DOKEZO Matrafiki wa Ifakara na Lupiro ni shida kubwa

DOKEZO Matrafiki wa Ifakara na Lupiro ni shida kubwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Ulongupanjala

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2013
Posts
8,273
Reaction score
13,567
Habari ndugu zangu?

Naomba niseme haya ili wenye mamlaka wawachukulie hatua ikiwemo waziri wa mambo ya ndani na IGP nk.

Ifakara na Lupiro ipo mkoa wa Morogoro.

Iko hivi trafiki wa Ifakara hasa maeneo ya kabla na baada ya daraja la Magufuli (Kivukoni) wamekuwa kero sana kwa waendesha bajaji kwa kuwadai 2,000(elfu mbili) kila wanapopita hapo, na dereva asipotoa hiyo pesa humwandikia faini ya elfu kumi au kumtishia kumpeleka kituo cha polisi.

Yaani wamejihalalishia malipo ya pesa hizo kuwa ni stahiki zao,nasikia huko nyuma dereva bajaji walilalamika sana mkuu wa wilaya aliingilia kati na wakapunguza kuchukua elfu mbili toka kwa kila bajaji inayopita.

Kwa kifupi hakuna bajaji inayopita bila trafiki kuchukua elfu mbili. Pia trafiki wa Lupiro jirani na stendi ya mabasi ya Lupiro nao tabia zao za kuchukua elfu mbili zipo palepale, najiuliza mshahara hautoshi au lengo lao ni kufanya maisha ya dereva bajaji yawe ya dhiki kila kukicha?

Kama kuna taasisi inayoitwa ya kuzuia rushwa nendeni Ifakara na wilaya ya Ulanga mkaone matrafiki wanaochukua rushwa bila haya wala woga.

Nawasilisha.
 
leo mada ni waziri mkuu na wapigaji,mahakama,trafiki tumeanza kuwatolea uvivu naona kila uzi
 
Piga simu TAKUKURU 113 ripoti na watachukua hatua
 
Pia kuna wale wanaokaa maeneo ya Kikwawila kama unatoka ifakara kwenda mikumi wale nao njaa kali sana. Umesikia habari ya yule aliegongwa na boda na kufa kule Mang'ula?
 
Kwa kuwa umeuliza maswali mawili basi Mimi najitolea kujibu swali la Kwanza.

Jibu NI kuwa "Hakuna mshahara unaotosha"
 
Iko hivi trafiki wa Ifakara hasa maeneo ya kabla na baada ya daraja la Magufuli (Kivukoni) wamekuwa kero sana kwa waendesha bajaji kwa kuwadai 2,000(elfu mbili) kila wanapopita hapo, na dereva asipotoa hiyo pesa humwandikia faini ya elfu kumi au kumtishia kumpeleka kituo cha polisi.

Yaani wamejihalalishia malipo ya pesa hizo kuwa ni stahiki zao,nasikia huko nyuma dereva bajaji walilalamika sana mkuu wa wilaya aliingilia kati na wakapunguza kuchukua elfu mbili toka kwa kila bajaji inayopita.

Kwa kifupi hakuna bajaji inayopita bila trafiki kuchukua elfu mbili. Pia trafiki wa Lupiro jirani na stendi ya mabasi ya Lupiro nao tabia zao za kuchukua elfu mbili zipo palepale, najiuliza mshahara hautoshi au lengo lao ni kufanya maisha ya dereva bajaji yawe ya dhiki kila kukicha?
Serikali ndiyo mfadhili wao
  1. Tukisema PCCB wawatege na kuwakamata wanakwepa zitapigwa wote ni askari
  2. Tukisema serikali kuu iweke vituo maalumu vya ukaguzi vyenye camera haitaki
 
Pia kuna wale wanaokaa maeneo ya Kikwawila kama unatoka ifakara kwenda mikumi wale nao njaa kali sana. Umesikia habari ya yule aliegongwa na boda na kufa kule Mang'ula?
Hapana mkuu,huyo aliyegongwa na kufa sina cha kusema.
Wamezidi aisee hawa watu.!!
 
Kwa kuwa umeuliza maswali mawili basi Mimi najitolea kujibu swali la Kwanza.

Jibu NI kuwa "Hakuna mshahara unaotosha"
Kama mshahara hautoshi waende Mombasa kule kila kitu watapewa bure huku Ifakara wengi maisha yetu ni tiamajitiamaji.
 
Back
Top Bottom