Matola kuondoka Simba

Chevi_masta

Member
Joined
Sep 13, 2021
Posts
11
Reaction score
15
Kocha Seleman Matola anaondoka Simba kwa muda ili akasome. Matola amepata fursa ya kwenda kusoma kozi ya leseni A ya CAF, ataanza Novemba 21 ambapo atasoma kwa wiki mbili, kisha atarejea kikosini hapo kwa kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo aliyoyapata.

Cc: Mwanaspoti
 
Kila la heri ktk masomo yakee, akirejeaa aje awalishe wachezaji alichojifunza darasan.
 
Huyu sidhani kama Form Four B alimaliza!! anyway acha ikae hivyo tu,,
 
Sasa mafunzo ya muda wa wiki mbili tu yanamuondoaje kikosini?
Kulikuwa kuna haja gani ya kuja na taarifa ya namna hiyo kwa umma?

Wakati wowote kuanzia wiki ijayo huenda ligi na mashindano ya kimataifa ya vilabu yakasimama ili kupisha mashindano ya kombe la dunia, na muda huo wachezaji, makocha na watu wengine hawatakuwa pamoja kikosini, na ndio muda huo huo Matola atakuwa mafunzoni.
 
Wanatafuta tu namna ya Kumuondoa Kijanja ( Kidiplomasia ) kwani Malalamiko dhidi yake kwa Uongozi yamezidi.
 
Jambo jema..kila la kheri mwalimu Matola
 
Ligi zinaanza kusimama baada ya mechi za leo..lakini sio kwa Tanzania.
 
wakisomeshwa.. wapewe nafasi pia ;ni wakati wa kuwapa nafasi makocha wakizawa nao waoneshe ufundi na sio kukariri tu wakigeni kuwa na ubora zaidi.

Sent from my itel A661W using JamiiForums mobile app
 
Tatizo siyo kwenda kusoma! Tatizo lipo kwenye kufaulu vizuri hayo masomo. Safari hatutaki tena visingizio.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…