Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi la Watu kupotea katika mazingira ya kutatanisha hasa ya Vijana wenzetu.

Yalianza mdogomdogo lakini kadiri siku zinavyozidi Kwenda mbele kumekuwa na taarifa za hapa na pale kuhusu fulani na fulani kupotea, binafsi nimeanza kupata hofu licha ya kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likitoa kauli flani za kuonesha hakuna kitu kibaya.

Hivi nini kinaendelea?
Unajua hizi mambo za matukio ya “kutisha” tulishaanza kuyasahau lakini yameanza kurejea.

Hivi karibuni tumeona baadhi ya Vyombo vya Habari na Mitandao ikizungumza kuhusu yule Sativa alivyopotea na kupatikana akiwa amechakazwa kwa kujeruhiwa vibaya.

Kiukweli sisi Wananchi tunaumizwa na kutishwa na hali inayoendelea kwasasa. Imefika hatua tunaanza kuogopa hata kukutana na watu tusiowafahamu huku mitaani.

Soma Pia: Freeman Mbowe: Viongozi wa CHADEMA na Watanzania wasio na Vyama wanaoendelea kutekwa na Vyombo vya Usalama vya Nchi yetu


Tunaomba Mamlaka zikomeshe haya matukio kwakuwa yanatishia usalama wetu, yanachafua taswira ya nchi yetu kitaifa na kimataifa. Pia, huu sio utamaduni wetu Watanzania.

Pia soma ~ Vijana Kariakoo wanapotea sana, Serikali iingilie kati
 
Bad thing jeshi la polisi linahusishwa kwa karibu na matukio hayo, na hakuna investigation inaganyika zidi yao
 
Matukio haya kwakweli yanasikitisha sana na hata kuanza kuogopesha baadhi ya raia hapa Nchini, mimi mwenyewe nina mdogo wangu (-) ambaye kwa sasa ni marehemu na tumemzika Ijumaa iliyopita mnamo tarehe 05/07/2024 ambaye alipotea tokea siku ya Ijumanne iliyopita mnamo tarehe 02/07/2024 mkoani Kagera na amekuja kupatikana siku ya Alhamis ya tarehe 04/07/2024 akiwa ameshafariki. Mwili wake ukiwa umetelekezwa ziwani hali ya kuwa akionekana kuwa alinyongwa kabla ya kufikwa na umauti.
 
Matukio haya kwakweli yanasikitisha sana na hata kuanza kuogopesha baadhi ya raia hapa Nchini, mimi mwenyewe nina mdogo wangu (-) ambaye kwa sasa ni marehemu na tumemzika Ijumaa iliyopita mnamo tarehe 05/07/2024 ambaye alipotea tokea siku ya Ijumanne iliyopita mnamo tarehe 02/07/2024 mkoani Kagera na amekuja kupatikana siku ya Alhamis ya tarehe 04/07/2024 akiwa ameshafariki. Mwili wake ukiwa umetelekezwa ziwani hali ya kuwa akionekana kuwa alinyongwa kabla ya kufikwa na umauti.
Poleni sana mkuu.
 
Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi la Watu kupotea katika mazingira ya kutatanisha hasa ya Vijana wenzetu.

Yalianza mdogomdogo lakini kadiri siku zinavyozidi Kwenda mbele kumekuwa na taarifa za hapa na pale kuhusu fulani na fulani kupotea, binafsi nimeanza kupata hofu licha ya kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likitoa kauli flani za kuonesha hakuna kitu kibaya.

Hivi nini kinaendelea?
Unajua hizi mambo za matukio ya “kutisha” tulishaanza kuyasahau lakini yameanza kurejea.

Hivi karibuni tumeona baadhi ya Vyombo vya Habari na Mitandao ikizungumza kuhusu yule Sativa alivyopotea na kupatikana akiwa amechakazwa kwa kujeruhiwa vibaya.

Kiukweli sisi Wananchi tunaumizwa na kutishwa na hali inayoendelea kwasasa. Imefika hatua tunaanza kuogopa hata kukutana na watu tusiowafahamu huku mitaani.

Tunaomba Mamlaka zikomeshe haya matukio kwakuwa yanatishia usalama wetu, yanachafua taswira ya nchi yetu kitaifa na kimataifa. Pia, huu sio utamaduni wetu Watanzania.

Pia soma ~ Vijana Kariakoo wanapotea sana, Serikali iingilie kati
Usalama mkubwa ukiwa busy na shughuli za maendeleo kuliko kutukana viongozi
 
Kuna nn Nyuma ya utekwaji WA watu na Ongezeko la ULAWITI kwenye jamii ?
t9a2dk.jpg
 
Kwa nini hizo taarifa za kuripotiwa kupotea zinazosambaa ni za wanaume tu?

Tangu nimeanza kusikia au kuona mfululizo wa taarifa za kupotea kwa watu wazima ni wanaume tu! Sijaona wanawake wakidaiwa kupotea.
 
Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi la Watu kupotea katika mazingira ya kutatanisha hasa ya Vijana wenzetu.

Yalianza mdogomdogo lakini kadiri siku zinavyozidi Kwenda mbele kumekuwa na taarifa za hapa na pale kuhusu fulani na fulani kupotea, binafsi nimeanza kupata hofu licha ya kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likitoa kauli flani za kuonesha hakuna kitu kibaya.

Hivi nini kinaendelea?
Unajua hizi mambo za matukio ya “kutisha” tulishaanza kuyasahau lakini yameanza kurejea.

Hivi karibuni tumeona baadhi ya Vyombo vya Habari na Mitandao ikizungumza kuhusu yule Sativa alivyopotea na kupatikana akiwa amechakazwa kwa kujeruhiwa vibaya.

Kiukweli sisi Wananchi tunaumizwa na kutishwa na hali inayoendelea kwasasa. Imefika hatua tunaanza kuogopa hata kukutana na watu tusiowafahamu huku mitaani.

Soma Pia: Freeman Mbowe: Viongozi wa CHADEMA na Watanzania wasio na Vyama wanaoendelea kutekwa na Vyombo vya Usalama vya Nchi yetu

Tunaomba Mamlaka zikomeshe haya matukio kwakuwa yanatishia usalama wetu, yanachafua taswira ya nchi yetu kitaifa na kimataifa. Pia, huu sio utamaduni wetu Watanzania.

Pia soma ~ Vijana Kariakoo wanapotea sana, Serikali iingilie kati
labda ni wale freedom fighters
 
Back
Top Bottom