Matukio ya watu kupotea na kutekwa na 'watu wasiojulikana' kuendelea kuzua hofu kwa wananchi, nini sababu ya matukio haya?

Matukio ya watu kupotea na kutekwa na 'watu wasiojulikana' kuendelea kuzua hofu kwa wananchi, nini sababu ya matukio haya?

tukitaka kupambana na hili kwanza tufute fikra kuhusisha matukio ya aina hii na siasa

imani yangu ipo kwa vyombo vya ulinzi kikubwa ni kulisaidia jeshi
Jeshi halina na wala halitaki kabisa kujishughulisha na swala hili


MImi naamini siku moja tu ambayo Rais Samia ataagiza vyombo vyote viwatafute na kuwashughulikia wahusika. Basi swala hilo litaisha na kusahaulika kwa miaka mingi.

Lakini imani yangu hainipi kuona mwanga huo
 
Sababu kuu ni pale CCM inapoamini kwamba, nchi na wananchi ni mali yao waliyopewa na Mungu, na hivyo kuamini kwamba, wanaweza kuwashurutisha kukubaliana nao tu hata kwa mambo maovu, na wakati mwingine, ccm ni kama wanaamini kuwa, Mungu amewapa Watanzania wote kuwalinda na kuwachunga hata kwa fimbo ya chuma, na ndiyo maana utakuta, watu wakihoji kwa nguvu kuhusu rasilimali za nchi, katiba na mambo ya msingi katika nchi, wanapofanya tathimini, wao huona ni kama wananyang'anywa tonge mdomoni, wao huchukua jukumu la kuanza kuwapoteza watu hao

Mauwaji na utekaji ulioendelea sana nchini, kwa nchi yenye viongozi wenye kuthamini uhai wa watu, hili lisingeendelea kama ilivyo sasa!
Kwani huyo Mungu wanamwamini kama.yupo? Alishafutika kwenye akili zao.
 
Uoga unatokana na kwamba ukionekana na kaujasiri hata kidogo tu unafumuliwa ubongo wazi wazi ili na wengine wakome.

Ktk.mazingira kama.haya wasiojulikana wamepata mbinu konki ya kutulemaza
Uoga huo utaupata akiwa anatekwa mwanao?
 
Wananchi. wakichoka nao watawavizia huku mtaani.Wale wajuzi si wanetajwa wananchi wakichoka watawavuxia ama wawawekee sumu,wawapige au walogwe
 
Matukio ya kutekwa au kuteka (kidnaped or kidnaping) ni jambo linalohusisha kuingilia uhuru wa mtu kwa kumkamata pasipo kufata utaratibu wa kisheria na haki za kibinadamu katika nchi husika na kisha kwenda kumuweka au kumficha katika sehemu isiyo rasmi kisheria mfano nyumba za mateso, nyumba binafsi, misitu mikubwa, magofu yasiyo tumika n.k

Mambo ya kuteka au kutekwa hutokea dunia nzima, kuteka au kutekwa kunaweza kufanywa kwa njia ya siri/kujificha au kunaweza fanywa kwa uwazi au kuonekana mbele ya watu.

Zifuatazo ni sababu za kuteka au kutekwa duniani.

1. SIASA
Hii ni sababu kubwa ya kwanza inayopelekea mtu kuteka au kutekwa, hii inasababishwa hasa na mtazamo tofauti wa kisiasa mfano ni tofauti ya kimtazamo kati ya vyama viwili, kugombania ushawishi baina ya vyama viwili, kugombania madaraka baina ya vyama viwili n.k
Pia sababu za kisiasa inaweza kupelekea kuteka au kutekwa kwa kugombania nafasi ya uongozi baina viongozi wa chama kimoja cha kisiasa.
Asilimia kubwa nchini Tanzania matukio ya kutekwa au kuteka yanahusishwa na siasa mfano kutekwa kwa Ben Saanane, Kupotea kwa Azory, Kupigwa Risasi kwa Tundu Lissu n.k
Aina hii ya utekaji inatokea sana katika nchi zenye uchanga wa demokrasia au nchi zinazoendeshwa kwa mfumo wenye chembe chembe za utawala wa mabavu (dictatorship) na nyingi ya hizi nchi zinapatikana barani Afrika mfano ni Tanzania, Kenya, Nigeria, Afrika Kusini, DRC, Rwanda n.k
Pia sababu za kuteka au kutekwa kwa siasa inaweza kuwa baina ya nchi mbili kugombania aina fulani ya ushawishi katika nchi fulani au rasilimali fulani au soko la bidhaa fulani n.k
Mfano inaweza kuwa baina ya wanasiasa wa nchi ya Tanzania na nchi ya Rwanda au Marekani na nchi ya China n.k

2. UKOSEFU WA AJIRA
Hii inasababisha watu kujihusisha na matukio ya kuteka au kutekwa kwa lengo la kupata kipato, hii hufanywa na wahalifu na walengwa hasa wakiwa ni familia za watu wenye vipato vikubwa, familia za viongozi wenye pesa na madaraka n.k
Kuteka au kutekwa kwa njia hii kunatokea sana katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea mfano ni Marekani, Ulaya, Afrika n.k.
Pia aina hii ya kuteka au kutekwa kunaweza kuhusishwa na mhusika mwenyewe yani akajiteka mwenyewe kwa kudanganya kwa watu wake ili apate pesa.
Pia aina hii ya kuteka au kutekwa inawezafanywa na magenge ya kihalifu katika nchi husika, magenge hayo yanaweza kuwa ya kukodishwa kwa lengo la kutimiza aina fulani ya kusudio mfano kujipatia pesa, kulipa kisasi kwa sababu mbalimbali kama mahusiano ya kimapenzi, kifamilia, kitaifa na kimataifa n.k

3. DINI
Hii inapelekea kutekwa au kuteka kwa sababu ya mtazamo tofauti wa kidini au kidhehebu baina ya dini tofauti au dhehebu tofauti.
Kutekwa au kuteka kwa sababu ya kidini hutokea hasa kwa viongozi wa kidini wa dini husika au dhehebu husika.
Hii hutokea hasa endapo nchi moja au eneo moja linaushawishi mkubwa dini moja au dhehebu moja hivyo kwa dini nyingine au dhehebu lingine linapotaka kujiingiza katika hio nchi au eneo hilo hukumbana na matukio ya aina tofauti ya upinzani ikiwemo kuteka au kutekwa, vifo n.k
Matukio haya hutokea sana katika nchi zenye msimamo mkali wa kidini kama nchi za Kiarabu kama Irani, Saudi Arabia, Libya n.k
Pia nchi kama India na China zimeonesha matukio ya aina hiyo kwa kutofautiana mtazamo na dini ya kiislamu katika maeneo mengi ya nchi zao.
Kuteka au kutekwa kwa njia ya kidini kunaweza sababishwa pia kwa kutokea mtazamo tofauti kati ya viongozi wa kidini na viongozi wa kisiasa.

Sababu zingine ni
4. UMASKINI
5. CHUKI
6. RUSHWA
7. UKOSEFU WA ELIMU NA UJINGA n.k
 
Hahaha......mzee naomba nisicomment.
Elimu ya uraia itolewe kwa wananchi,
Serikali iwe na kipao mbele juu raia wake , waone thamani ya ria wake kama nchi ya izaeli,marekani, nk Tanzania raia ni thamani ya kuku, watu wanakuwa, sekalali hachui hatua yoyote
Viongozi wote mpaka raisi inatakiwa wawe wazalendo ,matendo yao yaonekane kuwa ni wazalendo.

Viongozi wa dini wakemee matendo maovu, bila kujali nani anafanya.
 
Hahaha......mzee naomba nisicomment.
Elimu ya uraia itolewe kwa wananchi,
Serikali iwe na kipao mbele juu raia wake , waone thamani ya ria wake kama nchi ya izaeli,marekani, nk Tanzania raia ni thamani ya kuku, watu wanakuwa, sekalali hachui hatua yoyote
Viongozi wote mpaka raisi inatakiwa wawe wazalendo ,matendo yao yaonekane kuwa ni wazalendo.

Viongozi wa dini wakemee matendo maovu, bila kujali nani anafanya.
 
Kama litazungumziwa bungeni kama dharula, tatizo linaweza kuisha.
Tatizo hatuna bunge,yule mwovu alituachia genge vilaza wa CCM ambao utii wao ni kwa dola iliyowaweka hapo,laiti tungekuwa na bunge halisi yaani wawakilishi wa wananchi waliopelekwa hapo kwa kura wangewajibika kwa wapiga kura wao,na kwa dalili za hiki kinachoendelea kwenye mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakati tutakuwa na genge lingine la wahuni wa CCM.
 
Watawala tu wanashindana kutawala na kuhujumiana

Hivyo wanawatoa kafara raia na wanasiasa wasio na impact kubwa kwenye jamii!!

Kiufupi ni mwelekeo wa siasa za uchaguzi 2025-2030

Naamini kabisa Samia na Magufuli hawakuwa wahusika Wakuu wa utekaji Ila kila mtu kwa wakati wake amehujumiwa

Siasa chafu za nchi hii zilianza mwaka 2010 baada ya lowassa kuwa ashajizulu sita kanyimwa usipika kurudi

2015 zikapaliliwa zaidi baada ya Lowassa kukatwa na January makamba kunyimwa uwaziri mkuu!!

Makunndi ndani ya ccm ndio yanaumiza wananchi!!

Bila kufanya reform angalau ya kukipumzisha hiki chama kijipange upya nchi hii haitakaa itulie.

Kila mtu anajiona anawezakuwa Rais so anahujumu utawala uliopo ili yeye apate njia

Hivyo wananchi wanatumika na kuumia na kuwa mbuzi wa kafara!!

Cha kufanya ni kufyeka makundi ndani ya ccm
 
Elimu ya uraia itolewe kwa wananchi,
Serikali iwe na kipao mbele juu raia wake , waone thamani ya ria wake kama nchi ya izaeli,marekani, nk Tanzania raia ni thamani ya kuku, watu wanakuwa, sekalali hachui hatua yoyote
Viongozi wote mpaka raisi inatakiwa wawe wazalendo ,matendo yao yaonekane kuwa ni wazalendo.

Viongozi wa dini wakemee matendo maovu, bila kujali nani anafanya.
Kwenye Elimu ya uraia kenya wametupita mbali mno.
 
Kwani huyo Mungu wanamwamini kama.yupo? Alishafutika kwenye akili zao.
Wanajua yupo vizuri tu, ila hawatambui kama huyo Mungu, kazi ya kuhukumu ni yake yeye, wao wanaamini kuhukumu ni kazi yao na ndoyo maana wanateka
 
Lawama nyingi kwa jeshi la polisi ni halali. Hawa ndiyo wanayo yafanya haya kama wao wapo juu ya sheria. Hata wanapo mkamata mtuhumiwa vitisho vingi ambvyo havina hata msingi. Wanajuwa utamfanya nini hawa ndiyowabaya wameanza kwa wauza gongo wamenogewa sasa kwa yeyote aliye mbele yake
 
Back
Top Bottom