwa no matter what, nao ndio wakakubali kuitosa CCJ.

Hivyo kama wana CCM wa Nzega, wanawakilisha wakazi wote wa Nzega, na chaguo lao ni Bashe, basi atakayekwenda upinzani na awe Bashe, asimame na Selelii kwenye sanduku la kura, hivyo Jimbo la Nzega tuanze kulihesabu upinzani.

Kama na kuchekelea ushindi, kambi ya Bashe, chekeni sana, mkisubiria panga la NEC na mtalia sana, piga ua CCM haiwatemi makamanda wake, almanusura waimege ikatike vipande viwili, wakakubali kuinusuru CCM, sasa ni zamu ya CCM kuwanusuru.

Bashe ajiandae kwa safari, the only choice ni Chadema, tatizo langu kwake ni jee Chadema itawakubali hawa makuwadi wa RA?. Jee itafungua milango yake kuwakaribisha nyoka?.

Mwito wangu kwa Chadema, acha milango wazi kwa yoyote ajaye bila kujali alikuwa akimtumikia nani, concetration yao kwa sasa, iwe ni idadi ya viti vingi bungeni.
 
watu hawataki ujinga, sasa izi ngumi mkononi majimbo mbalimbali inaashiria nini?
 
jamani naomba mtu mwenye matokeo ya kura za CCM toka hizi sehemu, atueleze nataka kujua kama Ngawaiya na Mramba wamepita au la?
 
Kwanza hongera zako kushinda udiwani, pili hongera kwa Bashe kumshinda mpiganaji Seleli hata kama ni kwa kutumia masalia/mabaki ya Kagoda.

Wapenzi wa Selelii wasiwe na shaka, hata kama Bashe angeshinda kwa asilimia 99% na Selelii asilimia 01%, bado CCM itampitisha Selelii na kumtosa Bashe, kuna secret agreement kwa wabunge makamanda waliahidiwa kupitishwa no matter what, nao ndio wakakubali kuitosa CCJ.

Hivyo kama wana CCM wa Nzega, wanawakilisha wakazi wote wa Nzega, na chaguo lao ni Bashe, basi atakayekwenda upinzani na awe Bashe, asimame na Selelii kwenye sanduku la kura, hivyo Jimbo la Nzega tuanze kulihesabu upinzani.

Kama na kuchekelea ushindi, kambi ya Bashe, chekeni sana, mkisubiria panga la NEC na mtalia sana, piga ua CCM haiwatemi makamanda wake, almanusura waimege ikatike vipande viwili, wakakubali kuinusuru CCM, sasa ni zamu ya CCM kuwanusuru.

Bashe ajiandae kwa safari, the only choice ni Chadema, tatizo langu kwake ni jee Chadema itawakubali hawa makuwadi wa RA?. Jee itafungua milango yake kuwakaribisha nyoka?.

Mwito wangu kwa Chadema, acha milango wazi kwa yoyote ajaye bila kujali alikuwa akimtumikia nani, concetration yao kwa sasa, iwe ni idadi ya viti vingi bungeni.

...... yote tuyaonayo hapa duniani yalitoka kwa NENO!. Nai-boomark hii nyuzi nikiamini kabisa na kujipa wajibu wa kuifufua siku ya kutimia kwa uliyosema Mkuu.
 
Kwa nini kippi naye asiitwe Fisadi Kippi Warioba?

No, swali ni, kwa nini anayetaka kumuita Kippi Warioba amuite Kippi fisadi? The same applies to Adamjee.

Don't get it twisted, innocent until proven guilty, not guilty until proven innocent, get it ?
 
he!!!! si nilisikia kwamba kawe wamebatili matokeo?
 
Back
Top Bottom