Matukio ya Dada wa kazi kuwafanyia ukatili watoto wa maboss ikiwamo kuwaua nani alaumiwe?

Matukio ya Dada wa kazi kuwafanyia ukatili watoto wa maboss ikiwamo kuwaua nani alaumiwe?

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
3,925
Reaction score
8,853
Imeripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusu Mtoto aliyechinjwa na Dada wa kazi. Watu wanaishia kulalamika tu bila kutoa suluhisho ya kitu gani kifanyike kupunguza huu ukatili Mkubwa kwa watoto wasio na hatia.

Tumeshuhudia hivi karibuni kukamatwa haraka kwa kijana aliyechana picha ya Rais.

Kwa nini zisichukuliwe hatua za haraka kukinusuru kizazi kijacho.

Waziri Mwenye dhamana tunaomba hatua za haraka zichukuliwe ili wananchi waishi maisha ya furaha.

Nchi itapata vipi maendeleo kama wazazi wanafanya kazi kwa hofu wakiwaza usalama wa watoto nyumbani.

Ni kitu gani kinashindikana kuanzishwa au kuongeza taaluma ya mafunzo kwa dada wa kazi za nyumbani kwenye Vyuo vya Veta au kuwe na chuo maalumu cha mafunzo kwa ajili yao.

Hii itasaidia thamani yao kupanda lakini pia watafanya kazi kwa mikataba hata serikali itakuwa na takwimu za wadada wote na mahali walipo.

Hili suala haliumi hadi likufike wewe au mtu wa karibu yako.

Tunaomba serikali ichukue hatua za haraka kwa matukio haya ya kutisha kwa watoto wetu.

Mfumo mzuri wa upatikanaji wa Dada wa kazi nyumbani utasaidia kwa kiasi kikubwa sana kuliko sasa hivi wananchi wanaishi kwa hofu.

Dada wengi waliosomea mambo ya Hotel wako nyumbani kutokana na kukosa ajira, lakini kama wataongezewa taaluma ya kazi za nyumbani na mshahara ukawa mzuri kutokana na mikataba mizuri itasaidia Jamani.

Serikali mko wapi? Tunaomba mtusaidie.

Mwandishi wa Habari.
 
Hadi kupelekea dada wa Kazi kufanya ukatili sababu hua ni maboss wenyewe. Dada wa kazi wananyanyasika sana, na ukizingatia wengi wanakua ni wadogo kiumri Na wametoka mazingira duni

Kama manyanyaso yakizidi na akikosa watu wa kumpigania basi hapo tegemea kupokea payback kutoka kwake.

Shime kama una dada wa kazi nyumbani kwako ishi nae vizuri kama mwanao au tegemea kupatwa na tukio la kikatili utakalojutia maisha yako yote
 
Unamlipa elfu 30 ya masimango na manyanyaso kama mtumwa wako utegemee yeye akutendee wema.

Ni kweli serikali inapswa kuweka mkono wake hapo ila wananchi nasi tu wazinguaji sana.
Dada wa kazi umemtoa mpitumbwi huko wala hamjuani umeunganishwa tu na mtu usiyemjua ambae namba uneipata kwa rafiki wa rafiki yako.

Huyo dada ndo aje akuangalizie mtoto wako mdogo wa miaka miwili na mali zako wakati mwingine, huyo dada utamlipa 30-60k. Afanye kazi zote za hapo nyumbani.
Huku bosi ukijitetea kwa utetezi dhaifu ati anakula bure na kulala bure.

Wakati mwingine unatweza utu wa huyo dada kwa kumtamkia maneno makali mbele haya wageni, muonekano wake na mavazi yake kuukuu yanamtambulisha moja kwa moja kua huyo ni dada wa kazi.

Mkiwajali nao pia watawajali.
 
Hadi kupelekea dada wa Kazi kufanya ukatili sababu hua ni maboss wenyewe. Dada wa kazi wananyanyasika sana, na ukizingatia wengi wanakua ni wadogo kiumri Na wametoka mazingira duni...
Mfumo maalumu uwekwe kabisa jinsi ya kuwapata hawa wadada. Inatisha kumuachia mtoto mdada wa kazi usiyemjua alipotoka.
 
Imeripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusu Mtoto aliyechinjwa na Dada wa kazi. Watu wanaishia kulalamika tu bila kutoa suluhisho ya kitu gani kifanyike kupunguza huu ukatili Mkubwa kwa watoto wasio na hatia...
Mama wengi wana wanyanyasa Wadada wa kazi na pia Ujira wao wana wadhurumu na kuwafanyisha kazi ngumu!

Kuna familia zina wafanya kama part ya family na wana wapa Day off mara moja kwa wiki na awachelewi kuwapa pesa zao mwezi ukifika- na wana wapa atensheni wakiwa na shida etc!!

Kuna mijanamke Shetan anasubiri😭Hili ndo Tatizo- Tuwapende na kuwa jali house girl wetu
 
Imeripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusu Mtoto aliyechinjwa na Dada wa kazi. Watu wanaishia kulalamika tu bila kutoa suluhisho ya kitu gani kifanyike kupunguza huu ukatili Mkubwa kwa watoto wasio na hatia...
Acheni uvivu wa kijinga mlee watoto wenu.Kila kitu mnataka mfanyiwe na housemaids utadhani ninyi ni walemavu wa viungo vya miili na akili.

Matokeo yake mnaenda kuchukua wanafunzi mahiri wa ISIS wawalelee familia na kuwapeleka watoto wa miaka miwili shule za bweni.
 
Acheni uvivu wa kijinga mlee watoto wenu.Kila kitu mnataka mfanyiwe na housemaids utadhani ninyi ni walemavu wa viungo vya miili na akili.Matokeo yake mnaenda kuchukua wanafunzi mahiri wa ISIS wawalelee familia na kuwapeleka watoto wa miaka miwili shule za bweni.
Daaa inatishaa
 
Mama wengi wana wanyanyasa Wadada wa kazi na pia Ujira wao wana wadhurumu na kuwafanyisha kazi ngumu!

Kuna familia zina wafanya kama part ya family na wana wapa Day off mara moja kwa wiki na awachelewi kuwapa pesa zao mwezi ukifika- na wana wapa atensheni wakiwa na shida etc!!

Kuna mijanamke Shetan anasubiri😭Hili ndo Tatizo- Tuwapende na kuwa jali house girl wetu
Lakini hata nao unakuta ni wavivu sana
 
Huyo dada ana matatizo ya akili, hakuna sababu yeyote ya kuhalalisha mauaji ya mtoto mdogo.

Nakubaliana na wewe kuhusu kuanzishwa kwa taaluma ya dada wa kazi, hata huko mambele kuna nanny agencies, zinatoa mafunzo na kufanya uchunguzi kama huyo dada ana shida ya akili, madawa na vitu vingine....

Sema mabeki wasomi watakuwa ghali kwahiyo nadhani kila mtu awe makini anaajiri mtu wa namna gani.
 
Unamlipa elfu 30 ya masimango na manyanyaso kama mtumwa wako utegemee yeye akutendee wema.

Ni kweli serikali inapswa kuweka mkono wake hapo ila wananchi nasi tu wazinguaji sana.
Dada wa kazi umemtoa mpitumbwi huko wala hamjuani umeunganishwa tu na mtu usiyemjua ambae namba uneipata kwa rafiki wa rafiki yako.

Huyo dada ndo aje akuangalizie mtoto wako mdogo wa miaka miwili na mali zako wakati mwingine, huyo dada utamlipa 30-60k. Afanye kazi zote za hapo nyumbani.
Huku bosi ukijitetea kwa utetezi dhaifu ati anakula bure na kulala bure.

Wakati mwingine unatweza utu wa huyo dada kwa kumtamkia maneno makali mbele haya wageni, muonekano wake na mavazi yake kuukuu yanamtambulisha moja kwa moja kua huyo ni dada wa kazi.

Mkiwajali nao pia watawajali.
Mkuu ebu toa alternative, alipwe kias gani? Chukulia huyo boss wake ni mwalimu wa shule ya msingi ambaye mshahara wake hauzidi 410,000/=

Binafsi dada wa kazi regards kipato changu,siwezi kumlipa chini ya Elf 70.. tena mwezi ujao nimepanga nimuongezee iwe elf 80. Mtoto wa kisukuma anachapa kazi mnoo.
 
Achaneni nao.. house girls wote wanafanana tabia.
Hata uwe mwema vipi.

Ni kama wana laana fulani.

I have satisfied myself enough to come to this conclusion.
 
Mkuu ebu toa alternative, alipwe kias gani? Chukulia huyo boss wake ni mwalimu wa shule ya msingi ambaye mshahara wake hauzidi 410,000/=

Binafsi dada wa kazi regards kipato changu,siwezi kumlipa chini ya Elf 70.. tena mwezi ujao nimepanga nimuongezee iwe elf 80. Mtoto wa kisukuma anachapa kazi mnoo.
Walau wewe kidogo ila nje ya hiyo 70k hakikisha unaishi nae kama mwanao au ndgu yako.
Mpe mavazi na malazi anayopaswa kupewa binadamu.
Hiyo 70k iwe kama mnasaidiana maana kipato chako ni kidogo, na isiwe kama hilo ni donge nono analopawa kulitumikia kwa tabu.

Katika ukuaji wangu nimelelewa sana na hawa kina dada ila home katika udogo wangu sikujuaga ni wafanya kazi, ilikua ni dada dada dada, imagine siku hizi hata vitoto vidogo vinawanyanyapaa hawa kida dada na sababu kubwa ni wazazi kuwaona kama sio binadamu anaepaswa kuthaminiwa.
 
Hapa sasa inahitajika mavazi maalumu na nadhifu kwa ajili yake na kuthaminiwa pia
Wengi wanawaona kama sio watu aisee, hii kitu inauma acha tu.

Imagine familia nzima inakula chakula dining room halafu dada anasubiri wamalize halafu kama kitabaki na yeye ndo ale, kisipobaki atakula mkate kama upo au kama sio mvivu asonge kaugali au alale njaa asubiri kesho asubuhi.

Na wakikaliza kula aje atoe vyombo, bosi anakwambia halazi vyombo vichafu, inabidi aoshe wakati huo kala kidogo sana na hajashiba au hajala kabisa, bosi hajari.
Na kumbuka huyu ni binti asiezidi 18yrs, akimezeshwa sumu au siku akichoka, hakatafari ni kulipua tu.

Huyu mtu akikuulia mtoto unaita vyombo vya habari ukipiga nduru wakati muuaji umemjenga na kumvika mabomu mwenyewe.
 
Wengi wanawaona kama sio watu aisee, hii kitu inauma acha tu.

Imagine familia nzima inakula chakula dining room halafu dada anasubiri wamalize halafu kama kitabaki na yeye ndo ale, kisipobaki atakula mkate kama upo au kama sio mvivu asonge kaugali au alale njaa asubiri kesho asubuhi.

Na wakikaliza kula aje atoe vyombo, bosi anakwambia halazi vyombo vichafu, inabidi aoshe wakati huo kala kidogo sana na hajashiba au hajala kabisa, bosi hajari.
Na kumbuka huyu ni binti asiezidi 18yrs, akimezeshwa sumu au siku akichoka, hakatafari ni kulipua tu.

Huyu mtu akikuulia mtoto unaita vyombo vya habari ukipiga nduru wakati muuaji umemjenga na kumvika mabomu mwenyewe.
Hatari
 
Huyo dada ana matatizo ya akili, hakuna sababu yeyote ya kuhalalisha mauaji ya mtoto mdogo.

Nakubaliana na wewe kuhusu kuanzishwa kwa taaluma ya dada wa kazi, hata huko mambele kuna nanny agencies, zinatoa mafunzo na kufanya uchunguzi kama huyo dada ana shida ya akili, madawa na vitu vingine....

Sema mabeki wasomi watakuwa ghali kwahiyo nadhani kila mtu awe makini anaajiri mtu wa namna gani.
👏🏻👏🏻👏🏻
 
Back
Top Bottom