Matukio na vituko ulivyokutana navyo kwa waganga wa kienyeji

GUSSIE

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2014
Posts
3,880
Reaction score
11,134
Tujuzane matukio au vitu tulivyoona au kukutana navyo kwa waganga wa jadi au Kienyeji vya kutisha na kuchekesha, Na hii itawafunza Wengine ambao wanategemea kwenda au ambao hawajui kinachoendelea huko

Mimi kama mwana siasa na mfanyabiashara haya mambo kuna wakati unataka kuyakwepa lakini kundi au crue inayokuzunguka kwa ushauri inakulazimu uisikilize

Tukio namba moja
Mwaka 2004 Katika harakati za kujiandaa na uchaguzi wa ubunge utakaofanyika 2005 washauri wangu wakaniambia Bwana mkubwa inabidi twende tukaangalie kama kutakuwa na kikwazo mbele yetu

Tukaamka asubuhi tukaelekea kwa Mzee wa makamo( Huyu ni Mganga ana wake wengi sana na pia anafuga mbuzi wa kutosha hapo nyumbani kwake, Ana mbuzi zaidi ya mia moja hapo kwake. Mzee anavalia barakashee na kanzu yake yenye Rangi ya kijivu fulani, Kufika tu pale kwake tulikuwa watu watatu mlangoni akatuambia nilijua mnakuja toka mbali sana, Na sasa mnatakiwa kuelezea ukweli bila kuficha kitu, Nikambonyeza mwezangu kwa kumkonyeza kuwa tusiongee bali yeye ndio atuambie tumefuata nini pale kwake kutokana na uzoefu wetu wa maeneo mengine, Mzee akachukua kitabu chake akawa kama anakisoma hivi huku anaandika lugha ambayo sisi tulikuwa hatuifahamu, Baadae akasema Nyie ni wanasiasa na mpo hapa kujua nini kitatokea mwakani kwenye kura za maoni, Kusikia hivyo tu nikasema moyoni oooho Yes that I need it,

Sasa ngoma ikaanza, Mganga akasema ili kuweza kuona vikwazo vyetu anahitaji mbuzi beberu kubwa lililoshiba na lenye nguvu na lazima beberu awe na Rangi nyeupe ambalo saa tisa usiku itabidi tuelekee Yeye na sisi baharini na mtubwi katikati ya Bahari tukamchinje huyo mbuzi beberu, Beberu atakapochinjwa inabidi asitikisike wala kupiga kelele, Akitikisika na kupiga kelele maana yake zoezi letu itabidi tuanze upya tena kutafuta beberu mwingine mweupe.

Nikafikiria Beberu natoa wapi, Nikamuuliza Mganga sasa Beberu namtoa wapi akasema ni wewe mwenyewe ukatafute au ununue hapa kwangu kwa wakati huo akataja beberu shilingi TZS 120,000.Nikamwambia nitakupa Jibu, Nikaenda soko la mbuzi nikakuta mbuzi wanauzwa TZS 50,000 mpaka TZS 70,000.Nikasema moyoni nanunua hapa mbuzi wawili wa TZS 60,000 @ mmoja wa mganga na mungine nachinja kwa ajili ya nyumbani kwangu kama kitoweo

Nikapeleka beberu nililonunua elfu 60,000 mweupe badala ya yule wa Mganga wa Tzs 120,000.

Sasa kindumbwe ndumbe ni huko baharini saa tisa za usiku nani ataenda kati ya sisi, Sisi wote hatujawahi kanyaga saa tisa za usiku katikati ya Bahari Halafu na mtubwi, Kwa uwoga wangu nikasema Jamaa zangu waende huko na Mganga Bahari kuchinja mbuzi, Mbuzi alichinjwa huko cha kushangaza alitikisika na kupiga kelele hivyo zoezi la kwanza likafeli ikatakiwa warudi Halafu tujipange upya kwa mbuzi mwingine

Baada ya zoezi kufeli Nikamwambia Mganga sasa labda nijaribu kununua mbuzi wako kwa TZS 120,000 kama anavyouza, Nikachagua beberu mweupe na zoezi likafanikiwa huko katikati ya Baharini kwa kutumia mbuzi anafuga Mganga, Hivyo ni kapata hasara ya mbuzi mmoja, Hata nyama ya mbuzi wote hao wawili baada ya zoezi sikukabidhiwa na Mganga

Swali ambalo najiuliza mpaka Leo wale mbuzi kwa Mganga ni mbuzi wa kawaida au ni viini macho

Swali jingine ambalo najiuliza ile nyama ya mbuzi baada ya zoezi anakula na familia yake au anaitupa, Maana mimi hakunipatia hata kipande cha nyama wala damu
 
Tatizo ulihadithiwa hukuenda mwenyewe ungeshuhudia kama alilia au hakulia kweli beberu wa mganga


Kukujibu jibu la mwisho ni ndio kuku , mbuzi mnazopeleka kwa mganga zinakuwa vitoeo hapa nyumbani

Otherwise itokee ile ya kufukia wakichinja au kufukia wakiwa wazima
 
Nilikuwa msaidizi wa Mchongo wa mganga huko moro [emoji3] raha niliyokuwa naipata akija dada mkali namkonyeza mganga kiujanja

Basi ataambiwa avue nguo asimame mbele ashike dawa baadae ageuke aendelee kushika dawa


Nilikuwa nakula video maana wateja wengi ni wanawake
 
Alooo
 
Niliwahi kutibiwa kwa mganga baada ya hosptal kushind8kana, mganga alisema nikae pale pale bila kuondoka nilikaa miez 3 mpka nikawa vizur.

Pale kwanza kulikua na wagonjwa wengi tu wanaokaa pale kwahyo kampan ilikuwa ya kutosha... yule mganga anatumia kuku kukutibu na ukitaka kuangaliwa kama umekaa sawa anatumia kuku, anamchinja kuku alafu anamuachia kuku,, huyo kuku atakimbia kimbia na kuruka ruka bila kichwa mpka atakapo tulia alafu yeye mganga anamuangalia yule kuku amelalaje, au kageukia wapi, kakunja miguu yote au mmoja kisha atapata jibu atakwambia..

me nilipotaka kuondoka tulifanya zoez hilo likafeli kuku kakunja miguu, nikaambiwa bado subir mpka alhmis ijayo tuangalie tena kama umekaa sawa yaan turudie kuchinja kuku[emoji849] wakati najiona nimepona kabsa.

Basi bana nashukuru nilipona lkn kuhusu kuku na nazi baada ya matumizi wanatumia kama chakula hapo kwake , pale kila siku mboga ni kuku alafu wali sasa hawapikii mafuta ni nazi tupu zile walizovunja.

Masharti ya pale kama ni balaa mfano ukiumwa hata kichwa hautakiwi kunywa panado unapelekwa kwenye mvuke wa dawa unachomwa yaan huo mvuke unavua nguo zote lazima chozi likutoke nilijihisi nipo jehanam,,,haitakiwi kukaanga vitunguu pale ni kosa kubwa sana mboga zao hazina vitunguu ,, mambo ni mengi sana
 
Aisee!
 
Real, That is your thought
 
Wewe Cha mtoto. Nilikua msaidizi wa mganga, siku moja kaja mdada nikamwambia mganga niachie huyu nimdhalilishe. Basi nikapiga ramli chonganishi na kugundua dada amewekewa hirizi kifuani ili asizae. Ikabidi niivute ile hirizi kwa kutumia mdomo wangu. Basi nikamwambia dada avue nguo za juu na sidiria. Nilimnyonya maziwa mpaka Basi.
 
Mi naomba namba ya hyo wa kweli
 
Aisee
 
Kwangu mpaka yanikute labda naweza kuamini huu ujinga.

Nina cases mbili za kuamini kwamba waganga ni waongo.

1: Hii ilikuwa 2015 bro alikuwa anagombea ubunge akanambia twende kwa mganga ukashuhudie uongo wao. Tulivyofika jamaa akaaza kupiga ramli zake na kuanza kuotea kwamba bro ni mfanya biashara mkubwa lakini ana matatizo kwenye biashara zake(hii ilitokana na muonekano wa brother Kwa Mimi nilivyodhani). Basi bro akakubali kwamba ni kweli na anapitia wakati mgumu kwenye biashara zake na mambo kibao.

Mganga akampa madawa lukuki tukaenda kuyatupa njiani na kampeni zikapigwa mwisho uchaguzi ukawa safi tu.

2: Kuna demu nilimpa mimba nikawa nahudumia vizuri tu lakini siku zilivyozidi kwenda akawa anazidisha kero mpaka nikakata tamaa nikawa nampa mahitaji ya msingi tu Kama Kodi ya nyumba, chakula nanunua mwenyewe na kuweka ndani, akiumwa natuma mtu ampeleke hospital na bills zote analipa huyo mtu. Kifupi nikawa simpi pesa kama mwanzo ila Nampa pesa kidogo kwa ajili ya emergence zake ndogondogo na kwake nikawa siendi Tena.

Alivyoona mambo yamekuwa tofauti akashauriwa aende kwa mganga. Akaenda huko sijui wapi kuangalia nini kimenibadilisha. Majibu yanakuja kwamba Mimi nimeoa na Nina watoto wawili huyo mwanamke wangu nimempangishia Mwanza na amegundua Kama nimempa mimba na Ninamuhudumia so ameniloga nimchukie

Akaanza kupambana na yeye kuniloga nimchukie huyo mke wangu na nimpende yeye Kama zamani. Kiuhalisia Mimi sijawahi kuoa Wala kumpa mtu mwingine mimba tofauti na yeye, huyo mtoto wake(kashajifungua) ndo mtoto wangu wa kwanza.
Nikasema kweli waganga wanakula pesa za watu kirahisi sana asee.
 
Mambo yangu ya kazini yalikuwa yamekaa vibaya sana fitina kama zote ..
Nuksi kila saa pesa haikai mfukoni.
Nikaingia Facebook nikatafuta tangazo la mganga nikapata nikamcheki mganga KMMK kumbe mganga tapeli akanitapeli kama 85000 hivi....

Sikukata tamaa nikasema hapana lazima nipate mtaalam basi kwenye jamii forums huku nikakutana na thread moja hivi jamaa naatoa ushuhuda jinsi mganga alivyomsaidia kusafisha AURA au nyota.
Nkampandia jamaa DM akanipa namba na maelekezo ya kwa mganga.

Kweli nikajiandaa nikaelekea kwa huyo mtaalam anakaa kwenye pori moja hivi huko ....
Jamaa ana wateja wengi balaa kiasi kwamba kuna daladala zinapiga route kwenda kwake wanapatia kanisani na hapo kwake kuna kituo kabisa cha daladala..
Kweli nikaenda nikafika pale nikachukua namba.

Nikapewa namba na msaidizi wake nikaonana na mganga akaniambia muda wa saa 6 ndo mwisho wa kusafisha nyota na mimi niliingia kilingeni saa 7 so akanipa dawa ya kuoga siku tatu nikaambiwa niende jumamoc.

Nikiwa pale nilipata muda wa kuona vingi sana cha kwanza pale katikati kuna jiwe lile jiwe likikanyagwa tu shughuli imeharibika siku hiyo wagonjwa wote mnarudi nyumbani.

Mwanamke akiingia bila kufunga kanga ndo hivyo shughuli imevurugika.

Mwanaume kavaa au kunyoa kihuni ndo hivyo kazi hamna.

So kuepuka inabidi pale nje tuwaelekeze kabisa wagonjwa wenzetu namna ya kuvaa na ku behave.

So jumamoc nikaenda kwa mtaalam sasa kusafisha nyota kama ilivyo ada nikiwa pale nje nasubiri ikanibidi nidodose kwa wenzangu vipi una nini na je mtaalam ni wa uhakika?

Jamaa wa kwanza akaniambia yeye ana case iko mahakamani ya kumtapeli boss wake million 550 ndo amekuja kwa mtaalam afanye manouvre hiyo case ifutike.

Mwingine alikuja kwenye machela kalogwa na mke mdogo.

Na case ziingine nyingi...

Mwisho wa siku nikaingia kwa mtaalam akanisafishia aura yangu akanipa na dawa za kuoga na masharti nikasepa zangu..


Kweli baada ya hapo kila kitu kikaa powa mambo yakarudi kama mwanzo kila kitu kikawa njema maisha yakaendelea kama kawaida.

Mtaalam nilimlipa sh 2000 tu
 
anakula
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…